Posts

Showing posts from August 3, 2020

MATOKEO YA UCHAGUZI MKUU CHADEMA TAIFA.

Image
NancyTheDreamtz

Lulu Diva afunguka uhusiano wake na Lavalava

Image
Jana Kupitia big sunday live ya Wasafi Tv Msanii wa bono fleva Lulu Diva alitolea ufafanuzi Kuhusu story za yeye kuwa kwenye mahusiano na msanii mwenzake kutoka katika label ya WCB Wasafi Lavalava.  Story hizi zilizokuja baada ya video za utata za wawili hao kuzagaa Mitandaoni ambazo zikiwaonyesha kuwa ni wapenzi.  ''Kwani Mtu Akiwa Na Ukaribu Na Mtu Kuna Mahusiano? Sio Kwamba wcb Nimemzoea LAVA LAVA Wote Na Washikaji Zangu Kwahiyo Na Hata Kwa Jana Kuonekana Nipo Nae Ni Kwasababu Tulikuwa Wote Kwenye Harusi Baada Ya Hapo Tulitoka Tukaenda Kwenye After Party Kwahiyo Sidhani Kama Ni Kitu Kibaya Na Mimi Kukaa Na Wanaume Ni Kitu Ambacho Ni Kawaida Kwasababu Kampani Yangu Kubwa Ni Ya Watoto Wakiume'' Lulu Diva. NancyTheDreamtz

Soud Brown Amchomoa Mwijaku Mahabusu

Image
MTANGAZAJI wa runinga na msanii, Mwemba Burton, maarufu kwa jina la Mwijaku, leo Jumatatu, Agosti 3, 2020, ameachiwa kwa dhamana katika Mahakama ya Hakimu Mkazi jijini Dar es Salaam baada ya kusota mahabusu kwa siku kadhaa. Julai 29, 2020 mshtakiwa huyo alifikishwa mahakamani hapo na kusomewa mashitaka ya kusambaza picha za utupu ambapo alishindwa kutimiza masharti ya dhamana ambayo ni kuwa na wadhamini wawili kutoka Bongo Movie au tasnia ya muziki wenye barua zilizothibitishwa na Baraza la Sanaa Tanzania (BASATA), ambao watasaini bondi ya Sh 500,000 kila mmoja. Hatimaye, dhamana hiyo ameipata leo baada ya mtangazaji wa Clouds TV na Clouds FM, Soud Brown na Charles Mwendo,  kumdhamini mshtakiwa huyo. Kesi hiyo ipo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Richard Kabate, ambapo mshtakiwa huyo anadaiwa kuwa kati ya Septemba 17, 2019 na Oktoba 2019 katika jiji la Dar es Salaam alisambaza picha za utupu kupitia mfumo wa WhatsApp ambapo ni kinyume na sheria. Hakimu Kabate ameahirisha kesi hiyo hadi Agos

Mukutano mkuu CHADEMA umepitisha majina matatu

Image
Mkutano wa Baraza Kuu la CHADEMA, umepitisha majina matatu ya wanachama waliotia nia ya kuwania urais ambao ni Dk. Mayrose Majinge, Lazaro Nyalandu na Tundu Lissu.  Kati ya majina hayo, baraza leo litapendekeza jina moja litakalopitishwa na mkutano mkuu kesho kwa ajili ya kuwania urais kupitia CHADEMA katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 28, mwaka huu. NancyTheDreamtz

Mabinwa wa kombe la shirikisho wapokelewa Dar kwa shangwe

Image
Simba iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 mbele ya Namungo Uwanja wa Nelson Mandela hivyo wamerejea na taji la Kombe la Shirikisho. Ofisa Habari wa Simba, Haji Manara amesema kuwa wamerejea rasmi mjini kuendeleza shangwe la ubingwa walioutwaa Sumbawanga. "Mabingwa kama mabingwa tumerejea kuendelea na furaha kwa kuwa tumeshinda na tumerudi sasa kuendelea na furaha yetu Dar. "Mashabiki ni ngao yetu kubwa wamekuwa nasi bega kwa bega hivyo mambo mazuri yanakuja na tunafuraha kufikia malengo yetu," amesema. Wachezaji wa Simba wamepanda kwenye basi rasmi lililoandaliwa wakiwa na mataji mawili la Ligi Kuu Bara pamoja na Shirikisho wakiwa Kwenye msafara kuelekea Msimbazi. NancyTheDreamtz

Makocha 60 Waomba Kumrithi Eymael Yanga SC

Image
JUMLA ya makocha 60 wamewasilisha wasifu ‘CV’ za maombi ya kuifundisha Yanga katika msimu ujao wakimrithi aliyekuwa Kocha Mkuu wa timu hiyo, Mbelgiji Luc Eymael. Eymael alifutwa kazi ndani ya Yanga, Julai 27, mwaka huu baada ya kueneza taarifa zilizokuwa na viashiria vya ubaguzi wa rangi jambo ambalo linapigwa vita na familia ya michezo duniani kote. Timu hiyo hivi sasa ipo kwenye mchakato wa kumpata kocha mwingine na tayari wapo wanaotajwa kuifundisha Yanga ambao baadhi yao ni Hans Pluijm (Mbelgiji), Ernie Brandts (Mholanzi), Patrick Aussems (Mbelgiji) na Hitimana Thierry (Mrundi). Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Championi Jumamosi, bado uongozi wa Yanga unaendelea kupokea CV za maombi mengine ya makocha wakuu na wasaidizi kutoka nje na ndani ya nchi. Mtoa taarifa huyo alisema kuwa, wamepanga kufunga zoezi hilo la kupokea CV wiki ijayo na haraka watakutana na kuyapitia majina ya makocha hao kabla ya kufanya maamuzi sahihi ya kumteua kocha sahihi. Aliongeza kuwa vigezo watakavyo

Baada ya Kuachiwa Huru Rasmi Rapper Tekashi Aachia Video Mpya

Image
Baada ya kuachiwa huru rasmi rapper Tekashi tayari ameshaingia mitaa ya New York kushoot video mpya na ndani ya masaa 24 hayo hayo tayari ameiachia video hiyo 'Punani'  Rapper Huyo aliachiwa huru siku ya jana baada ya kutumikia kifungo chake cha nje (nyumbani) kwa miezi minne baada ya kuachiwa mapema kutoka gerezani kwa hofu ya kupata maambukizi ya corona. Ikumbukwe Tu Kuwa Rapper Tekashi 6ix9ine alikamatwa kwa makosa ya uhalifu na kutumia silaha kinyume cha sheria akihusishwa na makosa ya kundi lake la kihuni la kipindi icho NancyTheDreamtz

Maximo Rasmi Atuma CV Zake Yanga

Image
JINA la Mbrazili, Marcio Maximo ni kati ya makocha 60 waliotuma maombi ya kuifundisha Yanga katika msimu ujao. Yanga ipo kwenye mchakato wa kumpata kocha mpya atakayekuja kuinoa timu hiyo baada aliyekuwa kocha Mbelgiji, Luc Eymael kutimuliwa. Kocha mwingine anayetajwa kuwania kibarua cha Mbelgiji huyo ni Mfaransa, Patrick Aussems. Kwa mujibu wa taarifa ambazo limezipata Championi Jumatatu, Maximo amewasilisha maombi ya kuja kuifundisha timu hiyo. Mtoa taarifa huyo alisema kuwa kocha huyo ametuma CV zake wiki iliyopita na kuungana na makocha wengine 59 walioomba kukinoa kikosi hicho. Aliongeza kuwa uongozi wa timu hiyo umepanga kukutana wiki hii kwa ajili ya kupitia maombi na CV za makocha wote kabla ya kufanya mchujo. Maximo hivi karibuni aliliambia gazeti hili kuwa: “Nipo tayari kujiunga na Yanga kama wakinihitaji, hivi sasa nipo nafundisha timu ya taifa ya Naguya iliyopo Amerika Kusini.” NancyTheDreamtz

Majimbo Matatu Pasua Kichwa Uchaguzi Mkuu 2020

Image
DAR: WAKATI mchakato wa kuwapata wagombea ubunge kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) ukizidi kushika kasi, majimbo matatu ya Arusha Mjini, Mbeya Mjini na Tarime Vijijini, yameelezwa kuwa pasua kichwa kutokana na mchuano mkali unaotarajiwa kuelekea Oktoba 28, 2020. RISASI linachambua………… Mchuano huo unatarajiwa kuhusisha CCM na Chama kikuu cha upinzani nchini- Chadema ambacho wagombea wake wanatetea majimbo hayo ilhali CCM ikijiapiza kurudisha himaya yake. Majimbo hayo yamekuwa na mvuto wa kipekee baada ya wagombea waliojitokeza na kushinda katika mchakato wa kura za maoni CCM, kunogesha mpambano kutokana na mizizi waliyojijengea kisiasa huku umaarufu wa majina yao ukizidi kuwapasua kichwa wapiga kura. ARUSHA MJINI Mojawapo ya jimbo linalotazamiwa kunogesha uchaguzi mkuu ni Arusha Mjini ambalo mpambano wake unatarajiwa kuwa kati ya Mbunge aliyemaliza muda wake, Godbless Lema (Chadema) na Mrisho Gambo kutoka CCM. Gambo ambaye alikuwa miongoni mwa makada 29 wa CCM waliokuwa wamechukua fomu

PABLO ESCOBAR: Mfalme wa Cocaine, Anadaiwa Kuuwa Watu 70,000

Image
Kutana na Pablo Emiliano Escobar mzaliwa wa Colombia ambaye alifahamika kama Mfalme wa Cocaine kutokana na kazi yake ya usamabazaji wa dawa za kulenya aina ya Cocaine nchini Marekani na Colombia. Kutokana na kazi yake ya uuzaji wa dawa za kulevya jeshi la Marekani pamoja na Colombia liliungana ili kumkamata Pablo Escobar mwaka 1993 na ndipo walipofanikiwa kumuua kwa kumpiga risasi ya kichwa mnamo December 2,1993. Bonyeza PLAY kusikiliza historia.  VIDEO: NancyTheDreamtz

Binadamu Kuishi Milele Kama zoezi la Kuunganisha Ubongo na Mfumo wa Komputa Litakamilika

Image
Je utamani kuishi milele?. Huko nchini Marekani mjasiriamali mmoja wa masuala ya teknolojia, Eloni Musk anadhanii binadamu huwenda wakaepuka kifo kutokana na ujio wa teknolojia mbalimbali duniani. Mwanasayansi huyo kwa sasa anashughulikia teknolojia ambayo itaunganisha mfumo wa ubongo wa binadamu na komputa hali ambayo itazuia miili ya binadamu kutozeeka na kufungua miingiliano na kidigitali daima. Musk amedai mfumo huo utaweza kumsaidia binadamu kuishi bila kuzeeka na kuunganisha miili ya binadamu na mifumo ya kigitali. Ubongo wa binadamu una nyaya 68 mtandao ambao unaweza kuunganisha mfumo wa ubongo wa binadamu na wakomputa. Pia wamedai mfumo huo unaweza kuamisha akili za binadamu na kuzipeleka kwenye mfumo wa komputa lakini wadau wa mambo wamedai mfumo huo hauwezi kufanya kazi kwa kuwa ubongo wa binadamu una siri nyingi. Mfumo huo ambao umepewa jina transhumanism, umeonekana kupingwa na wadau wengi wa sayansi kwa madai akili za binadamu haziwezi kuamishika. NancyTheDreamtz

SNURA amjibu SHILOLE: Ananichukia, Anamtaka MENEJA wangu asifanye kazi na mimi, Ni WIVU hajaanza leo

Image
SNURA amjibu SHILOLE: Ananichukia, Anamtaka MENEJA wangu asifanye kazi na mimi, Ni WIVU hajaanza leo VIDEO: NancyTheDreamtz

Bilionea Laizer auza madini mengine kwa Serikali (+Video)

Image
Leo Agosti 3, 2020, Bilionea mpya nchini Saniniu Laizer, ataikabidhi Serikali jiwe lingine la Tanzanite. Makabidhiano hayo yanafanyika eneo la Mirerani wilayani Simanjiro mkoani Manyara. Related Articles NancyTheDreamtz

Aston Villa kumng’oa mshambuliaji wa Liverpool

Image
Kocha wa Aston Villa, Dean Smith anakusudia kukiimarisha kikosi chake katika safu ya ushambuliaji baada ya kufanikiwa kuepuka kushuka dara kutoka Premier League. Katika kuhakikisha inafanikiwa katika hilo, wamekusudia kumsajili mshambuliaji wa Liverpool, raia wa Ubelgiji Divock Origi, 25. Origi amefanikiwa kucheza jumla ya michezo 44 pekee ndani ya Liverpool msimu huu uliyomalizika, lakini mara zote amekuwa mtu wa kusugua benchi akiwapisha Mo Salah, Sadio Mane na Roberto Firmino wakianza.(Sun) Mabingwa wa kombe la FA klabu ya Arsenal wanamlia rada beki wa kati raia wa Brazil, Diego Carlos huku Mikel Arteta akikusudia kukisuka upya kikosi chake kwaajili ya msimu ujao. (Telegraph – subscription required) Arsenal inatarajia kutoa ofa nono kwa mshambuliaji wake raia wa Gabon, Pierre-Emerick Aubameyang 31, wiki hii ya pauni milioni 250,000 kwa wiki katika makubaliano ya miaka mitatu kuendelea kusalia kwenye klabu hiyo. (Mirror) Troy Deeney alifunga bao lake la 10 katika Ligi ya Premier msim

Tetesi za Usajili nchini Tanzania kwa klabu za Ligi Kuu

Image
Wakati Dirisha la usajili kwa Klabu za Ligi Kuu ya Vodacom (VPL), Ligi Daraja la Kwanza (FDL), Ligi Daraja la Pili (SDL) na Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) likiwa limefunguliwa Agosti 1,2020. Huku Klabu zikitarajiwa kufanya usajili kwa muda wa mwezi mmoja ambapo dirisha litafungwa Agosti 31 saa 5:59 usiku, hizi ndiyo tetesi za Usajili kwa sasa Tanzania. Zawadi Peter Mauya  @giftmauya  ametia saini mkataba wa miaka miwili kuwatumikia Wananchi kabu ya Yanga. (Yanga) Beki kisiki, Bakari Nondo Mwamnyeto  @bakarmwamnyeto  amejiunga na kikosi cha Timu ya Wananchi, Yanga kwa kandarasi ya miaka miwili. (Yanga) Timu ya Wananchi imeendelea kujiimarisha baada ya kuinasa saini ya Yassin Mustapha Salum  @yassaboy23  kutoka Polisi Tanzania.(Yanga) Harakati zinaendelea kuimarisha kikosi cha Timu ya Wananchi na jana wamemalizana na mshambuliaji mahiri, Waziri Junior  @wazir_junior_10  kutoka Mbao FC. (Yanga) Inadaiwa Simba SC inakaribia kumsajili mshambuliaji wa Ghana, Michael Sarpong baada ya kufeli kwa m

Manchester United yamalizana na Alexis Sanchez

Image
Manchester United hatimaye imemalizana na Alexis Sanchez baada ya klabu ya Inter Milan kukubali kumsajili nyota huyo raia wa Chilea moja kwa moja, kwa mujibu wa ripoti kutoka nchini Italia. Kwa mujibu wa gazeti la Corriere della Sera la Itali, limeripoti kuwa Mkurugenzi wa michezo wa Inter Milan,  Beppe Marotta amekubaliana dili hilo na United, ambalo litashuhudiwa miamba hiyo ya soka kutoka Serie A ikitoa kitita cha paundi milioni 13.5 kwaajili ya Sanchez. Inadaiwa sehemu ya makubaliano hayo ni kuwa nyota huyo atatangazwa rasmi baada ya mchezo wao dhidi ya Getafe wa michuano ya Europa League siku ya Jumatano. Inter inamsajili Sanchez kwa dau la paundi milioni 13.5 kwa mkataba wa miaka mitatu ambapo atasalia hapo hadi mwezi Juni mwaka 2023. Winga huyo mwenye umri wa miaka 31 alipaswa kurejea United, Agosti 7 ili kwenda kumalizia miaka yake miwili lakini sasa atasalia hapo. Sanchez amejiunga na United mwezi Januari, 2018 akitokea. NancyTheDreamtz