Posts

Showing posts from January 19, 2019

RC Makonda aandika barua ya wazi ‘Acha niseme nawe kidogo kaka yangu Tundu Lissu’

Image
NancyTheDreamtz Ikiwa ni siku chache toka Mbunge wa jimbo la Singida , Tundu Lissu ahojiwe na kituo cha runinga cha BBC cha Uingereza na kuzungumza mambo mengi kuhusu afya yake pamoja na serikali ya Rais John Pombe Magufuli na kumtuhumu mambo mazito, Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam, Paul Makonda ameibuka na kuandika barua ya wazi kwa mwanasiasa huyo wa Chadema. Barua yenyewe hii hapa chini.. ACHA NISEME NAWE KIDOGO KAKA YANGU TUNDU LISSU HASA NIKIANZA NA Shukran kwake muumba wa mbingu na ardhi kwa kumpa kaka yetu Tundu Lissu afya na siha njema. WENGI WALIOKO JIMBONI SINGIDA NA WA TANZANIA WOTE WALIHANGAIKA KWA SALA NA MAOMBI, USIKU NA MCHANA, WENGINE WAKICHANGA PESA ZAO NA HATIMAYE MOLA AKAJIBU MAOMBI YAO. KWA HESHIMA NA KUONYESHA UZALENDO, NAKUSHAURI KAKA YANGU TUNDU LISSU RUDI NYUMBANI UTOE SHUKRANI ZAKO KWAO. WATU WAKO WAMEKUMISS ZAIDI YA HAO UNAOWAKIMBILIA HIVI SASA. ZIARA YAKO HUKO HAINA TIJA KWA YOYOTE, NA KUICHAFUA SERIKALI SI KUMCHAFUA MH. RAIS NI KUICHAFUA TANZAN