Posts

Showing posts from August 29, 2018

Ommy Dimpoz Kafunguka Kila Kitu Kuhusu Ugonjwa Wake....Anasema Alilishwa Sumu Bila Kujua

Image
NancyTheDreamtz Vipimo  vya afya alivyofanyiwa msanii wa Bongofleva, Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz ambaye yupo nchini Afrika Kusini kwa matibabu, vimeonyesha aliwekewa sumu kwenye chakula. Ommy Dimpoz alianza kuugua mapema Mei mwaka huu na kwenda kutibiwa mjini Mombasa kabla ya kupelekwa Afrika Kusini ambako aligundulika kuwa na tatizo katika njia ya chakula ambako alifanyiwa upasuaji. Akizungumza na Kituo cha Redio cha Clouds, Dimpoz, alisema vipimo vya madaktari vimeonyesha tatizo lake linatokana na kuwekewa sumu kwenye chakula ama kinywaji. “Awali nilifanyiwa vipimo katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam na kugundulika nina kansa, lakini baada ya vipimo vikubwa huku Afrika Kusini, imeonekana nimekula sumu,”  alisema Ommy Dimpoz. Alisema anashukuru kuona hali yake imeanza kuimarika baada ya awali kushindwa kuzungumza kabisa na anaamini sala za Watanzania wenzake na watu ambao wamekuwa karibu naye zitamsaidia na kuweza kurejea kwenye hali yake.

Kauli ya Serikali kuhusu mwanafunzi aliyefariki kwa kipigo cha Mwalimu

Image
NancyTheDreamtz Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako amezungumzia tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Kibeta, mkoani Kagera Siperius Eradius akitaka vyombo vya usalama kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mwalimu anayetuhumiwa. Akizungumza leo Agosti 29 wakati wa Kongamano la Kimataifa la Hisabati linalofanyika Chuo Kikuu cha Aga Khan, Profesa Ndalichako amedai kusikitishwa na tukio hilo na kwamba Serikali haitamfumbia macho yeyote atakayebainika kuhatarisha usalama wa wanafunzi shuleni, wakiwamo walimu wao. Amesema mwalimu aliyesababisha mauaji hayo hakutumwa na mtu isipokuwa utashi wake. Profesa amewaomba wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya usalama vinapofanya kazi yake na kwamba tukio hilo lisitoe tafsiri kuwa shule  siyo mahali salama kwa watoto.     Shule ni sehemu ambayo ni salama kwa hiyo asitokee mtu akafanya vitendo ambavyo hata wazazi wajiulize harugusu mtoto kwenda shule au asiende lakini serikali itachukua hatua kwa mtu

Benki Ya Standard Charted Kuimwagia Tanzania Sh. Trilioni 3.3 Kujenga Reli Ya Kisasa-SGR

Image
NancyTheDreamtz Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam BENKI ya Standard Chartered Group imekubali kuipatia Tanzania mkopo nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.46 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 3.3 kwa ajili ya kujenga kipande cha Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) kuanzia Morogoro hadi Makutupora, mkoani Dodoma. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw. Bill Winters, Jijini Dar es Salaam. Dkt. Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa kukubali kugharamia ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa ambayo lengo lake ni kuimarisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo kwenda bara na nchi jirani za Maziwa Makuu na zile ambazo hazipakani na Bahari. "Tunajenga Reli hiyo ya Kisasa kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Makutupora ambazo ni awamu mbili lakini pia tutajenga reli hiyo kuelekea Isaka mpaka Mwanza na baadaye Rusumo ambapo wenzetu wa nchi ya Rwanda, tutasaidiana,

Tundu Lissu Kurejea Nchini Mwakani.....Kaka Yake Asema Risasi Iliyoko Ndani ya Uti wa Mgongo haitaondolewa

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine na ataendelea kubaki na risasi moja kwenye uti wa mgongo. Hayo yameelezwa leo Agosti 29 na kaka yake Lissu, Wakili Alute Lissu, alipozungumza na wanahabari. Amesema Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine baada ya kufanyiwa upasuaji zaidi ya mara nne akiwa Ubelgiji ingawa kuna risasi moja ambayo bado imebaki nyuma ya uti wa mgongo. “Wakijaribu kuitoa huenda ikaathiri uti wa mgogo na hivyo kupata tatizo la kupooza,"amesema. Lissu alihamishiwa hospitali ya Leuven iliyopo Ulelgiji akitokea hospitali ya Nairobi, baada ya kushambuliwa kwa risasi kadhaa na watu wasiojulikana Septemba 7 mwaka jana. Alute ambaye amerejea nchini, wiki hii akitokea Ubelgiji kumjulia hali Lissu, amesema huenda mwanasiasa huyo akarejea nchini mwakani, hasa kutokana na mfupa wa mguu wa kulia kuwa bado haujaunga vizuri. "Hali ya Lissu inaendelea vizuri, lakini napenda kukanusha taarifa kuwa kuna kamati ya mapokezi yake k

Chadema kumshtaki Waitara Kamati ya Maadili

Image
NancyTheDreamtz Chama cha Demokrasia Maendeleo (Chadema) kimempeleka kwenye kamati ya maadili mgombea ubunge wa jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CCM, Mwita Waitara kwa kile walichodai kufanya uchochezi. Akizungumza leo Agosti 29, mkurugenzi wa oparesheni na mafunzo wa Chadema, Dingo Kigaila kuwa amesema sababu ya kumpeleka kwenye kamati hiyo ni kutokana na madai ya kuhamasisha vurugu kwa kupitia mtandao wa kijamii. Amesema kwa kutumia simu yake ya kiganjani Agosti 26 mwaka huu aliandika kwamba watu wa kabila lake yaani Wakurya hususani ukoo wa Wairegi wanoe mapanga yao na kumwaga damu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi jimbo la Ukonga. Amesema Waitara alitumia lugha ya Kiswahili na Kikurya kuandika ujumbe huo, hivyo wameitaka kamati ya maadili, kumuita na kumuhoji mgombea huyo. Julai 28, 2018 Mwita Mwikwabe Waitara, alitangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge na kujivua nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA na kuhamia CCM.

Waziri Mkuu: Flyover Ya Tazara Imekamilika Kwa Asilimia 98

Image
NancyTheDreamtz WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesemaujenzi wa barabara ya juu katika eneo la Tazara umekamilika kwa asilimia 98 na itafunguliwa Oktoba mwaka huu na Rais Dkt. John Magufuli. Mradi wa barabara ya juu (Mfugale flyover) chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani, unalengo la kupunguza msongamano wa magari katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere.   Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 29 ,2018) baada ya kukagua ujenzi wa mradi huowa barabara ya juu katika eneo la Tazara jijini Dar Es Salaam. Waziri Mkuu amesema ameridhishwa kazi ya umaliziaji wa mradi huo inayoendelea kwenye hilo. “Mradi utapunguza muda wa usafiri katika barabara ya Nyerere hususani  kwa wananchi wanaotoka katikati ya jiji kwenda uwanja wa ndege na wanaotoka Buguruni, Temeke.” Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi Mkoa wa Dar Es Salaam watafute eneo kwa ajili ya  wafanyabiashara ndogondogo ili waweze kuondoka kandokando ya barabara hizo za juu zinazojengwa.

Halima Mdee amuunga mkono Waziri Mpango Sakata la Makonda....."Laana ya KuKu haiwezi mpata Mwewe"

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Halima Mdee ameunga mkono agizo la Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango la kupiga mnada makontena 20 ya mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda. Kupitia mtandao wake wa Twitter ameunga mkono agizo hilo huku akiwataka wananchi kujitokeza kununua samani hizo kama ambavyo Waziri Dkt.Mpango aliwataka watu wenye uwezo wa kununua wajitokeze bila kuogopa chochote. “Wenye pesa zenu mnada ukipigwa jongeeni kwa wingi, laana ya kuku haiwezi mpata mwewe,” ameandika Mdee kwenye ukurasa wake wa Twitter Aidha, Dkt. Philip Mpango, Agosti 27, 2018 aliagiza makontena 20 ya samani yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yapigwe mnada ikiwa ni sehemu ya kusimamia sheria na kanuni za kodi zilizopo nchini. Hata hivyo, tangazo la TRA lililotolewa na Kaimu Kamishna wa Forodha na Ushuru, Ben Asubisye lilikuwa na orodha ya makontena zaidi ya 800, huku jina l