Posts

Showing posts from September 1, 2018

Parent's Relation can Destroy the Family if Dad with Mom will be separated

Image
NancyTheDreamtz We must to be the same in all time especially to the People who like to generate the family's Because if Dad staying far with mom what will happen mom must find another dad to recover the place of your dad so don't live your family a lone  Thanks Dad Nancy Dream

Katibu Mkuu Atoa Neno Wanachama wa CCM Kuchafuana Mitandaoni

Image
NancyTheDreamtz Katibu Mkuu wa CCM, Dk Bashiru Ally amesema chama hicho kinafuatilia majadiliano ya wanachama wao katika mitandao ya kijamii ili kujiridhisha kuwa haivuki mipaka ya uhuru wao. Akizungumza leo Ijumaa Agosti 31, 2018 katika ufunguzi wa baraza kuu la vijana wa chama hicho (UVCCM) amesema mitandao hiyo imekuwa chanzo cha fitna, kebehi na kuchafuana. Amesema wakati mwingine mwenyekiti wa CCM, Rais John Magufuli anachafuliwa katika mitandao hiyo na hakuna hatua yoyote inayochukuliwa na UVCCM kulinda hadhi ya taasisi ya urais na chama. “Tunafuatilia mijadala ya wanachama wetu wote ndani ya chama na jumuia ili tujiridhishe hawavuki mipaka ya uhuru wa kujadili masuala ya chama ndani ya mitandao hiyo,” amesema. Ametoa mfano wa kiongozi mmoja (bila kumtaja jina) wa UVCCM  mkoani Mara kuwa alikuwa akiingilia masuala ya kisheria na kuandika mambo ya ovyo mitandaoni kuhusu Serikali. Amesema mambo aliyokuwa akiandika kiongozi huyo hayakuwa na ukweli na hivyo k

Wazazi wanaposalitiana isiwe sababu ya Mmojawao kumdanganya mtu mungine juu ya Mtoto aliyezaa nae

Image
NancyTheDreamtz Jamani tunapokuwa kwenye mahusiano kama mmoja wao anamdanganya mungine basi ajue mwisho wasiku ataachika na isiwe sababu yakumfanya huyo wasasa kuwa yuko sahihi ila wamwanzo hana zuri alilowahi kumfanyia kwani huwezi nufaika kwakusema uongo mungu anakuona mara mia ya unavyojiona wewe

Makamu wa Rais Kuzindua Jengo la Kitega Uchumi la Ghorofa 16 Jijini Arusha

Image
NancyTheDreamtz Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan, anatarajiwa kuwaongoza maelfu ya wananchi wa Mkoa wa Arusha katika hafla ya uzinduzi wa jengo la kitega uchumi la Jakaya Kikwete Ngorongoro Tower (JKNT). Jengo hilo la ghorofa 16, ambalo ni mali ya Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro (NCAA), linatarajiwa kuzinduliwa rasmi na Makamu wa Rais, Septemba 16, mwaka huu. Akizungumza na waandishi wa habari wakati walipotembelewa na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya Mkoa wa Arusha, kukagua jengo hilo, Mwenyekiti wa Bodi ya NCAA, Profesa Abiud Kaswamila, alisema Makamu wa Rais amethibitisha kuhudhuria katika hafla ya uzinduzi wa jengo hilo. Alisema jengo hilo ni kati ya majengo ya kisasa zaidi kujengwa mkoani hapa na litatumika maalum kama kituo kimoja cha kukuza na kurahisisha biashara ya utalii nchini. Maneja wa mradi wa ujenzi wa jengo hilo, Profesa Camillius Lekule, ambaye ndiye aliyebuni mchoro wa jengo hilo, alisema kiasi cha fedha zilizotumika hadi sasa ni Sh. bilioni 39.9 kati ya Sh. bil

Video: Sakata la Makontena ya Makonda Le Mutuz Amuomba Msamaha Waziri Mpango

Image
NancyTheDreamtz Mjasiriamali ambaye ni mtoto wa Waziri Mkuu Mstaafu, john Malecela, William Malecela maarufu kwa jina la Lemutuz amesema amemuomba msamaha Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango kufuatia kauli yake kuhusu mkontena ya RC Paul Makonda yaliyokamatwa bandarini kwa kushindwa kuyalipia kodi. Lemutuz amesema kwa uelewa wake alidhani baada ya makontena hayo kukamatwa, samani zote zilizomo ndani zingepelekwa na kugawiwa mashuleni, lakini baada ya Rais Magufuli kufafanu juzi kwamba mwenye mamlaka ya kupokea misaada ni Waziri wa Fedha pekee, hivyo Lemutuz aliielewa sheria, amemuomba msamaha Waziri na kuiachia serikali ifanye maamuzi.

Dr. Slaa Hawezi Kuwa Shujaa Alikimbia Mapambano Kabla Vita Haijaisha

Image
NancyTheDreamtz " Dr. Slaa hawezi kuwa shujaa kwakuwa alikimbia mapambano, yale aliyofanya wakati yuko kwenye chama cha CHADEMA alipaswa kuyafanya maana alikuwa analipwa na chama na chama kilimhudumia kila kitu hivyo ulikuwa wajibu wake kufanya maana alikuwa analipwa na chama" || Ameyasema hayo Sosopi Mwenyekiti BAVICHA

Breaking News: Makontena ya Makonda Yakosa Wateja Tena....

Image
NancyTheDreamtz MNADA wa makontena 20 ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda, umefanyika leo Jumamosi, Septemba 1, 2018 katika Bandari ya Dar, lakini imeshindikana kupatikana mnunuzi, hivyo mnada huo utaendelea Jumamosi ijayo. Mkurugenzi wa kampuni ya Udalali ya Yono Auction Mart, Scolastika Kevala, amesema hawajapata mnunuzi wa kontena hata moja lakini wamefanikiwa kuuza bidhaa 10 tu zilizokuwemo kwenye makontena hayo. Sehemu kubwa ya bidhaa zilizomo kwenye makontena hayo ni samani za ofisini kama vile viti, meza na makabati na vitu vingine. “Mpaka sasa tayari tumefanya mnada wa makontena yote 20 lakini hayajapata mteja ingawa tumefanikiwa kuuza bidhaa 10 zilizokuwemo kwenye makontena hayo. Hivyo mnada wa makontena utaendelea tena Jumamosi ijayo,” amesema Kevela. Itakumbukwa kuwa Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango aliagiza makontena hayo kupigwa mnada licha ya RC Makonda kutoa vitisho kuwa atakayenunua vitu vilivyomo kwenye makontena hayo atapata laana. Aidha, mn

Hatimaye Serikali ya Uganda Yamuachilia Bobi Wine Kusafiri Kwenda Marekani Kwaajili ya Matibabu

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Uganda ambaye inadaiwa aliteswa na maafisa wa usalama, Robert Kyagulanyi  maarufu kwa jina la Bob Wine ameruhusiwa kusafiri kuelekea Marekani kwaajili ya matibabu. Alhamisi usiku Polisi walimkamata Kyagulanyi na mbunge mwenzake wa upinzani Francis Zaake uwanja wa ndege wa Kampala wakati wakijiandaa kwenda nje ya nchi kupatiwa matibabu. Polisi walidai kuwa viongozi hao wa upinzani, ambao wote wanakabiliwa na tuhuma za uhaini walikuwa katika harakati za kukimbia nchi. Hata hivyo, wabunge hao wawili wamesema kuwa waliteswa baada ya kukamatwa huko nyuma na hospitali ya Kampala ilitoa pendekezo kwamba wapatiwe matibabu nje ya nchi.

Hafla ya Wabunge Yafana.... Wachangisha Mill. 800 Kwaajili ya Ujenzi wa Vyoo

Image
NancyTheDreamtz Takribani shilingi milioni 800 zimepatikana katika Hafla Maalum ya kuchangisha fedha kusaidia ujenzi wa vyoo vya watoto wa kike mashuleni iliyofanyika Mlimani City Jijini Dar es Salaam usiku wa jana. Mgeni rasmi Spika Mstaafu Mama Anna Makinda akipokea mfano wa hundi kutoka kwa taasisi mbalimbali ambazo zimechangia Fedha kwa ajili ya ujenzi wa vyoo kwa watoto wakike mashuleni. Mbunge wa Mbulu Vijijini mhe;Flatey Maasai akiongoza jopo la wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika kuruka sarakasi na kuendesha baiskeli ya tairi moja jukwaani na mhe; Vicky Kamata Mbunge wa viti maalumu akaongoza kwaya(choir) ya bunge,lakini singeli ikasimamiwa na mhe;Ali Ungando mbunge wa Kibiti ni katika hafla ya kuchangia  ili mtoto wa kike aweze kupata choo bora Wabunge wakiburudika kwenye hafla ya kuchangia  ili mtoto wa kike aweze kupata choo bora iliyofanyika Mlimanin City, jijini Dar es Salaam.

Hamisa Mobetto: Matusi ya Mtandaoni Yamemnufaisha Kimtindo

Image
NancyTheDreamtz Kama unafikiri mwanamitindo Hamisa Mobetto anatikiswa na mambo yanayozungumzwa mitandaoni utakuwa unakosea. Mrembo huyu ameweka wazi kuwa hatikiswi na maneno hayo kwani alishazoea kuzungumziwa tangu utotoni. “Mimi huwa naangalia mtandaoni nikikuta matusi namblock mtu aliyefanya hivyo kwa sababu matusi hayakubaliki katika jamii yetu, suala la kuzungumziwa wala sishangai tangu nikiwa mdogo watu walikuwa wakinizungumzia, mama akawa ananiambia ‘am so special’,” Amesema yeye ni miongoni mwa wenye mioyo migumu kiasi cha kutoumizwa na maneno ya watu. Amesema licha ya changamoto nyingi anazokutana nazo kwenye mitandao ya kijamii, imemsaidia kufanikiwa. Hamisa ambaye pia ni mmiliki wa duka la mitindo la Mobettostyle amesema maendeleo hayo ya teknolojia yamekuwa na matokeo hasi na chanya kwake. Akizungumza muda mfupi baada ya kuzinduliwa kwa kampeni ya kuhamasisha matumizi sahihi ya vijana ya ‘Be Smart’, Hamisa amesema amefanikisha vingi kupitia mitandao. Amefafanua kuwa hata

Cheyo: “Vijana Njooni Niwajaze Mapesa”

Image
NancyTheDreamtz Mwenyekiti wa UDP taifa John Cheyo amefunguka kuwa hawezi kuhama chama alichokianzisha mwenyewe na kuhamia CCM, na kuwataka vijana kujiunga na chama chake ili wajipatie pesa. Cheyo ambaye ni maarufu kwa jina la Bwana Mapesa amefunguka hayo kupitia Weekend BreakFast leo Jumamosi Septemba mosi, ambapo amesema kuwa siasa za upinzani zikiendelea hivi kwa viongozi wa upinzani kuhama na kupandikiza chuki wapiga kura hakutakuwa na mtu wa kumtoa Rais Magufuli madarakani. “Siwezi hama chama kwenda kuunga jitihada ntaunga nikiwa UDP siwezi hama nyumba yangu mimi ndio baba mwenye nyumba, nawakaribisha vijana na wote wenye mapenzi na siasa waje kwangu UDP niwajaze mapesa”, amesema Cheyo. John Cheyo ni moja ya viongozi wa vyama vya upinzani nchini akiwa mwanzilishi wa Chama cha United Democratic Part (UDP). Cheyo alipata umaarufu sana nchini katika kinyanganyiro cha uchaguzi cha mwaka 2005, ambapo alisema kwa ufupi kwamba sera zake ni "kuwajaza watanzania mapesa". Hii il

Ali Kiba Apewa Zigo la Mabao Coastal Union

Image
NancyTheDreamtz Mshambuliaji wa Coastal Union, Alli Salehe ‘Alikiba’ ni kama amepewa zigo la mabao katika Ligi Kuu Bara msimu huu baada ya kocha wa kikosi hicho, Juma Mgunda kumtaka afunge zaidi ya mabao 25 kwa kile alichodai uwezo wa kufanya hivyo anao. Alikiba tangu asajiliwe na timu hiyo msimu huu, bado hajaoneka­na uwanjani wakati tayari wenzake wameshacheza mechi mbili mpaka sasa na leo Jumamosi wanatarajiwa kupambana na KMC katika Uwanja wa Mkwakwani mkoani hapa. “Mashabiki wa Coastal Union wa­nachotakiwa kufahamu ni kwamba timu hii imesajili wachezaji 30 na kila mchezaji anataka kucheza, hivyo muda ukifika kila mmoja ataonekana uwanjani. “Najua wengi wanamuulizia Alikiba, niseme tu ataonekana uwanjani muda si mrefu na niwaambie ni mshambulia­ji mzuri na anaweza kufunga zaidi ya mabao 25 msimu huu,” alisema Mgun­da.