Posts

Showing posts from July 11, 2021

Zari Ammisi Diamond Platnumz

Image
B AADA  ya kuachana  na bwana’ke mwingine  aliyepewa jina la Dark  Stallion (Farasi Mweusi),  baby mama wa staa wa muziki  barani Afrika, Nasibu Abdul  au Diamond Platnumz, Zarinah  Hassan au Zari The Boss Lady  amesababisha sintofahamu,  IJUMAA limedokezwa.   Mwanamama Zari ambaye ni  raia wa Uganda mwenye maskani  yake, Durban nchini Afrika  Kusini, amesababisha mjadala  mpya kutoka kwa wafuasi wake  almaarufu Team Zari kwamba ni  rasmi sasa amerejesha majeshi  kwa mwamba Diamond.   ZARI AMEMMISI MONDI? Team Zari wanadai kwamba,  Zari amesababisha mshangao  kwao baada ya kudaiwa kummisi  Diamond au Mondi; muda mfupi  baada ya kumwagana na huyo Dark  Stallion ambaye jina lake halisi  ni Frederick Nuamah, mwigizaji  na prodyuza mkubwa wa filamu  nchini Ghana. Zari ambaye ni mama wa watoto  watano, anasema kuwa, anammisi  mtu f’lani ambaye Team Zari  wanadai si mwingine, bali ni  Mondi. TIFFAH ATHIBITISHA Madai hayo ya Team Zari  yanathibitishwa na binti yake  ambaye Zari amezaa na Mond