Posts

Showing posts from June 27, 2019

Chama Aongeza Mkataba Mpya Simba SC

Image
NancyTheDreamtz MFUNGAJI wa mabao ya mwisho yaliyoipeleka hatua ya makundi na Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika timu ya Simba Mzambia, Clatous Chota Chama ‘Triple C’ ameongeza mkataba mwingine wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea timu hiyo. Huyo, ni mchezaji wa sita kwa Simba kuongezewa mkataba wengine ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Aishi Manula, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na Meddie Kagere. Chama alijiunga na Simba kwenye msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara akitokea Power Dynamo inayocheza ligi ya nchini huko. Taarifa ya klabu ya Simba inaeleza kuwa kiungo huyo atakuwa sehemu ya kikosi hicho hadi 2020 baada ya kuongeza mkataba huo. Simba hivi sasa ipo kwenye mikakati ya kukiboresha kikosi hicho kwa ajili ya michuano ya kimataifa Afrika na kikubwa kufika hatua ya fainali baada ya msimu uliopita kufika robo fainali. Timu hiyo hadi hivi sasa tayari imefanikiwa kuwasajili wachezaji wapya watano ambao ni Beno Kakolanya, Kennedy Juma, Gerson Fraga

HAMISA AAPA KUTOZAA TENA BILA NDOA!

Image
NancyTheDreamtz Mwanamitindo na msanii wa Bongo Fleva, Hamisa Mobeto. BAADA ya kuzaa watoto wawili kabla ya kuolewa huku kila mtoto akiwa na baba yake, mwanamitindo na msanii wa Bongo Fleva, Hamisa Mobeto amefunguka kwamba kwa sasa hafikirii tena kufanya hivyo. Akipiga stori mbili-tatu na gazeti hili, mrembo huyo alisema kuwa katika maisha yake hakuwahi kuamini katika ndoa ndiyo maana akaamua kuzaa watoto wawili bila ndoa, lakini sasa anatamani kuongeza watoto wengine watano ndani ya ndoa ili atimize ndoto yake ya kuwa na watoto saba. “Sasa hivi ninahitaji mwanaume wa kufunga naye ndoa na Mungu akitujalia nizae naye watoto watano ili nitimize ndoto yangu ya kuwa na watoto saba,” alisema Mobeto. Katika watoto wawili alionao Mobeto, mmoja amezaa na msanii Nasibu Abdul ‘Diamond’ na mwingine amezaa na Mkurugenzi wa EFM na TVE, Francis Ciza‘Majizo

BREAKING: KAPOMBE AONGEZA MIAKA MIWILI MIWILI SIMBA

Image
NancyTheDreamtz Beki wa kulia wa Simba Shomari Kapombe ameongeza mkataba wa miaka miwili kuichezea timu hiyo. Makubalia hayo hayo yamefikiwa baina ya klabu ya mchezaji kuendelea kutoa huduma kwa miaka miwili ijayo. Kapombe ambaye msimu uliomalizika hivi karibuni haukuwa mzuri kutokana na kusumbuliwa na majeruhi atakuwa mmoja wa wachezaji watakaoendelea na Simba msimu ujao. Simba wameendelea kuwaongezea mkataba wachezaji wao ambao wameshamaliza na wanahitaji kuwa nao kwa sasa.

MOSHI: Wananchi wenye hasira kali wachoma moto Kanisa, Wamtuhumu Mchungaji kusababisha vifo vya watoto wawili (+Video)

NancyTheDreamtz Wanawake waliojawa na jazba wamechoma moto kanisa la Unyakuo lililopo kata ya Msaranga manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro kwa kumtuhumu mchungaji wa Kanisa hilo, kujifanya mkunga jambo ambalo limesababisha vifo vya vichanga wawili ambao walikuwa ni mapacha. Wakiongea na kituo cha runinga cha Azam TV, Wananchi hao wamesema kuwa Mchungaji huyo alikuwa anawadanganya wanawake wajawazito kuwa wasiende Kliniki, Elimu ambayo imewapotosha watu wengi.

Ndugai Akerwa na Kiongozi wa Serikali Aliyesema Mbele ya Rais Kuwa Wabunge Wamewadhihaki Wachezaji wa Taifa Stars

Image
NancyTheDreamtz Spika wa Bunge la Tanzania, Job Ndugai amesema kiongozi mmoja wa Serikali aliyezungumza maneno yasiyofaa kuhusu Bunge la Tanzania na wabunge na kumdanganya hadharani Rais John Magufuli kuwa wawakilishi hao wa wananchi wamewadhihaki wachezaji wa timu ya Taifa ya Tanzania ‘Taifa Stars’, hajitambui. Spika ametoa kauli hiyo bungeni  jana Juni 25, baada ya Mbunge wa Kigoma Mjini Zitto Kabwe, (ACT-Wazalendo), kuomba muongozo kwa kutumia kanuni ya 68 (7), kuhusu jambo lililotokea mapema bungeni. Zitto alilazimika kuomba muongozo huo baada ya Spika Ndugai kutoa ufafanuzi kwamba hakuna mbunge yeyote aliyewadhihaki wachezaji wa Taifa Stars baada ya mchezo wake na Senegal. “Mheshimiwa Spika, kwa kutumia kanuni 68 (7), kuhusu jambo lililotokea bungeni mapema, umeelezea jambo ambalo limetokea nje ya bunge kuwa mmoja ya viongozi wa serikali kuwabagaza wabunge waliokwenda Misri. Mara baada ya mbunge huyo kuomba muongozo huo, Spika Ndugai, alijibu aki

Wananchi 13,234 Wapatiwa Elimu Ya Madhara Ya Mimba Za Utotoni

Image
NancyTheDreamtz Na.Faustine Gimu Galafoni,Dodoma Jumla ya wananchi 13,234  wamefikiwa na elimu ya madhara ya mimba za utotoni hapa nchini . Hayo yamesemwa leo bungeni jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya  jamii,jinsia wazee na watoto Dokta Faustine Ndugulie  wakati akijibu swali la mbunge wa Viti Maalum Fatma Tafiq aliyehoji,ndoa  za utotoni ni tatizo kubwa katika jamii zetu  hususan katika jamii zenye umasikini ,je ,serikali haioni kuwa kuna umuhimu wa kutoa elimu kwa umma hasa katika maeneo ya vijijini ili wananchi wafahamu athari za kuozesha watoto katika umri mdogo.   Katika majibu yake,Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia,Wazee na watoto Dokta Ndugulile amesema serikali ina tambua umuhimu wa elimu kwa umma katika kupambana na ndoa za utotoni ambazo zina madhara makubwa kwa watoto wa kike .   Hivyo amesema kupitia mbalimbali za mawasiliano ikiwemo TV,Radio,Magazeti na Majarida serikali imekuwa  ikitoa elimu kwa  kuandaa jumbe

Zitto Kabwe Aipongeza Serikali...Chama Chake Chamkana, Chasema Siyo Yeye

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Kigoma Mjini na Kiongozi wa ACT Wazalendo, Mhe. Zitto Kabwe amesema kuwa licha ya yeye kuwa mpinzani lakini ataendelea kuipongeza Serikali ya Rais Magufuli. Zitto kupitia ukurasa wake wa Twitter ameandika “ACT Wazalendo kimekuwa chama kinachohubiri Ujamaa lakini kwa kuingia huku kwa Maalim Seif ambaye kwenye chama chake cha CUF walikuwa wakitumia mfumo wa Kibepari inabidi tuhamie huko sasa kama tulivyokubaliana na kutakuwa na mabadiliko ya Kiuongozi.“. “Ni kweli tumekuwa tukiikosoa Serikali kwa muda mrefu lakini lazima nikiri kuwa kuna mabadiliko makubwa sana yamefanywa na Serikali hii ya JPM. Japokuwa najua kuna baadhi ya viongozi aliowateua wanamuangusha kiuhalisia MAGUFULI amefanya mengi.” ameandika Zitto Kabwe na kusisitiza. “Wapo ambao najua wataniita majina mengi ya ajabu kwa maamuzi yangu haya kama jinsi ambavyo wamekuwa wakimshambulia ndugu yangu @Nnauye_Nape kwa kutokuwa na misimamo thabiti lakini nataka niwaambie huo

Baadhi ya Wabunge Kenya wamuunga mkono Jaguar....Wataka aachiwe huru

Image
NancyTheDreamtz Matamshi ya mbunge wa Starehe nchini Kenya Charles 'Jaguar' Kanyi kuhusu kuwatishia raia wa kigeni wakiwemo watanzania  wanaofanya kazi nchini Kenya yaliwasilishwa jana  mbele ya kikao cha bunge ili kujadiliwa. Baadhi ya wabunge nchini humo  wakichangia mjadala huo wameunga mkono kauli ya Jaguar huku wakitaka aachiwe huru kwani alichosema ndio mtazamo wa Wakenya waliowengi. Akichangia maoni bungeni jana Juni 26, 2019, Mbunge wa Garissa mjini, Aden Duale amesema Jaguar alifanya jambo la kizalendo kwani Taifa hilo linahitaji kuwalinda wananchi wao kwenye masuala ya kibiashara. Mbunge mwingine ni Moses Kuria wa jimbo la Gatundu Kusini, Amesema kuwa kauli ya Jaguar sio ngeni kwani viongozi wengi wa nchi hiyo walishawahi kuongea kuhusu wageni kupora fursa za kibiashara nchini humo. Jana Mbunge wa jimbo la Starehe, Jaguar alishikwa na maafisa polisi katika viunga vya bunge la nchi hiyo na mpaka sasa bado hajaachiwa. ==>.Wasikilize

Mbunge Jaguar wa Kenya aburuzwa mahakamani

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Starehe, nchini Kenya Charles Njagua maarufu Jaguar na amefikishwa mahakamani leo. Hata hivyo, ametupwa ndani hadi kesho mahakama itakapoamua iwapo ataachiliwa kwa dhamana. Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka ya Umma (ODPP) yaomba Mbunge huyo azuiliwe kwa siku 14 kwa uchochezi na kutoa vitisho dhidi ya wafanyabiashara wa kigeni. Hapo jana Mbunge huyo alikamtwa nje ya majengo ya Bunge kufuatia kauli zake za ‘kibaguzi' akiwataka wafanyabiashara wa Tanzania na Uganda wanaoendesha shughuli zao katika masoko mjini Nairobi na miji mingineyo kuondoka nchini humo ndani ya saa 24   Mbunge huyo analionekana katika video fupi ambayo ilisambaa katika mitandao ya kijamii akizungumza na wafanyabiashara wa jijini humo na kuwaeleza kuwa hawatokubali watu wa nje waje kufanya biashara nchini mwao. ''Wakenya ni sharti wafanye biashara zao bila kushindana na watu kutoka mataifa mengine. Raia wa Pakistan wametawala biashara za kuuza magari nchini h