Posts

Showing posts from April 10, 2020

Ifahamu Siku ya Ijumaa Kuu Kiundani...

Image
NancyTheDreamtz Siku kama ya leo saa tisa alasiri, ni maarufu kama Ijumaa Kuu, katika nyumba za ibada za Kikristo, kimya hutanda, mishumaa huzimwa na kuashiria kuwa ni siku ya majonzi. Ijumaa Kuu ni siku ambayo Wakristo duniani kote hukumbuka mateso aliyoyapata Yesu Tanzania ni miongoni mwa nchi ambazo zimeipa thamani siku hii kwa kuitangaza kuwa ya mapunziko. Siku hii huadhimishwa kwa ibada inayoambatana na kusoma mistari ya Biblia inayoelezea undani wa matukio yaliyosababisha kusulubiwa kwa Yesu Kristo miaka zaidi ya 2000 iliyopita. Hii ni siku ambayo inatajwa kuwa na maana kubwa katika imani ya Kikristo. Waumini wanaamini kwamba, kusulubiwa na kufa kwa Yesu, kumeleta ukombozi duniani kote. Ijumaa Kuu haithibitishwi tu na vitabu vya dini, bali hata machapisho ya kihistoria, yanathibitisha juu ya kusulubiwa na kufa kwa Yesu. Huadhimishwa kwa ibada huku zikitawaliwa na mistari na nyimbo za maombolezo ya kufa kwa Yesu. Rangi za vitambaa vipamb

Sakata la Mameya wa Chadema Kuondolewa Madarakani Latinga Bungeni

Image
NancyTheDreamtz Dodoma. Sakata la kuondolewa kwa mameya wawili wa halmashauri zilizokuwa zikiongozwa na Chadema limetinga bungeni ambapo Mbunge wa Iringa Mjini, (Chadema), Peter Msigwa amesema hata barua ya kukata rufaa iliyoandikwa kwa Waziri wa Tamisemi, Selemani Jafo haijajibiwa. Msigwa aliwataja walioondolewa kuwa Meya wa Iringa Mjini, Alex Kimbe na Meya wa Jiji la Dar es Salaam, Isaya Mwita ambaye ameandika barua ya rufaa mwezi mmoja uliopita. Akichangia mjadala wa bajeti ya Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi) kwa mwaka 2020/2021, leo Alhamisi Aprili 9, 2020 Msigwa amesema Manispaa ya Iringa ni miongoni mwa manispaa bora na nzuri nchini. Amesema katika kipindi cha miaka mitano akiwa mbunge wamekuwa na hati safi, wamekusanya mapato, wamepatiwa zawadi ya usafi na madiwani wengine kufika kujifunza chini ya uongozi wa meya huyo. Amesema Serikali imekuwa ikijinasibu kukataa wizi lakini wamekuwa na meya huyo ameweza kusimamia jam

Gwajima Aiomba Radhi Congo Kuhusu Chanjo ya Corona

Image
NancyTheDreamtz Askofu wa kanisa la Ufufuo na uzima, Josephat Gwajima amesema kuwa ameomba radhi kwa wananchi wa DRC Congo baada ya kutoa kauli kuwa nchi hiyo imekubali kufanyiwa majaribio ya chanjo ya Covid 19. Gwajima alitoa mahubiri ya kukemea kitendo hicho siku chache tu baada ya umoja wa madaktari kutoka nchini Ufaransa kusema kuwa itaanza kufanya majaribio ya chanjo za Corona Akizungumza kwenye kipindi cha 360 cha kituo cha televisheni cha Clouds tv jijini Dar es salaam leo, Gwajima amesema alipewa taarifa zisizo sahihi kabla ya mahubiri yake “Niliwaomba msamaha wakongo maana kabla ya ibada niliambiwa kuwa Kongo wameshaanza majaribio nikasema kwenye ibada lakini baadaye nikajua ukweli kwamba hakuna majaribio yoyote yale nikapiga simu kwa wakongo,”amsema  Gwajima. Shirika la Afya Duniani (WHO) limesema Afrika sio sehemu ambayo chanjo ya corona itafanyiwa majaribio.