Posts

Showing posts from September 8, 2018

Haya Hapa Matokeo ya Mpira Kati ya Tanzania na Uganda Jioni ya Leo

Image
NancyTheDreamtz Tanzania wanafanikiwa kurudi nyumbani na pointi 1 kwa sare tasa dhidi ya Uganda Cranes katika mchezo wa kuwania kufuzu kucheza mashindano ya African Cup of Nations 2019.

Flavian Matata Akutana na Nick Minaj Baada ya Kumpamba Kucha

Image
NancyTheDreamtz Baada ya Kupata Deal ya Kupamba Kucha za One of the Best female Rapper Kutokea Pande za Marekani @nickiminaj , Mwanamitindo Maarufu @flavianamatata amekutana nae na Kupata Picha ya Pamoja kwenye Tukio la Utolewaji wa Tuzo za #FMAS2018 August 21 Mwaka Huu, Flaviana Kupitia Account yake ya Twitter aliandika kuwa #NickiMinaj alitumia Product za Lavy Namba 29, wakati wa kupiga picha zilizotumika kwenye Jarida la Fashion la @voguearabia la Mwezi September Mwaka Huu

Rais Magufuli Asema Mkuu wa mkoa wa Simiyu Antony Mtaka Ndo Anayeongoza Kwa Kuchapa Kazi Vizuri Tanzania Nzima..Makonda Je?

Image
NancyTheDreamtz Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amemtaja mkuu wa mkoa wa Simiyu Mh. Anthony Mtaka, kuwa ndiye mkuu wa mkoa kinara anayepiga kazi na kwamba hana mfano licha ya kupuuzwa kabla  hajamteua. Hayo ameyasema leo mkoani Simiyu wakati akihutubia wananchi wa mkoa huo kwenye mkutano wa hadhara uliofanyika jioni hii ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya siku 7 katika mikoa ya kanda ya ziwa. Rais Magufuli ameeleza kuwa, wakati anajaribu kutafuta wakuu wa Wilaya na wakuu wa mikoa aliambiwa na vyombo vyake kuwa Mtaka hafai hata U-DC lakini yeye akaamua kumteua kuwa mkuu wa mkoa kwasababu anajua watu wazuri huwa wanapingwa vita sana. ''Nilipotaka kumteua niliuliza vyombo vyangu nikaambiwa hafai kabisa lakini nimeuliza ripoti ya Wakuu wa Mikoa wanaofanya kazi vizuri, wakaniletea Mtaka ndio namba moja na namba mbili ni yeye kwa kifupi hana mfano'', amesema. Aidha Rais Magufuli ambaye atakamilisha ziara yake katika mikoa hiyo siku ya Jum

Masanja Mkandamizaji Aingia Katika Bifu Zito na Kanye West

Image
NancyTheDreamtz Mchekeshaji Masanja Mkandamizaji amuwakia Rapper Kanye West hii ni baada ya kuandika ‘Sisi ni Miungu’ kupitia ukurasa wake wa twitter na wengi kutafsiri kuwa anajiita Mungu kitu ambacho sio kizuri. Masanja Mkandamizaji ambaye pia ni mchungaji amechukulia kitu hicho kuwa ni dharau na kusema mtu akishapata hela anasahau kama kuna Mungu na badala yake anajiita yeye Mungu. Kupitia ukurasa wa twitter wa Masanja ameandika mawazo yake kuhusiana na kile alichokiandika Kanye West na kusema “Acha Kuvuta bangi, huwa una umama sana”

Hiki ndicho alichokishutumu Obama kutoka kwa Trump akiuita ni “Upuuzi unaotoka White House”

Image
NancyTheDreamtz Aliyekuwa rais wa Marekani Barrack Obama amemshutumu mrithi wake Donald Trump na mambo ya ‘kipuuzi yanayotoka’ katika ikulu ya Whitehouse. kwa kusema ”Hii sio kawaida huu ni wakati usio wa kawaida na ni wakati hatari”, Obama aliwaambia wanafunzi katika chuo kikuu cha Illinois. Alitaka kurejeshwa kwa uaminifu na heshima na sheria kufuatwa katika serikali, Rais huyo wa zamani amekuwa akifanya mambo yake kwa siri tangu alipoondoka mamlakani 2017. Bwana Obama aliambia sherehe hiyo ya kuwatuza wanafunzi mjini Urbana jimbo la Illinois kwamba amekuwa akitaka kufuata utamaduni wa marais wa zamani kupitia kuondoka katika ulingo wa kisiasa. Badala yake aliushutumu utawala uliopo wa Republican. Akimjibu, rais Trump alisema katika mkutano wa mchango wa Republican huko fargo kaskazini mwa Dakota siku ya Ijumaa kwamba aliitazama hotuba ya mtangulizi wake ,”lakini nililala”. ”Bwana Obama alijaribu kujipatia sifa ya mambo mazuri yanayoendelea nchini”, Wanachama wa Democr

Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth afunguka kilichombeba ‘sijabebwa’

Image
NancyTheDreamtz Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth amefunguka mwanzo mwisho kile kilichopelekea kushinda taji hili la U-Miss kwa walikuwa wanashindana na warembo wengi halafu wazuri. Queen alisema “Nafurahia kushinda taji ili najisikia vizuri sana asante Tanzania” akiongeza “ukiwa kama mrembo lazima ujiandae kama unavyoona warembo ni wazuri sio kwamba ni wazuri kumuonekano tu hata kichwani pia wako vizuri” Hapa ndio maelezo yake:-

Hili ndio Swali la Mobetto lililompa ushindi Miss Tanzania 2018 Queen Elizabeth

Image
NancyTheDreamtz Mashindano ya Miss Tanzania yamemalizika kwa mrembo, Queen Elizabeth kutoka Zone ya Dar es salaam kuondoka na taji hilo huku akiwamwaga wenzake 19. Baada ya kuingia tano bora. Warembo hao waliulizwa na maswali na aliyejibu vizuri alijichukulia maski nyingi kutoka kwa majaji,kati ya warembo hao kuna wengine walijibu vizuri huku mmoja wao akipata kigugumizi wakati wa kujibu swali husika. N kati ya warembo hao warembo watatu walijibu maswali kwa lugha ya Kiingereza huku warembo wawili yaani aliyeshika nafasi ya tano na ya nne hao waliweza kujibu maswali kwa kutumia lugh ya taifa ya kiswahili huk mshindi namba tatu mpaka namba moja wakijibu kwa lugha ya kiingereza. Na haya ndio miongoni mwa maswali waliyoulizwa na hapa ndio mshindi wetu anajibu swali baada ya kuulizwa na mshereheshaji wa sherehe hiyo mwanamitindo Hamissa Mobetto.

Hamisa Mobetto kusimamia Show Miss Tanzania 2018

Image
NancyTheDreamtz Mwanamitindo Hamisa Mobetto ndiye atasimama kama host wa shindano la Miss Tanzania ambalo litafanyika usiku wa leo September 08, 2018. Mrembo huyo anachukua nafasi huyo akiwa na uzoefu wa kutosha na mashindano kama hayo kwa kuwa ameshashiriki hadi Miss Univeristy Afrika. Utakumbuka mwaka 2010 alitwaa taji la Miss XXL, After School Bash, mwaka uliofuata Hamisa alishiriki mashindano ya Miss Dar Indian Ocean na kushika nafasi ya pili, pia aliwahi kufanikiwa kuingia nusu fainali ya Miss Tanzania. 

Magufuli aagiza uchunguzi madai ya maji yenye sumu

Image
NancyTheDreamtz Rais , John Magufuli, ameagiza kufanyika upya kwa uchunguzi wa madai ya maji yenye sumu yanayotiririka kutoka mgodi wa Acacia North Mara kwenda kwenye vyanzo vya maji baada ya ripoti ya kwanza kujaa udanganyifu. Agizo hilo limetolewa ikiwa ni zaidi ya miaka 10 tangu wananchi wa vijiji vinavyozunguka mgodi huo kudai kuwa maji hayo yamekuwa yakisababisha madhara makubwa kwa binadamu ikiwemo vifo vya watu, mifugo na kuathiri vyanzo vya maji. Rais Magufuli aliyasema hayo jana akiwa kwenye ziara ya kikazi na kuagiza Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kufanya upya uchunguzi huo kwenye Mto Tigiti. “Maji wanayokunywa watu na wanyama kwenye mto huo kwenye ripoti ya kwanza iliyoundwa nikiwa bado Waziri waliichezea, ng’ombe walikuwa wanakufa, watu walikuwa wakioga wanaungua mikono ripoti ikachezewa,” alisema na kuongeza: “Mimi ni mkemia ninafahamu. Nataka mfanye uchunguzi vizuri na hiyo ripoti iwe wazi. watu wa Nemc waje wachunguze hay

Tundu Lissu Kudai Stahiki zake Mahakamani

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Singida Mashariki (Chadema), Tundu Lissu, amesema atalifikisha Mahakama Kuu suala la gharama za matibabu yake ili iweze kutoa tafsiri sahihi baada ya Bunge kushindwa kumlipia. Lissu aliyasema hayo kupitia andiko lake lililoanza kusambaa jana akiwa anatimiza mwaka mmoja tangu alipopigwa risasi Septemba 7, mwaka jana eneo la nyumbani kwake jijini Dodoma. Katika andiko  lake hilo ambalo pia  ameelezea tukio zima la kujeruhiwa kwake,  mwenendo wa matibabu katika kipindi chote cha mwaka mmoja na kile alichodai kiini cha kuumizwa kwake, kuhusu suala la matibabu ambalo amelifafanua kwa kina  Lissu ametoa sababu za kimazingira na kisheria  ambazo ndio msingi wa yeye kuamua kulifikisha suala hilo mahakamani. “Kwa upande wetu, njia pekee iliyobaki sasa ni kulipeleka suala hili mahakamani ili Mahakama Kuu itoe tafsiri sahihi ya jambo hili. Maandalizi ya kwenda mahakamani yanaendelea,” alisema Lissu. Akirejea mvutano kuhusu Bunge kukataa kulipia ghara

Rais Magufuli Akerwa na Ugomvi wa DC na Mkuu wa Mkoa

Image
NancyTheDreamtz Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli amekemea tabia ya wakuu wa wilaya na mikoa kugombana wakati wanapotumikia wananchi. Ameyasema hayo wakati akihutubia wananchi wa wilaya ya Tarime mkoani Mara wakati wa ziara yake ya kikazi, ambapo kuna mgogoro mkubwa kati ya DC wa wilaya Glorius Luoga na mwenyekiti wa CCM wa wilaya hiyo Daud Ngicho na mkuu wa mkoa huo Adam Malima. Rais Dkt. Magufuli ameonyesha kukerwa na misiguano ya viongozi wa mkoa wa Mara unaofanya hata miradi mbalimbali ya maendeleo kukwama kufuatia DC Luoga na RC Malima kutofautiana. “Kwanini mnagombana, wewe DC uko chini ya RC Malima, umheshimu na si kugombana kila wakati mpaka shughuli za maendeleo zinakwama,”amesema JPM Hivi karibuni  Rais pia alikemea mgogoro kati ya mkuu wa wilaya ya Chemba na Naibu waziri wa Fedha, Dkt. Ashatu Kijaji na viongozi wa wilaya hiyo wakati wa kuzindua barabara inayounganisha Afrika.

Kusini Kivipi tutakwepa Hili Wanafunzi wa chidya wachoma moto Shule

Image
NancyTheDreamtz Kama kunaumasikini unaoutesa Mkoa wa Mtwara ni Elimu kwani kirekodi za matokeo huwa sio mzuri kiujumla Leo unakuta Shule ambayo inasifa kubwa Mkoani Mtwara Wilaya ya Masasi Chidya wamediriki kuleta Mgomo kwakuchoma ofisi ya taaluma moto kama mtakavyojionea hapo chini ni aibu sana kusini wapi tunaelekea katika kuhakikisha tunaondoa aibu ya elimu duni. Wanafunzi wa shule ya sekondari Chidya iliyoko Halmashauri ya Wilaya ya Masasi Mkoani Mtwara wamefanya fujo na kusababisha uharibifu wa mali za shule na walimu  wakidai walimu wanawabana sana kwenye masomo wakati wenyewe wanataka uhuru wa kutembea sio kuwa bize na masomo kila wakati. Katika vulugu hizo wanafunzi walichoma pikipiki mbili, kuharibu vitu vyote ikiwemo tv, vitanda na vyombo vingine kwenye nyumba ya mwalimu wa taaluma pamoja na kuiba kuku 20 za mwalimu. Kutokana na Vulugu hizo, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Mhe. Gelasius Byakanwa aliyefika shuleni hapo kujionea hali halisi, alieleza kuwa sababu iliyowafany