Posts

Showing posts from September 25, 2018

Papa Francis awatambua na kuwaridhia maaskofu saba walioteuliwa China

Image
NancyTheDreamtz Makao makuu ya Kanisa Katoliki, Vatican na China zimetangaza juu ya kutiwa saini mkataba wa kihistoria, wa muda mfupi uliofikiwa kati ya pande hizo mbili kuhusu uteuzi wa maaskofu nchini China. Papa Francis amekubali uhalali wa maaskofu saba wa China, walioteuliwa na China bila idhini ya Vatican. Hatua hiyo imemaliza mzozo wa kidiplomasia uliokuwepo kwa miongo kadhaa na ambao umesababisha mgawanyiko miongoni mwa waumini wa Kikatoliki nchini China. Ni miongo saba sasa tokea Vatican na China zikate mahuasiano rasmi kati yao. Uamuzi huo ni sehemu ya makubaliano ya kihistoria kati ya Kanisa Katoliki na China juu ya uteuzi wa maaskofu, jukumu ambalo kwa kawaida huwa la Papa. Mkataba huo wa muda ulisainiwa mjini Beijing na kutangazwa wakati Papa Francis alipokuwa anafanya ziara nchini Lithuania ikiwa ni mwanzoni mwa safari yake ya siku nne katika mataifa yanayoizunguka bahari ya Baltic, kaskazini mwa Bara la Ulaya. Kwa mujibu wa taarifa kutoka Vatican, Papa Franc

Sitaki kuolewa tena na kijana, nataka mwanaume mzungu aliyeachika – Hamisa Mobetto

Image
NancyTheDreamtz Mwanamitindo Hamisa Mobetto ameamua kuweka wazi mwanaume ambaye anataka kuishi naye kwa sasa, ambapo amedai kuwa anataka mwanaume wa kizungu ambaye alishawahi kuachika na mwenye watoto. Hamisa Mobetto Akizungumzia vigezo vya mwanaume anayemtaka, Hamisa amesema kuwa kwa sasa hapendi kuolewa na vijana na anatafuta Mzungu mwenye umri mkubwa kuanzia miaka 45. “ Mimi hapa nataka labda mzungu au mtu mzima,  awe alishawaki kuachwa au Mgane kwa hiyo ndio hivyo, yaani nikisema kijana dah hapana. Awe angalau miaka 45 kwa sababu mimi mwenyewe nina watoto sasa ukisema kijana yeye mwenyewe bado anakua atawezaje kulea watoto wangu, “amesema Hamisa Mobetto kupitia EATV. Hamisa Mobetto tayari ameshazaa watoto wawili na wanaume wawili tofauti tofauti, ambao ni Diamond Platnumz na Majizzo na amesema kwa sasa hawezi kurudiana na yeyote kati yao. Kwa upande mwingine, Hamisa Mobetto amekiri kuwa sauti iliyosambaa mitandaoni wiki mbili zilizopita akiongea na Mganga wa kienyeji ili

Wamiliki wa Blog ya Dauda.com waachiwa kwa dhamana Mahakama ya Kisutu

Image
NancyTheDreamtz Wamilikiwa wa blog ya Dauda.com  wameachiwa kwa dhamana na Mahakama ya Mkazi Kisutu ambao ni pamoja na mtangazaji wa Clouds fm Shaffih Dauda. Wawili hao wanatuhimiwa kwa kosa la kuendesha blogs bila kuwa na kibali. Licha ya Kesi hiyo imehairishwa mpaka tarehe 8 mwezi wa kumi,washtakiwa hao walikataa tuhuma hizo za kumiliki blog bila kuwa na kibali. Wakili wa upande wa Jamhuri ameiomba Mahakama kuhairisha shauri hilo mpaka pale upelelezi utakapokamilika, na kwa Wakili wa upande wa utetezi Jebra Kambone ameiomba Mahakama kuwapa dhamana wateja wake kwa kuwa haki ya kupata dhamana ipo na Hakimu wa kesi hiyo amekubali kuwapa dhamana washtakiwa hao. Shafiih na wenzake ambaye anashikiliwa ni Ben Ali (Ben On Air) ambaye alikuwa muendeshaji wa Dauda TV kupitia mtandao wa (Youtube) walikamatwa wiki iliyopita kwa kosa la kuendesha blog hiyo bila kuwa na kibali kutoka TCRA.

Afya ya Haji Manara yatetereka, mwenyewe adai amelishwa sumu na sio presha ya matokeo ya Simba

Image
NancyTheDreamtz Baada ya taarifa kusambaa mitandaoni kuwa Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara ameshikwa na presha iliyopelekea kulazwa mkoani Shinyanga, hatimaye mwenyewe aweka wazi kinachomsumbua. Haji Manara Manara amesema kuwa alikula chakula chenye sumu, na ndio sababu iliyompelekea kulazwa na sio presha ya matokeo mabaya ya klabu yake kama inavyoandikwa mitandaoni. “ Siumwi pressure wala moyo kama inavyoandikwa mitandaoni..nahic nimepata food poisoning na niwashukuru Madaktari walionihudumia awali Shinyanga na Mwanza ..now nisharejea Dar teyari kwa vipimo zaidi…Insha’Allah kila kitu kitazidi kuwa salama, “ameeleza Haji Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram. Klabu ya Simba imekuwa na matokeo mabovu kwa msimu huu ambapo wiki iliyopita imepokea kichapo cha goli 1 dhidi ya Mbao FC ya Mwanza.

Wanaharakati hawa watatu watunukiwa tuzo mbadala ya Nobel wakiwa Jela

Image
NancyTheDreamtz Wanaharakati watatu wa haki za binadamu kutoka Saudia walioko jela watunukiwa tuzo mbadala ya Nobel na taasisi ya Nobel mjini Stolkholm.Pia wapinga rushwa kutoka Guatemala watunukiwa tuzo ya heshima. Washindi wa tuzo maalum ya haki za binadamu au tuzo mbadala ya Nobel wametangazwa leo hii mjini Stolkholm Sweden. Tuzo hiyo imetunukiwa watetezi watatu wa haki za binadamu wakisaudi waliofungwa jela pamoja na wanaharakati wa kupinga rushwa kutoka Amerika Kusini. Taasisi ya tuzo hiyo mjini Stolkholm imesema dolla 113,400 zinazoambatana na tuzo hiyo mbadala ya Nobel zitagawanywa kwa washindi Abdullah al Hamid,Mohammad al-Qahtani na Waleed Abu al Khair wote wa Saudi Arabia kutokana na juhudi zao za kijasiri zinazosimamia misingi ya haki za binadamu ya kimataifa,ili kuleta mageuzi katika mfumo wa kidhalimu wa kisiasa nchini Saudi Arabia. Tuzo  ya heshima ya mwaka huu imetunukiwa Thelma Aldana wa Guatemala na mkolombia Ivan Velasquez kutokana na mchango wao mkubwa katik

Maua Sama na Soudy Brown kuendelea kusota mahabusu (Audio)

Image
NancyTheDreamtz Mwanamuziki Maua Sama Jumatatu hii hajapandishwa mahakamani kama ilivyotarajiwa na wadau wengi huku wenzake Soudy Brown akipandishwa mahakamini na kusomewa shtaka moja la kutumia mitandao ya kijamii bila kuwa na kibali. Wawili hao kwa pamoja walikamatwa na jeshi la polisi wiki iliyopita kwa tuhuma za kuidhalilisha nembo ya Taifa baada ya kupost video moja mtandaoni inayowaonyesha watu wakichezea hela za Tanzania. SoudyBrown amesomewa shtaka moja la kuweka maudhui mtandaoni bila kuwa na kibali lakini dhamana ya kosa hilo iko wazi lakini anadaiwa bado anashikiliwa na jeshi la polisi kwa kuwa ana kesi nyingine ya kujibu. Hakimu anayeisikiliza kesi hiyo Augustine Rwizile ameghailisha kesi hiyo hadi 18 October 2018. Naye Maua Sama hakuletwa mahakamani leo kama watu walivyotarajia huku wadau wa mambo wakidai kesi yake nitaanza kusikilizwa katikati ya wiki hii. Mmmoja kati ya mawakili ambao walijitokeza mahakamani hapo walidai wamewasiliana na jeshi la polis

Hamisa Mobetto atua Kenya na kupokewa mchekeshaji huyu (Audio)

Image
NancyTheDreamtz Mwanadada Hamisa Mobetto Jumatatu hii ametua nchini Kenya na kupokelewa na mchekeshaji, ChipuKeezy ambaye kwa sasa anaendesha kipindi kimoja cha TV nchini humo. Hatua hiyo ni siku moja toka Diamond ampost mama watoto wake wa zamani Zari na kueleza kwanini hawezi kuanika mambo ya Zari mtandaoni tofauti alivyofanya kwa Mobetto. Wawili hao waliingia kwenye mgogoro wa kutupiana maneno toka Diamond anyake sauti ya Mobetto akizungumza na mtu anayedaiwa kuwa ni mganga wa kienyeji. Rel

Huyu ndio mrithi mpya wa Zari na Hamisa Mobetto kwa Diamond Platnumz ? (Audio)

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa muziki wa kizazi kipya na C.E.O wa lebo ya muziki ya Wasafi Diamond Platnumz amekuwa ni mtu wa matukio kila siku kukicha. Msanii huyo asiyeishiwa matukio kwenye mitandao ya jamii bado anaendelea kuwa gumzo mitandaoni baada ya kupost video inayomuonyesha mwanadada mmoja ambaye jina lake halijajulikana mpaka hivi sasa na kuandika caption yeye utata akiweka imoji zenye kuonyesha upendo huku akiweka hashtag “Usingiz” huku wasanii na wadau mbalimbali wa sanaa wakicoment chini ya video hiyo wengine wakiandika Simba mla nyama. Tukio hilo halikuishia hapo kwa mama yake Diamond mama Dangote aliirepost video hiyo na maneno yale yale ya Diamond ila yeye akaweka hashtag yake na kuandika “Mmemaliza kuchamba”

Bobi Wine afanya kufuru kwa vijana katika jimbo lake jijini Kampala

Image
NancyTheDreamtz Mwanamuziki na mbunge nchini Uganda, Bobi Wine amemkejeli rais Yoweri Museveni, kwa kutoa mchango wa dola 26,000 ambazo ni sawa na milioni 59 za kitanzania kwa vijana katika eneo bunge lake mjini Kampala. Kwa mujibu wa ripoti katika televisheni ya NTV Uganda, Bobi Wine amesema ”Kwa kuwa serikali haina la kuwaambia watu, sasa imegeukia kuwanunua-wakiona hamtishwi na risasi wanawarushia pesa” Bobi pia amesema kuwa ”Utawala hauamini kuwa mtu anaweza kuzungumza na watu bila kuwarushia pesa” Mwanasiasa huyo anadai kuwa serikali ilijaribu kuipatia pesa familia ya dereva wake aliyeuawa kwa kupigwa risasi Agost 13.Gazeti la Daily Monitor pia limeangazia madai hayo likisema familia ya dereva huyo aliyeuawa ilikataa kupokea pesa hizo. Bobi Wine pia alidai kuwa ni yeye aliyekuwa analengwa katika kisa cha kupigwa risasi na kuuawa kwa dereva wake Bobi Wine, ambaye jina lake kamili ni Robert Kyagulanyi anakabiliwa na mashtaka ya uhaini kutokana na kupigwa mawe msafara

Audio: Diamond sio husband material, ametembea na wengi sana – Hamisa Mobetto

Image
NancyTheDreamtz Mwanamitindo Hamisa Mobetto amedai mzazi wenzake Diamond Platnumz sio aina ya wanaume ambaye alikuwa anamwitaji katika maisha yake. Amedai muimbaji huyo ni mwanaume wa kutembea na wanawake wengi na hawezi tulia na mmoja huku akidai nchini Tanzania ametembea na wanaume wengi sana. Related Articles

Kwa jeuri hii ya fedha aliyoionesha Davido, angekuwa Bongo angepata tabu sana (+Audio)

Image
NancyTheDreamtz Msanii kutoka Nigeria, Davido jana ameonesha jeuri ya fedha kwa mara nyingine baada ya kuwanunulia members 18 wa 30 Billion Gang toleo jipya la simu za iPhone XS. Davido kupitia Insta Story alionesha simu hizo na kusema kuwa amenunua kwa ajili ya watu wake wote wa 30 Billion Gang akiwemo mchumba wake, Chioma . Toleo hilo la iPhone XS ndio toleo jipya la simu hizo pendwa duniani, na simu moja inauzwa dola $1,400 ambayo ni sawa na Tsh milioni 3. Kwa hesabu ndogo Davido ametumia tsh milioni 54 kuwanunulia simu rafiki zake ambao wanaunda kundi hilo la 30 Billion Gang. 30 Bilion Gang ni kundi ambalo Davido ndio kiongozi lakini pia wapo binamu zake wawili Sina Rambo na B-Red na meneja wake Asa Asika. Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wake wameshusha maombi wakitaka nao wapewe zawadi za simu hiyo mpya  ya iPhone XS. mrbrownchips @davidoofficial  boss abeg bless me with phone…I saw the ones you got for your team…me na your team too abeg. youngwiz_official @d

Meli iliyopata ajali miaka 400 yapatikana, inadaiwa ilikuwa njiani kutoka India

Image
NancyTheDreamtz Watafiti wa mambo ya kale wamegundua meli iliyopata ajali miaka 400 iliyopita karibu na pwani ya Ureno, katika tukio ambalo wataalam wameliita “ugunduzi muhimu”. Kwa mujibu wa mtandao wa REUTERS, baadhi ya viungo, vyombo vya kauri na mizinga ikiwa na nembo ya Ureno vimetapakaa katika eneo la karibu na Cascais ambapo si mbali sana kutoka Mji Mkuu Lisbon. Wagunduzi hao waamini kwamba meli ilikuwa njiani kutoka India wakati ilipozama kati ya mwaka 1575 na 1625. Nyakati hizo zinakadiriwa kuwa ndiyo kilele cha biashara ya viungo kati ya Ureno na nchi za Asia. Inadhaniwa kuwa huu ni ugunduzi mkubwa kabisa ambao umechukua takribani miaka 10 kwa mujibu wa mkurugenzi wa zoezi hilo, Jorge Freire ambapo akisisitiza ni jambo muhimu zaidi kwa Ureno.

Simba Yaenda Kuweka Kambi Zanzibar Kwaajili ya Kupambana na Yanga

Image
NancyTheDreamtz Kikosi cha Simba kinaondoka leo jijini Dar es Salaam kuandaa dawa maalum ya kuwamaliza Yanga katika mchezo wa Ligi Kuu Bara Septemba 30 Jumapili hii. Simba wanaenda kuweka kambi hiyo Zanzibar kama ilivyo mara nyingi pindi wanapojiandaa kucheza na Yanga tayari kuja kukabiliana na watani zao wa jadi walio na alama 12 kileleni. Kuelekea mchezo huo, wachezaji wa kikosi cha timu hiyo waliokuwa Dar es Salaam kwa ajili ya program maalum iliyokuwa chini  ya Kocha Msaidizi, Masoud Djuma, wataungana na wenzao visiwani humo. Wachezaji hao ambao miongoni mwao ni Haruna Niyonzima na Juuko Murushid wataongeza nguvu kwa ajili ya kujifua vilivyo kuelekea mechi hiyo. Ikumbukwe Simba inaenda kucheza na Yanga ikiwa na kumbukukumbu ya ushindi katika mchezo wao wa mwisho kwa bao 1-0 msimu uliopita.

Wasanii Wengi Hawaweki Maisha yao Halisi Katika Mitandao:-JB

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa bongo movies jacob steven amefunguk na kusema kuwa wasanii wengi wa bongo movies wako tofauti sana  na wale wa bongo fleva kwa sababu hawaweki uhaisia wa maisha yao na kazi yao katika mitandao yya kijamii kitu ambacho kiko tofauti sana. JB anasema kuwa ukiangaia profile nyingi za bongo fleva artst utagundua tu kwa urahisi kuwa huyu ni msanii wa muziki lakini inakuwa ngumu sana kwa wale waigizaji kuweka profile yake hadharani kama wanavyofanya wengine. akiongea na waandishi wa habari JB Anasema ‘wasanii wengi wa bongo movies hawawekagi maisha yao halis katika mitandao, tofauti sana na wale wa bongo fleva ambao wao  ukichungulia tu akaunti zao unakuwa unajua kuwa huyu ni msanii.hii yote ni kwa sababu ya watazania wengi ni malimbukeni wa matumizi ya mitandao ya kijamii.’ Ujumbe huu wa JB unawaendea moja kwa moja wasanii wanaotaka kuishi maisha  ambayo sio ya kwao, Jb anasema kuwa ni bora kuwa muwazi ili shabiki anapoamua kukukubali basi inakuwa amekubali kwa

Zoezi la Kubinua Kivuko cha MV. NYERERE Limefikia Pazuri..Tazama Video

Image
NancyTheDreamtz Leo September 24, 2018 Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi nchini Venance Mabeyo amesema zoezi la kukinasua Kivuko cha Mv. Nyerere limefikia pazuri tayari wamekiinua upande mmoja na wana matumaini kitatoka vizuri. “Wameanza kukinyanyua kwenye injini, ili kukinyanyuliwa kije juu kielee lakini sasa kinafungwa maboya kwa chini, tunaandaa pampu ili kikichota maji yaweze kunyonywa, tuwe na matumaini kivuko kitatoka vizuri” -Mabeyo VIDEO: 

Kijina wa Sekondari Agundua Simu Isiyotumia Vocha wala Kadi

Image
NancyTheDreamtz Kijana Simon Petrus Mwanafunzi wa Sekondari raia wa Namibia ameuelezea ugunduzi wake kuwa unatumia mawimbi ya redio na hauhitaji kuwa na 'simcard na airtime' - Amesema kuwa imemchukua miaka 2 kukamilisha ugunduzi huo alioufanya kwa kutumia mabaki ya simu na runinga zilizoharibika - Wazazi wake ambao hawana ajira kwa sasa walihangaika kumsaidia kijana wao ili akamilishe mradi huo uliogharimu kiasi cha zaidi ya Shilingi za Kitanzania Milioni Nne

Mwili wa Mtoto Mdogo Waopolewa Leo Wakati Shughuli ya Kunyanyua Kivuko Ikiendelea...

Image
NancyTheDreamtz Idadi hiyo imefikia baada ya Mwili wa mtoto mmoja kuopolewa leo ambapo shughuli ya kukivuta Kivuko hicho inaendelea Itakumbukwa kuwa jana Septemba 24 miili ya watu wawili iliopolewa katika eneo la ajali hiyo kwenye Ziwa Victoria Aidha, baada ya kufanikiwa kukilaza kwa ubavu Kivuko hicho baadhi ya mizigo ikiwamo mikungu ya ndizi, mikoba na majamvi imeanza kuelea na kusukumwa na maji hadi ufukwe wa kijiji cha Bwisya katika kisiwa cha Ukara Kazi ya kunyanyua kivuko hicho kilichozama Septemba 20 na kujifunika inafanywa na wataalam kutoka JWTZ na vikosi vingine vya ulinzi na usalama wakishirikiana na Maafisa kutoka kampuni ya Songoro Marines ya jijini Mwanza

Mizigo ya Waliofariki na Majeruhi Yaanza Kuibuka

Image
NancyTheDreamtz Mizigo zaidi inasukumwa ufukweni kutoka ndani ya kivuko cha Mv Nyerere baada ya wataalam kufanikiwa kukinyanyua na kukilaza ubavu  Ukara. Baadhi ya mizigo ikiwamo mikungu ya ndizi, mikoba na majamvi  iliyokuwa ndani ya kivuko cha Mv Nyerere kilichozana ziwa Victoroa imeanza kuelea na kusukumwa na maji hadi ufukwe wa kijiji cha Bwisya kisiwa cha Ukara wilayani Ukerewe. Hali hiyo imejitokeza baada ya wataalam wa uokoaji kufanikiwa kikilaza ubavu kivuko hicho hicho kilichopinduka Septemba 20 na kujifunika kifudifudi. Kazi ya kunyanyua kivuko hicho inafanywa na wataalam kutoka Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) na vikosi vingine vya ulinzi na usalama wakishirikiana na maofisa kutoka kampuni ya Songoro Marines ya jijini Mwanza. Operesheni ya uokoaji tayari imefanikisha kuopoa miili ya watu 227 waliokufa katika ajali hiyo, huku wengine 41 wakiokolewa hai.