Posts

Showing posts from June 18, 2021

Video: Meja Kunta Afanya Balaa Nandy Festival Mwanza

Image
MWANAMUZIKI anayefanya poa kwenye muziki wa Singeli Bongo, Khalid Sadick ‘Meja Kunta’  amefanya balaa usiku wa kuamkia leo Juni 18, 2021 jijini Mwanza kwa kupiga shoo ya nguvu kwenye Tamasha la Nandy Festival. NancyTheDreamtz

Nandy Festival 2021; Ben Pol Apiga Shoo ya Kibabe Mwanza – Video

Image
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini  Mwanza  kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine.  NancyTheDreamtz

Breaking: Papa Msofe Afutiwa Mashtaka, Aachiwa Huru

Image
Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu leo Juni 18, 2021 imemfutia mashtaka na kumwachia huru mfanyabiashara  Marijan Msofe (53) maarufu Papa Msofe na wenzake wanne.   Hatua hiyo inatokana na Mkurugenzi wa Mashtaka nchini (DPP) kuwasilisha hati mahakamani hapo akieleza kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo dhidi ya washtakiwa hao. Msofe na wenzake walikuwa wanakabiliwa wa mashtaka matano likiwemo la kujipatia Sh943 milioni kwa njia ya udanganyifu.   Mbali na Papa Msofe, washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya uhujumu uchumi namba 124/2019 ni Wenceslaus Mtu(49), Mwesigwa Mhingo (36), Josephine Haule (38) na Fadhil Mganga (61).   Uamuzi wa kuwafutia kesi hiyo na kuwaachia huru washtakiwa hao umetolewa Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo, Huruma Shaidi wakati kesi hiyo ilipoitwa kwa ajili ya kutajwa. Awali, wakili wa Serikali mwandamizi, Wankyo Simon amedai kuwa DPP ameieleza mahakama hiyo kuwa hana nia ya kuendelea na shauri hilo. Baada ya upande mashtaka kueleza hiyo, Shaidi alikubaliana na