Posts

Showing posts from August 5, 2020

Jolly Twins – Uweponi Mwako (Official Video)

Image
Ukitaja miongoni mwa waimbaji wanaofanya vizuri kwa sasa ndani ya Gospel Tanzania huwezi kuwaacha Jolly Twins ambao awali waliotoa wimbo wao na Godluck Gozbert ‘Baba eeeh’ ambao ulifanya vizuri. Leo August 5, 2020 wametuletea ‘Uweponi mwako’  imetayarishwa nchini Australi ambapo ndipo wanaishi karibu kuitazama. NancyTheDreamtz

JPM Akichukua Fomu NEC, Wasanii 109 Kukesha Uhuru Stadium – Video

Image
MGOMBEA Urais kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika uchaguzi Mkuu wa 2020, Dkt. John Pombe Magufuli atachukua Fomu ya Kugombea Urais wiki hii katika ofisi za Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC)  jijini Dodoma.   Hayo yamesemwa leo Jumatano, Agosti 5, 2020 na Katibu wa Itikadi na Uenezi (CCM), Humphrey  Polepole wakati akizungumza na vyombo vya habari katika  Ofisi Ndogo ya Makao Makuu ya CCM (OND) Lumumba Jijini Dar es Salaam.  “NEC imetutangazia kuanzia leo tunaweza kuchukua fomu kwa ajili ya wagombea wa nafasi ya urais. Mwenyekiti wetu na Rais wetu ambaye pia ni mgombea urais kupitia chama chetu, Dkt. John Magufuli atachukua fomu wiki hii NEC, Dodoma akiomba dhamana ili akafanye makubwa zaidi kwenye muhula wa pili. Nitawaambia ni siku gani atachukua.   “Kampeni tutakazozifanya mwaka huu zitakuwa ni bora zaidi na zitakuwa za kisayansi. Kwa mujibu wa tafiti tuliyoifanya mwezi Juni mwaka huu, tunaingia kwenye uchaguzi tukiwa na mtaji wa wapiga kura milioni 16.8, amba

Yanga Yajifungia Hotelini, Kumsajili Hassan Kessy wa Nkana

Image
KAMPUNI ya GSM iliyochukua jukumu la usajili Yanga kwenye msimu ujao, imemuwekea kitita cha Sh 50Mil, beki wa pembeni wa Nkana Rangers ya Zambia, Hassan Kessy.   Beki huyo ni kati ya wachezaji wanaowaniwa na Yanga katika kuiimarisha safu ya ulinzi ya kulia pamoja na beki wa KMC, Kelvin Kijiri ambaye klabu yake inahitaji Sh 60Mil ili imuachie kutokana na kubakisha mwaka mmoja katika mkataba wake. Yanga hivi sasa ipo kwenye mipango ya kukisuka kikosi chao baada ya juzi kutangaza kuachana na wachezaji wake 14 wakiwemo mastaa Papy Tshishimbi, David Molinga, Mrisho Ngassa na Issa Mohammed ‘Banka’.   Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumatano, uongozi wa Yanga kwa kushirikiana na GSM wamemuita beki huyo juzi Jumapili usiku na kukaa naye mezani kwa ajili ya kufanya mazungumzo ambayo yalishindwa kufikia sehemu mzuri kutokana na dau kubwa ambalo amelitaka. Mtoa taarifa huyo alisema kuwa beki huyo ametaka kitita cha Sh 60Mil kabla ya kupunguza kufikia Sh 55Mil kabla ya viongozi ha

Magufuli Kuchukua Fomu NEC Kesho Mapemaa!

Image
MGOMBEA Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dkt. John Pombe Joseph Maguful ata chukua fomu ya kugombea Urais kesho Alhamisi tarehe 6 Agosti saa 3:00 Asubuhi Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) Jijini Dodoma. NancyTheDreamtz

Straika Mpya Yanga Aitisha Simba

Image
MSHAMBULIAJI mpya wa kikosi cha Yanga, Waziri Junior ametamba kuwa ametua ndani ya klabu hiyo ili kumaliza utawala wa muda mrefu wa Simba na mshambuliaji wao Meddie Kagere.   Waziri ambaye msimu wa 2019/20 aliibuka mfungaji bora wa klabu ya Mbao baada ya kutupia mabao 13 alitambulishwa rasmi ndani ya Yanga siku ya Jumapili jioni baada ya kukamilisha usajili wake na kusaini mkataba wa miaka miwili.   Akizungumza na Championi Jumatano, Waziri ambaye anatajwa kuwa kati ya washambuliaji mahiri alisema licha ya kutambua kuwa haitakuwa kazi rahisi kufanikisha hilo lakini amejipanga na anaamini ataweza kulifanikisha.   “Tangu mwaka 2015, nilipoanza rasmi kucheza Ligi Kuu Bara kwenye klabu ya Toto Africans ndoto yangu ilikuwa ni kumaliza msimu nikiwa mfungaji bora, nashukuru Mungu kwa kuweza kukamilisha usajili wa kujiunga na Yanga kwani sasa ninaona dhahiri kuwa nipo karibu kukamilisha malengo hayo.   “Najua haitakuwa kazi rahisi kutokana na uwepo wa washambuliaji wengi bora kama, Meddie Kage

Video Vixen Wamewaponza!

Image
K UMEKUWA  na kasumba ambayo inawaandama sana mastaa wa muziki hapa Bongo. Hii imesababisha baadhi ya mastaa waponzwe na warembo hao, kwani watu wamekuwa wakiona tu picha za video wakiwa pamoja, basi wanajiongeza kwa kusema walikuwa wapenzi. Japo nyingine zinaweza kuwa ni uvumi lakini wapo wanamuziki waliofanya kweli kwa video vixen hao. Makala haya yanakuletea orodha ya wanamuziki wakubwa ambao wamewahi kuhusishwa katika ishu hizo: DIAMOND-HAMISA Mwanamuziki mkubwa Afrika Mashariki, Nasib Abdul ‘Diamond Platnumz’ na mzazi mwenza wake Hamisa Mobeto ambaye alionekana katika video mbili ya Nataka Kulewa na Salome. Licha ya kuwa video vixen, wawili hao walikuwa wapenzi na kufanikiwa kuzaa mtoto mmoja. DIAMOND-TUNDA Anastazia Sebastian almaarufu kama Tunda, aliwahi kutoka kimapenzi na Diamond Platnumz ikiwa ni baada ya kuonekana katika wimbo wa Salome. Japo wawili hao walificha, habari zikasambaa baada ya video yao kuvuja. KIBA- HAMISA Mfalme wa Bongo Fleva na Bosi wa Lebo ya King’s Music

Minu: Nitakuwa Mjinga Nispomuoa Snura

Image
Mpenzi wa mwanamuziki wa Singeli nchini, Snura Mushi, Minhal azad ‘Minu’ amesema kuwa hatakuwa mjinga aliyepitiliza kama atamuoa mpenzi wake huyo kwasababu ni mwanamke mwenye busara na anafaa kuwa mama wa familia yake. Akizungumza na Risasi Jumatano, Minu alisema kuwa tanu ameanza uhusiano na Snura, ameweza kubadilisha sana maisha yake kutokana  na uelewa mkubwa wa aliokuwepo nao, tofauti kabisa na uhusiano mwingine wowote aliowahi kupitia,hivyo kwake mwanamuziki huyo anatosha. “ Nitachekwa na kuonekana mjinga sana kama nisipofanya maamuzi sahihi ya kumuoa Snura, yaani kwangu ametosheleza kila kitu na busara zake kwangu ndio msingi mkubwa sana yaani kiufupi ni mwanamke wa kuoa” alisema Minu. NancyTheDreamtz

Polepole: CHADEMA Imemdhulumu TID ‘Ni Yeye’

Image
KATIBU wa Itikadi na Uenezi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) amesema kuwa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) wamemzulumu mwanamuziki TID kwa kutumia kaulimbiu aliyoibuni ‘Ni Yeye’ bila kumshirikisha.   Akizungumza na waandishi wa Habari jijini Dar es Salaam Humphrey Polepole ameeleza kuwa kitendo hicho hakikubali na kwamba Watanzania watakichukulia hatua chama hicho cha upinzani.   “Nampa pole TID sababu hawa majamaa ni mazulumati wametudhulumu wimbo wa Taifa. TID anapambana mtu wa watu ametengeneza Ni Yeye na ile ilikuwa Magufuli, wale majamaa wameichomeka kule. Hawajamshirikisha hawajamuomba kwa kweli sisi kama Watanzania tutawachukulia hatua,” ameeeleza Polepole.   Katika hatua nyingine ameeleza kuwa Rais Dkt. Magufuli ambaye ni mgombea wa CCM atachukua fomu ya uteuzi wa kugombea Urais wa Tanzania wiki hii jijini Dodoma, lakini hakutaja siku ya tukio hilo.   Aidha, amesema Agosti 15 mwaka huu chama hicho kitakutana na wasanii zaidi ya 109 pamoja na bendi katika Uwanja wa Uhuru,

Alikiba: Nilimuomba Rais Magufuli kitu na anaweza kuwepo kwenye mchezo wetu na Samatta, anatukubali sana

Image
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Alikiba leo an Samatta wamezindua rasmi mchezo wao na Samatta ikiwa ni muendelezo wa project yao ya Samakiba Foundation ambapo kila mwaka hucheza mchezo rasmi kwa ajili ya kuchangia sekta ya Elimu. Wakizindua leo Alikiba amesema kuwa tayari wameanza kufanya kazi na wizara ya Elimu kutokana na juhudi zao za kuchangia sekta hiyo. Mbali na hilo Alikiba amethibitisha kuwa aliongea na Mh. Rais  Magufuli na huenda akawepo kwenye mchezo wao na Samatta ambao utachezwa tarehe 8/8/2020 uwanja wa Mkapa jijini Dar Es Salaam. NancyTheDreamtz

Ni muda wa kudondosha hit nyingine- Diamond

Image
Mkali wa Bongo Fleva anaeendelea kuteka vichwa vya habari ndani na nje ya nchi , Zuchu , ameonesha dalili kuwa Muda wowote kuanzia hivi sasa , atawadondoshea Mashabiki zake ngoma mpya . Kupitia ukurasa wake wa Instagram , imesomeka “comment “ ya CEO wa WCB Diamond Platnumz ikiesema kuwa sasa ni Muda wa Malkia huyo kuachia Kazi mpya . Kupitia ujumbe huo , SIMBA Diamond Platnumz ameandika “It’s Time to Drop another Hit Zulu” , akimaanisha kuwa sasa ni Muda muafaka wa kudondosha HIT mpya Mjini . NancyTheDreamtz

Eymael Aigomea Adhabu ya TFF, Asema Aipo Kisheria

Image
ALIYEKUWA kocha mkuu wa klabu ya soka ya Yanga, Luc Eymael amesema kuwa hakubaliani na adhabu iliyotolewa na Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) ya kumfungia miaka miwili na kumtaka alipe faini ya Shilingi Milioni 8 kutokana na adhabu hiyo kukiuka taratibu za kisheria ikiwamo kutotoa nafasi ya yeye kujitetea.   Eymael hivi karibuni aliingia matatani baada ya kutoa kauli zilizotafsiriwa kuwa ni za kibaguzi baada ya mchezo wao dhidi ya Lipuli.   Akizungumza na Championi Jumatano kutokea nchini Ubelgiji, kocha Luc alisema taarifa za kufungiwa kwake hazijafikishwa kwa taarifa rasmi. “Kwanza niseme kuwa sijapokea taarifa yoyote rasmi kutoka kwa uongozi wa Shirikisho la soka la Tanzania (TFF), kuhusu adhabu ya kunifungia na kulipa faini, hata mimi nimekuwa nikiziona taarifa hizo kupitia mitandao.   “Lakini suala jingine ambalo ndilo kubwa zaidi ni kwamba adhabu hii imetolewa bila kunipa nafasi ya kujitetea kitu ambacho kisheria ilikuwa haki yangu na wakili wangu aliwasilisha maombi hayo, hivyo