Posts

Showing posts from April 18, 2019

Sugu agoma kusoma hotuba ya upinzani bungeni

Image
NancyTheDreamtz Msemaji wa Kambi rasmi ya upinzani Bungeni katika Wizara ya Habari Joseph Mbilinyi (Sugu) amegoma kuendelea kusoma hotuba yake Bungeni kwa madai kuwa zaidi ya 80% ya maneno yameondolewa katika hotuba yake kuhusu bajeti ya Wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2019/20. Sugu amelazimika kuchukua uamuzi huo leo Alhamisi Aprili 18, bungeni jijini Dodoma, baada ya  Naibu Spika wa Bunge, Dk. Tulia Ackson kumtaka asisome baadhi ya maeneo yaliyoko katika hotuba yake.   Kwa mujibu wa Dk. Tulia, hotuba aliyotaka kusoma Sugu ilikuwa na mambo yaliyoondolewa baada ya kuonekana yanakiuka kanuni za kudumu za Bunge.   Kabla ya Sugu kuchukua uamuzi huo, alianza kusoma hotuba kupitia katika kitabu alichokuwa nacho lakini baada ya muda mfupi tangu alipoanza kusoma, Dk Tulia alimtaka asiisome bali asome kupitia kitabu kipya cha hotuba yake ambacho wabunge wote walikuwa wamegawiwa.  Kutokana na maelekezo hayo,Sugu alisema hawezi kufanya hivyo kwani kitabu kipya hakina maoni ya kambi yake

Rose Muhando Yupo Fiti Aruhusiwa Kutoka Hospital Kenya

Image
NancyTheDreamtz MWIMBAJI  maarufu wa nyimbo za injili nchini, Rose Muhando, hatimaye ameagwa katika hospitali aliyokuwa amelazwa nchini Kenya baada ya kuugua kwa muda mrefu. Rose ambaye aliibua hisia kali miongoni mwa mashabiki wake nchini Kenya na Tanzania miezi minne iliyopita alipoonekana jijini Nairobi akiwa na majeraha makubwa na akiombewa na mhubiri wa Neno Evangelism jijini Nairobi, James Nganga, ameonekana akiwa na waimbaji wenzake wa nyimbo za dini, Betty Bayo, Solomon Mkubwa na wengine. Katika picha hizo, majeraha aliyokuwa nayo hayaonekani tena na anaonekana ni mchangamfu kabisa ikiashiria hali yake ya kiafya ikiwa imeimarika huku uso wake uking’aa na mwenyewe akitabasamu kutokana na matendo makuu ya Mungu aliyemponya. Katika video iliyochapishwa na Solomon Mkubwa, anaonekana akiimba na kumshukuru Mungu kwa kumponya. Solomon ame-post picha akiwa na Rose na waimbaji wengine na kuandika: “Mungu mukubwa Rose muhando amekua vizuri. Malkia Rose yuko poa sasa.” 

Msukuma Ataka Adhabu Mbadala Kwa Wafungwa Wenye Makosa Madogomadogo

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku (Musukuma) ameitaka Wizara ya Katiba na Sheria kufanya marekebisho ya baadhi ya sheria zinazoonekana hazina manufaa kwa mazingira ya sasa. Musukuma ametoa kauli hiyo katika vikao vya Bunge kwenye mjadala wa Wizara ya Katiba na Sheria ambapo kupitia Waziri wa Katiba na Sheria, Agustino Mahiga aliwasilisha makadirio ya bajeti yake. "Niseme tu kiukweli ni vizuri mkaangalia mkarekebisha sheria, hasa kwenye makosa madogodogo ambayo yamepelekea magereza mengi kujaa mahabusu ambayo kwa kweli mengine yanastahili makofi tu mtu akaenda nyumbani", amesema. Musukuma ameongeza kuwa, "nashauri sana hizi sheria zilizotungwa tukiwa milioni 20, leo tuko milioni 55 mtu anawekwa wiki 2 kwa kesi ya kuiba kuku, ni vitu ambavyo tufikirie adhabu ili kupunguza mrundikano wa mahabusu kule ndani." "Nilisoma kwenye kitabu cha Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni kuhusiana na uteuzi wa Majaji, inampa mamlaka Rais kuteua na anakuwa jo

Kayumba Amfungukia Irene Uwoya

Image
NancyTheDreamtz BAADA ya kutamba na Ngoma ya Wasiwasi, msanii wa Bongo Fleva ambaye pia ni mshindi wa Bongo Star Search 2015, Kayumba Juma ‘Kayumba’ amekuja na ngoma mpya ambayo ndani yake amemuimba staa wa Filamu Bongo, Irene Uwoya. Akichonga na Risasi Vibes, Kayumba ambaye pia ni zao kutoka Mkubwana Wanawe alifunguka kuwa, sanaa ni  ubunifu hivyo kutokana na kumkubali Uwoya ameamua kumuimbia wimbo unaoenda kwa jinala Uwoya. “Ujue katika muziki unaweza kumuimbia mtu yeyote na nimemuimbia Uwoya kwa sababu amekuwa akisapoti kazi zangu mara kwa mara ninapotoa,” alisema Kayumba.