Meli iliyopata ajali miaka 400 yapatikana, inadaiwa ilikuwa njiani kutoka India

NancyTheDreamtz
Watafiti wa mambo ya kale wamegundua meli iliyopata ajali miaka 400 iliyopita karibu na pwani ya Ureno, katika tukio ambalo wataalam wameliita “ugunduzi muhimu”.
Kwa mujibu wa mtandao wa REUTERS, baadhi ya viungo, vyombo vya kauri na mizinga ikiwa na nembo ya Ureno vimetapakaa katika eneo la karibu na Cascais ambapo si mbali sana kutoka Mji Mkuu Lisbon.
Image result for Shipwreck discover 400 years past in Cascais
Wagunduzi hao waamini kwamba meli ilikuwa njiani kutoka India wakati ilipozama kati ya mwaka 1575 na 1625. Nyakati hizo zinakadiriwa kuwa ndiyo kilele cha biashara ya viungo kati ya Ureno na nchi za Asia.
Image result for Shipwreck discover 400 years past in Cascais
Inadhaniwa kuwa huu ni ugunduzi mkubwa kabisa ambao umechukua takribani miaka 10 kwa mujibu wa mkurugenzi wa zoezi hilo, Jorge Freire ambapo akisisitiza ni jambo muhimu zaidi kwa Ureno.

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais