Posts

Showing posts from August 6, 2020

Ifahamu Kemikali Iliyoisambaratisha Beirut

Image
TAKRIBANI tani 3,000 za kemikali ya ammonium nitrate zilizohifadhiwa miaka sita iliyopita katika ghala zimeelezewa kusababisha mlipuko huo uliotokea katika jiji la  Beirut ambayo ni bandari na mji kuu wa  Lebanon siku ya Jumanne. Lakini ammonium nitrate ni nini na kwa nini inaweza kuwa kemikali hatari? Ammonium nitrate (NH4NO3) ni kemikali iliyo na umbo la madonge meupe ambayo hutengenezwa viwandani. Matumizi yake huwa ni chanzo cha naitrojeni kwa ajili ya mbolea, lakini pia inatumika kwa ajili ya kutengeneza vilipuzi kwa ajili ya migodi. Kemikali hii hutengenezwa duniani kote na ni rahisi kuinunua. Lakini utunzaji wake unaweza kuwa tatizo, na kemikali hii imekuwa chanzo cha ajali kadhaa za viwandani miaka ya nyuma. Ammonium nitrate ni hatari kwa kiasi gani? Yenyewe ilivyo, ni salama, anasema profesa wa kemia, Andrea Sella, kutoka shule ya sayansi ya Chuo Kikuu cha London. Hata hivyo, ukiwa na kiasi kikubwa cha kemikali hiyo kwa muda mrefu, huanza kuoza. ”Tatizo ni kwamba kadiri muda u

Mtu Wangu Jua Ishara 11 za Mwanamke Anayekupenda, Lakini Anashindwa Kukueleza.

Image
Kwa muda mrefu kumekuwa na wimbi la imani potofu kwa wanawake na wanaume kwamba mwanamke hawezi kumwambia mwanaume ukweli kama anampenda, wengi wao husubiri kwanza mpaka mwanaume aanze kuweka wazi hisia zake, lakini ni ukweli usiopingika kwamba wanawake nao pia hupenda na wengi wao wanakuwa hawapo tayari kuwa wawazi na mara nyingi wao wakianza kupenda huwa wanapenda kweli kufikia hata hatua ya kuhisi kutokuwa sawa katika mambo yao wanayoyafanya. Nimekuorodhoshea baadhi ya ishara za mwanamke anaekupenda ila anaogopa kukuambia kwa kuhofia namna atakavyoonekana mbele ya macho ya jamii au kuwa na hofu na jambo analotaka kukueleza kwa kufikiria kuwa itakuwaje endapo hautakuwa tayari kuwa nae na hapo ndio hukumbwa na hofu ya kuelezea hisia zake. 1. Kukupa majaribu madogomadogo ili kujua thamani yake kwako. Hufanya mambo ambayo yatamfanya kuona kama unampenda na kumthamini au lah, mfano wa mambo hayo ni kama kujifanya anaumwa na kauangalia muitikio wako kwake, ili kutambua ni kiasi gani unamj

Atuhumiwa kwa Kuua Ndugu Zake Waliomtuhumu Kuiba Kuku na Redio

Image
Mwanaume wa miaka 33, mkazi wa Lira, Uganda anashikiliwa na polisi baada ya kuwaua ndngu zake waliomtuhumu kuiba kuku na redio. Mtu huyo alimkataka mjomba wake, Jackson Olong na alimshambulia mke wa mjomba wake na kumkata koromeo. Mtu huyo aliwalaumu nduguze kwa kuchafua jina lake kuwa amewaibia vitu vyao. Mwenyekiti wa Agweng, Marino Ogwang alisema mtu huyo alituhumiwa na nduguze kuuza vitu vyao ili akanunue pombe. Kamanda wa polisi Paul Nkore amesema mtuhumiwa atashtakiwa kwa kesi ya mauaji. ==== A 33-year-old man has been detained for allegedly killing his two relatives who had accused him of stealing their radio set and a chicken in Lira District. It is reported that the attacker on Tuesday hacked his uncle, Jackson Olong. After cutting Olong into pieces, he attacked Olong’s wife and slit her throat. He accused the two of tarnishing his name by claiming that he had stolen their property. The gruesome murder took place at Ayitunga Village, Te-oburu Parish in Agweng Sub-county at abo

Afrika Kusini ndio taifa lililoathirika kwa kiasi kikubwa na maambukizi ya covid-19

Image
Idadi ya watu ambao wamekwishaambukiwa virusi vya corona ulimwenguni, idadi yake imefikia watu  milioni  18,7 huku  idadi ya watu waliofariki ikiripotiwa kufikia watu   704 632.  Idadi ya jumla ya watu ambao wamekwishapona vilevile baada ya kupatiwa matibabu  inaendelea kuongezeka, idadi hiyo imefahamishwa kufikia watu   zaidi ya   milioni 11,9 kote ulimwenguni.  Ndani ya masaa 24  nchini India , watu  904 wamefariki kwa maambukizi ya virusi vya corona.  Vifo hivyo  ambavyo vimetokea ndani ya masaa 24 vimepelekea idadi ya watu ambao wamekwishafariki kutomana na maambukizi ya virusi hivyo kufikia watu  40 772.  Idadi ya watu ambao wamekwishaambukiwa covid-19 nchini India inaripotiwa kufikia watu   milioni  1,9.  Katika jimbo la Gujarat,  ajali ya moto iliotokea katika hospitali moja imepelekea vifo vya watu  wanane.  Nchini Urusi,  watu  14 606 wamekwishafariki huku watu  871 894 wakiwa na maambukizi.  Nchini Iran ni watu  17 802 ndio ambao wamekwishafariki kwa virusi hivyo huku idadi y

Shiboub Apewa Ofa Nono Yanga, Akubali Kusaini

Image
WADHAMINI wa Yanga, Kampuni ya GSM, imempa ofa kiungo mchezeshaji fundi wa Simba raia wa Sudan, Sharraf Eldin Shiboub kwa ajili ya kujiunga na timu hiyo kwenye msimu ujao. Kiungo huyo hivi sasa ni mchezaji huru anayeruhusiwa kujiunga na klabu nyingine itakayomuhitaji katika msimu ujao kutokana na mkataba wake wa mwaka mmoja kumalizika ndani ya Simba huku dalili za kuongezewa zikiyeyuka. Nyota huyo alitua Simba mwanzoni mwa msimu uliopita akitokea Al Hilal ya Sudan ambapo inaelezwa alisaini kwa dau la Sh Mil 100. Kwa mujibu wa taarifa ambazo imezipata Spoti Xtra, juzi Yanga ilimpelekea Shiboub ofa hiyo, , lakini wakashindwana katika dau la usajili ambalo amewatajia mabosi hao ambalo ni siri. Mtoa taarifa huyo alisema kuwa kiungo huyo mwenyewe amekubali kujiunga na Yanga kama watakuwa tayari kutoa dau zuri la usajili ambalo yeye amelitaka na mshahara mnono.Aliongeza kuwa kiungo huyo juzi alirejea nyumbani kwao Sudan huku akiwaacha mabosi wa Yanga wajadiliane na kama wakifikia makubaliano

Papa Francis awateuwa wanawake sita kusimamia fedha za Vatican

Image
Kiongozi wa Kanisa Katoliki Duniani Papa Francis amewateuwa wanawake sita, akiwemo mweka hazina wa zamani wa Mwanamfalme Charles wa Uingereza, kuhudumu katika baraza linalosimamia fedha za Vatican.  Uteuzi huo kwenye mojawapo ya ofisi muhimu kabisa za Makao makuu ya kanisa hilo unadhihirisha jitihada ya karibuni ya papa Francis kutimiza ahadi za kuimarisha usawa wa kijinsia alizotoa miaka kadhaa iliyopita lakini wanawake wakasema zilichukua muda mrefu sana kutimizwa.  Francis tayari aliwateuwa wanawake kuwa naibu waziri wa mambo ya kigeni, mkurugenzi mkuu wa Majumba ya Makumbusho ya Vatican, na naibu mkuu wa Ofisi ya Habari ya Vatican, pamoja na wanawake wanne kama wanachama wa Baraza la Maaskofu, ambalo huandaa mikutano mikuu. NancyTheDreamtz

Wema Sepetu na Aunty Ezekiel wapatanishwa

Image
Meneja na mfanyabiashara Petitman Wakuache amesema amewapatanisha Wema Sepetu na rafiki yake wa muda mrefu Aunty Ezekiel baada ya kuwepo na taarifa kwamba wawili hao  wanatofauti na imepita muda mrefu bila kuonekana wakiwa pamoja.  Akitumia ukurasa wake wa Instagram kufikisha ujumbe huo Petitman Wakuache amepost video fupi akiwa na Wema Sepetu na Aunty Ezekiel huku akiwapa onyo kwamba ole wao wagombane tena.  "Kama kawaida nipo na ndugu zangu wa ukweli kabisa, kwani mlipotelea wapi nishawapatanisha sasa ole wenu mgombane tena, kwa nini mliniacha mwenyewe sasa kwenye group mkaleft" amesema Petitman Wakuache NancyTheDreamtz

Majanga Yaendelea Kumwandama Mtoto Aliyeokolewa Chooni

Image
MISUKOSUKO imeendelea kumwandama mtoto (jina linafichwa) ambaye aliopolewa kwenye shimo la choo cha Shule ya msingi Murganza iliyoko wilayani Ngara mkoani Kagera baada ya kutupwa na mama yake mzazi ambapo sasa wasamaria wema waliokuwa wamejitokeza wakihitaji kumlea, wameingia mitini.   Afisa Ustawi wa Jamii Wilaya ya Ngara, Musa Baragondoza amesema wasamaria wema hao wameingia mitini baada ya kugundua kuwa mtoto huyo ana tatizo kwenye ubongo ambalo limesababisha ashindwe kukaa, kutembea wala kusimama.   “Sababu ya wasamaria wema hao kukimbia ni baada ya ripoti ya madaktari kuthibitisha kuwa mtoto ana matatizo kwenye ubongo ambayo yamesababisha ulemavu huo kwa kuwa waliona ni mzigo ambao hauvumiliki.   “Mtoto huyo kwa sasa yuko kwa Belesi Mitengo, ambaye alikuwa anamuuguza wakati akiwa hospitali ya Nyamihaga akitibiwa mguu uliovunjika baada ya kutupwa kwenye tundu la choo,” alisema afisa huyo.   Aliongeza kuwa, licha ya Belesi kuonyesha moyo wa kumlea mtoto huyo, kwa sasa mlezi huyo ame