Posts

Showing posts from December 9, 2018

Nape Nnauye: CCM Imevamiwa na Wasaka Tonge

Image
NancyTheDreamtz Na Bakari Chijumba, Mtwara. Wakati sakata la Katibu mkuu wa Chama Cha Mapinduzi Dr.Bashiru Ally na kada wa Chama hicho, Bernard Membe likiendelea kuchukua nafasi kubwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii, mbunge wa Mtama Nape Nnauye ameibuka na kusema CCM imevamiwa na wasaka Tonge wenye maslahi na matumbo yao kuliko chama. Nape Nnauye ambaye ni mbuge wa Mtama, ametoa kauli hiyo baada ya kuenea kwa taarifa kuhusu madai ya  kuanzishwa kwa chama kipya kitakachoitwa USAWA, ambapo Bernard Membe na Nape Nnauye wametajwa kuwa miongoni mwa watakaotimkia kwenye chama hicho kipya. Taarifa iliyoandikwa kwenye ukurasa wa facebook unaofahamika kwa jina la "Sauti ya Kisonge" na kuenezwa kwenye mitandao hii leo, inadai Chama hicho kinachotarajiwa kusajiliwa hivi karibuni, kinawahusisha pia  mawaziri kadhaa wa utawala uliopita, mawaziri wanne kutoka Zanzibar  na mabalozi kadhaa wastaafu na waliopo nje. "Chama Kipya kinachotarajiwa kusajiliwa hivi karibuni kwa jina

IKULU Yampongeza Msanii Diamond...Mwenyewe Afunguka Maneno Mazito

Image
NancyTheDreamtz Baada ya ukurasa wa kijamii wa instagram wa Ikulu kumpongeza msanii Diamond Platnumz kwa mchango wake wa maendeleo ya jamii ikiwemo kuchangia shule ya msingi ya Sumbawanga katika ujenzi wake hatimaye mwanamuziki huyo ameandika ujumbe wa shukrani kwa Serikali  kwa kutambua mchango wake na sanaa kwa ujumla. Diamond ambaye kwa sasa yupo Sumbawanga kwaajili ya tamasha lake la Wasafi Festival, amekubali kubeba jukumu la kujitolea kuimalizia shule ya Msingi ya Sumbawanga ambayo ilihitaji milioni 68 ili kuhakikisha imemalizika na kuanza kupokea wanafunzi mwezi Januari ambapo aliridhia kubeba jukumu hilo huku akiongezea kuwa yupo tayari kujitolea na mabati 150. Advertisement

Angalia SABABU Ya Diamond Platnumz KUANGUKA JUKWAANI Huko SUMBAWANGA.

Image
NancyTheDreamtz

Diamond akiongea baada ya kuanguka jukwaani Sumbawanga

Image
NancyTheDreamtz

Sababu diamond na rayvanny kuanguka stejini sumbawanga wasafi festival

Image
NancyTheDreamtz

Irene Uwoya Adai Kuwa Hataki Kuolewa Tena

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa Bongo movie na mjasiriamali Irene Uwoya ameibuka na kuweka wazi kuwa hakuna kitu hataki kusikia maishani Mwaka kwa Hivi sasa Kama kuolewa tena au ndoa. Uwoya amefunguka na kusema kuwa amefikia kwenye uamuzi huo kwani aliyokutana nayo ndani ya ndoa yameshatosheleza moyo wake hivyo kwa sasa yupo kwa ajili ya kuangalia maisha yake na si vinginevyo. Katika mahojiano yake aliyofanya na Gazeti la Ijumaa Wikienda, Uwoya alisema kuna vitu vingi anavyo moyoni, lakini pia anaona siyo vyema kuwapa watu faida na ndiyo maana alikuwa anakaa kimya kwa muda mrefu tangu kusambaa kwa habari zake za kuachana na Abdulaziz Chende ‘Dogo Janja’. Kiukweli kabisa nimeapa moyoni mwangu sitaki kabisa kusikia kama kuna kitu kinaitwa ndoa kwa sababu nahisi hivyo vitu kwenye maisha yangu vimeshapita, sihitaji kuvirudia, naangalia maisha mengine ya kujiendeleza mwenyewe. Kama sasa hivi nina kazi kubwa ya kumalizia pub (baa) yangu ya Last Minute (ipo Sinza-Mori, Dar). Kwa hiyo akili y