Posts

Showing posts from March 7, 2020

Mwijaku Aampa Ushauri Hamisa Mobetto " Ulifanikiwa Kuchomoka, Ukapona! Kuwa Makini, Usiangukie Kwenye Mikono yao Tena"

Image
NancyTheDreamtz Ujumbe wa Mwijaku kwa Hamisa Mobeto "Wataanza Kukumiss pale watakapokosa mbadala wako. Wataanza kukumiss pale watakapoona uso wako umejaa tabasamu na muonekano wako ni bomba kuliko awali. Ulifanikiwa kuchomoka, ukapona! Kuwa makini, usiangukie kwenye mikono yao tena"

Koffi Olomide Amwagia Sifa Kibao Mwanamuziki Nandy

Image
NancyTheDreamtz Kupitia kwenye kipindi cha Jahazi kinachorushwa Radio Clouds FM nguli wa muziki wa dansi 💥Koffiolomide amefunguka na kusema anakubali uimbaji wa NANDY KOFFI ALISIKIA NA KUSEMA Kuna msanii wa kike huyo nani kaimba kivuruge, oooh nandy namkubali'- Koffi Olamide Kabla sijarudi congo inshallah tutafanya jambo Tanzania ni nyumbani'- Koffiolomide

Jokate Awataka Yanga Kujaza Taifa Waiue Simba

Image
NancyTheDreamtz Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegello. MMOJA wa wapenzi maarufu wa Yanga ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegello, amewataka wapenzi wa timu hiyo kujitokeza kwa wingi Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wakati watakapopambana na watani wao wa jadi, Simba. Mchezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara ambao Yanga ndio watakaokuwa wenyeji, unatarajiwa kupigwa kesho saa 11:00 Jioni kwenye Uwanja wa Taifa. Ikumbukwe katika mchezo wa mzunguko wa kwanza baina ya timu hizo uliisha kwa sare ya mabao 2-2. Simba waliongoza kwa mabao 2-0 kabla ya Yanga kupambana na kuchomoa yote ndani ya dakika saba. Akizungumza na Championi Jumamosi, Jokate alisema Yanga watashinda mchezo huo wa Jumapili kutokana na ubora wa kikosi chao. “Sina wasiwasi na timu yangu ya Yanga, naamini itashinda tu mbele ya Simba, niwaombe mashabiki wa Yanga wajitokeze kwa wingi uwanjani wakiwa wamevaa jezi za timu yetu ili wawape morali wachezaji wetu waweze

Katibu Mkuu CCM: Tutatumia Dola Kubaki Madarakani

Image
NancyTheDreamtz Katibu  Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Bashiru Ali, amekiri chama chake kuitumia dola kuhakikisha kinabaki madarakani. Amesema kama chama chochote kinachoongoza serikali kitashindwa kutumia dola kubaki madarakani, utakuwa uzembe wa chama chenyewe. Kwa kulitambua hilo, Dk. Bashiru amesema CCM imekuwa ikitumia dola kujihakikishia ushindi wakati wa uchaguzi na mwaka huu wamepanga "kuitumia dola kweli kweli". Lakini, kiongozi huyo wa CCM akaonya kuwa chama kinachoongoza serikali, hakipaswi kuitumia dola kunyanyasa wapinzani wake. Dk. Bashiru aliyasema hayo katika mahojiano maalum na vyombo vya habari vya IPP alivyovitembelea jijini Dar es Salaam jana. "Ukishakuwa chama tawala, kuna dhana inaitwa nafuu ya mwenye madaraka. Ukishindwa kutumia nafuu hiyo, utakuwa kama KANU (chama tawala cha zamani cha Kenya), iliposhindwa kutumia nafuu hiyo, haikuwahi kurudi madarakani au UNIP ya Zambia. "Unashika dola halafu unatumi