Posts

Showing posts from October 16, 2018

Samatta na Msuva waiangamiza Cape Verde Uwanja wa Taifa

Image
NancyTheDreamtz Washambuliaji wawili wanaochezea soka la nje Mbwana Ally Samatta na Saimon Msuva wamefanikiwa kuitoa kimasomaso timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars baada ya kuisaidia kuibuka na ushindi wa goli 2-0 dhidi ya wapinzani wao Cape Verde. Ikumbukwe katika mchezo wa kwanza ambao ulifanyika Cape Verde Taifa Stars walipoteza kwa kufungwa jumla ya goli 3-0. Magoli ya leo yamepatikana dakika ya 28 goli lililofungwa na Saimon Msuva baada ya kupokea mpira kutoka kwa Samatta,hadi mapumziko timu hizo zilienda kwa Stars kuongoza kwa goli moja licha ya Samatta kukosa mkwaju wa penati mnamo dakika ya 23 ya mchezo. Kipindi cha pili kilipoanza Stars walijipatia goli la pili mnamo dakika ya 58 lililofungwa na mshambuliaji wa klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji Mbwana Ally Samatta baada ya kupokea pasi kutoka kwa Mdathiri Yahya na Samatta kufanikiwa kumalizia goli hilo kwa shuti kali. Lakini mnamo dakika ya 89 taa za Uwanja wa Taifa zilizima na mashabiki kuwasha taa za simu zao kuon

Msanii Lulu Diva baada ya ngoma yake ya “Ona” ft Mavoko kufanya vizuri ameachia video ya “Alewa” aliyomshirikisha S2kizzy (+Video)

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa muziki wa kizazi kipya Lulu Diva alimaarufu Sexy lady ameachia video ya ngoma yake ya “Alewa” ambayo amemshirikisha mwandaaji wa muziki (Producer) katika studi za Switch rekodi S2kizzy. Msanii huyo wakati anaongea na Bongo five wiki moja iliyopita alifunguka na kusema kuwa nyimbo hiyo imeandikwa na S2kizzy ambaye pia ndio Producer wa ngoma hiyo lakini video ikitengenezwa na Director Ivan.

Mhe. Lema amlipua Waziri Lugola na Kamanda Mambosasa sakata la kutekwa Mo Dewji ‘heti Kamera hazikunasa gari vizuri’ (+video)

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Arusha Mjini kwa Tiketi ya CHADEMA, Godbless Lema ambaye pia ni Waziri Kivuli wa Mambo ya Ndani amefunguka kwa mara ya kwanza kuhusu tukio la kutekwa kwa Mfanyabiashara maarufu nchini Tanzania, Mo Dewji. Lema akizungumza na Waandishi wa Habari leo Oktoba 16, 2018 jijini Dar Es Salaam amehoji vitu kadhaa zikiwemo kauli zilizotolewa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola na zile taarifa zilizotolewa na Jeshi la Polisi Kanda maalum ya Dar Es Salaam.

Irene Uwoya afunguka kuhusiana na ndoa yake na Dogo Janja “Alishawahi kuchepuka kwenye ndoa”

Image
NancyTheDreamtz Msanii muigizaji kutoka katika tasnia ya Bongo Movie Irene Uwoya amefunguka mwanzao mwisho kuhusiana na maisha yake lakini pia kuhusiana na maisha ya ndoa ambayo alioana na msanii wa muziki wa kizazi kipya Dogo Janja. Msanii huyo ameongea hayo wakati anapiga stori katika kipindi cha PlayList kinachofanyika katika kituo cha habari cha TimesFm, Irene amefunguka kuhusiana na maisha yake lakini haswa kuhusiana na yale yanayoendelea kuenea kwenye mitandao ya kijamii kuhusiana na ile kinachosemekana ameachana na mume wake huyo ambaye ni Dogo Janja. Irene amesema kuwa ” Yeye kuonekana yuko nje ya nchi akionekana anakula bata bila Dogo Janja,Kila mtu anazungumza kile anachohisi kuzungumza na mimi siwezagi kuongelea mambo yangu kwenye media, Mimi kuonekana nje niko kwenye biashara zangu mbona Dogo Janja akiendaga kufanya video za nyimbo zake mfano Afrika ya Kusini hanibebagi ? kwahiyo mimi naendaga kibiashara kama yeye anavyoendaga kikazi. lakini katika ndoa yake haon