Afya ya Haji Manara yatetereka, mwenyewe adai amelishwa sumu na sio presha ya matokeo ya Simba
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Baada ya taarifa kusambaa mitandaoni kuwa Msemaji wa klabu ya Simba, Haji Manara ameshikwa na presha iliyopelekea kulazwa mkoani Shinyanga, hatimaye mwenyewe aweka wazi kinachomsumbua.
Haji Manara
Manara amesema kuwa alikula chakula chenye sumu, na ndio sababu iliyompelekea kulazwa na sio presha ya matokeo mabaya ya klabu yake kama inavyoandikwa mitandaoni.
“Siumwi pressure wala moyo kama inavyoandikwa mitandaoni..nahic nimepata food poisoning na niwashukuru Madaktari walionihudumia awali Shinyanga na Mwanza ..now nisharejea Dar teyari kwa vipimo zaidi…Insha’Allah kila kitu kitazidi kuwa salama,“ameeleza Haji Manara kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Klabu ya Simba imekuwa na matokeo mabovu kwa msimu huu ambapo wiki iliyopita imepokea kichapo cha goli 1 dhidi ya Mbao FC ya Mwanza.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
NancyTheDreamtz Mshambuliaji hatari ndani ya klabu ya KRC Genk ya Ubelgiji raia wa Tanzania, Mbwana Samatta amesema kuwa kabla ya maisha yake ya soka alitamani kuwa mwanajeshi. Samatta ambaye ni nahodha wa timu ya taifa ameyasema hayo kupitia mtandao wake wa kijamii wa Instagram huku akiwaacha washabiki wake na swali. Muda mwingine mungu akupi unaloliomba ila anakupa linalo kustahili… Kabla ya soka,nilikuwa natamani kuwa mwanajeshi,je kwa sura hii unadhan ningependeza kuwa soja? Kwa sasa nyota huyo yupo njiani akielekea nchini Uganda akiwa na wachezaji wenzake wa Taifa Stars kwaajili ya kuikabili timu ya Uganda ‘The Cranes’ ikiwa ni mchezo wa kuwania kutafuta tiketi ya kufuzu Afcon utakao pigwa siku ya Jumamosi ya Septemba 8 mwaka huu 2018.
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini Mwanza kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine. NancyTheDreamtz
Comments