Posts

Showing posts from December 20, 2018

CHADEMA Kulipa Fidia Wananchi Waliobomolewa Nyumba zao

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa jimbo la Ubungo, Saed Kubenea (CHADEMA) amewataka wananchi wa Ubungo kuhifadhi vyema nyaraka zao za maeneo waliyobomolewa na kwamba CHADEMA ikiingia madarakani watahakikisha wanawalipa fidia zao.   Kubenea ameyasema hayo jana  ikiwa ni siku moja kupita tangu Rais John Pombe Magufuli alipotamka hadharani kuwa wahanga waliobomolewa nyumba kuanzia maeneo ya Ubungo hawatalipwa fidia kwa kuwa walivunja sheria kwa kujenga kwenye hifadhi ya barabara. Akizungumza jana na wanahabari, Kubenea amedai kushangazwa na kauli ya rais kwamba waliovunjiwa nyumba walijenga kwenye hifadhi ya barabara lakini serikali ndiyo iliyokuwa ikipokea kodi zao, kuwapatia hati za maeneo, kuwawekea maji na umeme huku wakijua hilo ni eneo la hifadhi. "Naomba wananchi wa Ubungo, Kimara waliovunjiwa nyumba zao wahifadhi vizuri nyaraka zao. Mungu akipenda Sisi CHADEMA tukiingia madarakani tutalipa waathirika wote waliobomolewa kuanzia ubungo hadi Kibaha. Inawezekana siyo laz

Diamond, Rayvanny Waiomba Msamaha BASATA na Serikali .....Waahidi Kutorudia Makosa

Image
NancyTheDreamtz Mwanamuziki Diamond Platnumz na Rayvanny wameomba radhi kwa kuimba wimbo wa Mwanza uliofungiwa na Baraza la Sanaa la Taifa (Basata), huku wakiwasihi wasanii wenzao kuwa mabalozi wazuri wa utamaduni wa Tanzania. “Kwa unyenyekevu mkubwa tunaomba radhi Serikali, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Basata na kila aliyekwazika tulivyoimba wimbo wa Mwanza katika Wasafi Festival mkoani Mwanza,” amesema Diamond. Wanamuziki hao wameomba radhi baada ya Basata kutangaza kuwafungia kwa muda usiojulikana likidai kufikia uamuzi huo baada ya wasanii hao Jumamosi Desemba 15, 2018 kuonyesha dharau kwa kuimba wimbo wa Mwanza uliofungiwa na baraza hilo. Mbali na kuwafungia wanamuziki hao, Basata imetangaza kukifuta kibali cha Tamasha la Wasafi Festival. Video inayosambaa mtandaoni leo Ijumaa Desemba 21, 2018 inamuonyesha Diamond akiwa pamoja na Rayvanny, kwa pamoja wakiomba radhi mamlaka husika. “Japo tunajitahidi kuwa vijana wenye mfano bora kwa Taifa

Bao Alilofunga Ndemla Jana Dhidi ya KMC Lazua Gumzo

Image
NancyTheDreamtz Shuti alilopiga kiungo wa Simba, Said Hamis Ndemla dakika ya 14 akimalizia pasi ya Mzamiru Yasin na kumshinda mlinda mlango wa KMC Jonathan Nahima, limekuwa gumzo kubwa. Simba ilishinda kwa mabao 2-1 katika mechi ya Ligi Kuu Bara kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam, jana. Shuti hilo la Ndemla akitumia mguu wa kulia nje ya 18 limekuwa gumzo kubwa mitandaoni. Ndemla alipiga shuti hilo haraka sana baada ya kupokea pasi kutoka kwa Mzamiru na kuwaduwaza KMC. Mjadala huo umekuwa ukiendelea namna shuti hilo alivyoweza kulipiga haraka na kuweza kulenga lango. Ndemla amekuwa akikaa benchi kutokana na Simba kuwa na kikosi kipana lakini jana alikuwa mmoja wa wachezaji walioonyesha wanaweza kufanya vema wakipata nafasi.

Paul Pogba Aonyesha Furaha Yake Muda Mchache Baada ya Mourinho Kutimuliwa Man U

Image
NancyTheDreamtz Muda mchache baada ya kocha Jose Mourinho kutimulia ndani ya Manchester United, mchezaji ghali zaidi ndani ya timu hiyo Paul Pogba ameonesha kufurahishwa na uamzi huo. Kupitia mtandao wa Twitter Pogba ameweka picha iliyoambtana na ujumbe unaotaka wafuasi wake kuweka maoni yao juu ya picha hiyo. Hata hivyo Pogba aliifuta picha hiyo baada ya muda mfupi. Naye mkongwe wa klabu hiyo ambaye pia ni kocha, Gary Neville ameunga mkono ujumbe wa Pogba kwa kuuandika na kuweka kwenye ukurasa wake. Vyanzo mbalimbali pia vinataja makocha kadhaa ambao wanaweza kuchukua nafasi ya Mourinho mwisho wa msimu huu baada ya klabu kuweka wazi kuwa kocha wa muda atakayetangazwa ndani ya saa 48 atadumu hadi mwisho wa msimu.

Kimenuka Diamond Afuta Picha zote za Mrembo Tanasha Instagram....Tanasha Afunguka Haya...

Image
NancyTheDreamtz Kimenuka Diamond Afuta Picha zote za Mrembo Tanasha Instagram....Tanasha Afunguka Haya huku na yeye pia akifuta picha zote alizowahi kipiga na Diamond... _ From #tanashadonna - Just to make things clear... D and I came to a mutual understanding that it may be too soon to be Kwanini Uteseke? Jipatie Dawa Bora ya Matatizo Mbali Mbali kwa Afya Yako with our relationship on social media right now. So we decided to keep our relationship private for the moment until we feel like going public again. May God bless you all .🙏❤️

Mbasha Amtolea Povu Zito Shabiki Alimwambia Anajichubua

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa nyimbo za injili nchini Emmanuel Mbasha amtole povu la kufa mtu shabiki yake katika mtandao wake wa instagram ambae anadai kuwa weupe wa Mbasha ni wa kujichubua. Mbasha amtolea uvivu shabiki huyo na kumpa za uso huku akimwambia kuwa weupe wake ni wa asili wala sio wa kuchakachua. Hiki ndicho alichoandika: hivi wewe unayenipakilia kwenye comment kwamba niache mkorogo nani alikwambia mie najicream sijawahi kujicream weupe wangu ni waasili waulize wanaonijua wakueleze, sawa na sura yako mbaya ilivyo ya asili domo kubwaa hata lipsi halina wanja sasa lipua kubwa kama bukta ya fudenge😀😀 macho kama mzeee wa likwidiii mamaanakufaa....kabala hujaniponda kwanza jiangalie wewe kwanza cheki mikorogo ilivyokukataaa jamani watu wa bongo muvi mkitaka kuigiza picha ya kutisha hapa kunajitu halihitaji hata mekapuuu.eti mamawatatu jamani haya mumfolo mkajionee @apoloniapeter12 kila siku unanipondaga tu navumilia haya leo Utajibeba

Diamond Platnumz Atishia Kuondoka Tanzania na Kuchukua Uraia Kenya

Image
NancyTheDreamtz Ameandika Ibrahim Augustine Mwimbaji maarufu na CEO wa WCB namzungumzia Diamond platnumz ametishia kuondoka Tz na kuhamia nchini Kenya hii ni kwa sababu nyimbo zake kufungiwa kila wakati na BASATA Maneno haya ameyasema kipindi akihojiwa na Times FM , nimekutana na Video Youtube Niki nukuu maneno yake "Mimi kama nyimbo zangu wataendele kuzifungia fungia hivi itabidi nisepe sasa wanataka tifa na mama yangu wale nini makaratasi?,mziki ndio ajira yangu naweza nikaenda hats Kenya na mambo yakawa fresh" Nini unajifunza Nimegundua kwamba msanii diamond anatumia cheo chake kikubwa ama wadhfa wake kuitishia BASATA Ili basata wamfungulie I swear wakifanya hivi wanaua vizazi kitu ambacho hakifai kwani hawezi kuimba nyimbo bila kuweka video au maneno ya matusi Mimi kama anataka asepe aondoke tena hata sasa hivi asituharabie maadili ya watoto wetu sasa hivi mitaani watoto wetu wanaongea maneno ya ajabu na machafu hata mbele za wageni (ila Mimi sijaoa na wale sina mke i