Ruge Mutahaba na Nikki wa Pili watoa neno kwa muandaaji wa shindano la Miss Tanzania 2018
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds FM, Ruge Mutahaba, na Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nikki wa Pili wamemmwagia sifa za kutosha Muandaaji wa shindano la Miss Tanzania 2018, Basilla Mwanukuzi.
Basilla Mwanukuzi.
Ruge kwenye barua yake ya pongezi amesema Bi. Basilla amerudisha heshima ya shindano hilo ambalo lilikuwa linaonekana kupoteza sifa yake kwa miaka ya hivi karibuni.
“Basila Hongera sana mdogo wangu, kikubwa ulichofanikisha kufanya ni kuanza kurudisha imani kwa waliopoteza imani na hiyo brand. Sio siri, itakuchukua mwaka mmoja, miwili hata mitatu kufika kwenye level ya kupata the same integrity na value iliyokuwa imepotea. Kurudisha imani za wadhamini, wahisani na mwisho sisi wananchi tutarudi labda kwa ukubwa kuliko ilivyokuwa. Umefanya makosa mengi sana kwenye hii hatua ila ni sehemu ya ukuaji because najua hakuna mtoto anajaribu kutembea bila kuangukaanguka. Kama Clouds Media Group tupo na wewe na mawakala wote kwa pamoja mmewezesha jambo hili kurudi kupata heshima yake. Kubwa kuliko yote ili kujenga heshima inayodumu ungalizi wa washindi uendelee kwa muda mrefu kupata role models wengi kwa taifa letu. Mungu awabariki sana.“ameeleza Ruge.
Kwa upande mwingine, Nikki wa Pili naye amemmwagia sifa muandaaji huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika “nimpongeze mwandaaji wa miss tanzania @basillamwanukuzi kwanza kwakuwa ni mwanamke(yes) pili kuona fursa katika passion yake ya urembo, tatu kuirudisha misstanzania iliyo kuwa imepotea, nne kwa kuanza na kidogo lengo si zawadi lengo kujenga brand ya misstanzania na warembo pia……..Nachosema songa mbele ifanye kuwa taasisi itengeneza pesa na ajira mwaka mzima…….warembo wa 5 waliopata ajira nao wata tengeneza ajira kwa wapiga picha, wabunifu, na watu wa branding, media zimepata content, biashara zimetangazwa, watu wamepata burudani na fursa kibao umezifungua ni kwa vijana kufikiria kuziendeleza kutokea jana kwenda mbele..#wenye wingi wa lawama wana uchache wa kuona fursa.“.
Jana usiku kulikuwa na shindano la Miss Tanzania 2018 ambapo mrembo, Queen Elizabeth aliibuka kidedea kwa kuwamwaga wenzake 19.
Mimi ni mwanamke.Naomba msaada wa mawazo maana sijui nina nini mimi... Umri unanitupa mkono maana nakaribia miaka 35 lakini sijampata aliyewahi kunitangazia ndoa.Cha ajabu kila anayelala na mimi siku ya pili harudii tena na hata nikimpigia simu hapokei Hapo ndo linapoanzia tatizo na kunifanya nijisikie vibaya...Saivi hata mtaani nachagua kwa kupita... Kuna mwanaume mmoja huyo ndo aliwahi kunichana live kuwa nina maji mengi ila sielewi alimaanisha nini Jamani naomba msaada nifanyaje mie nipendwe kama wengine nyandichethedreamtz
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo amesema atawachukulia hatua za kisheria wazazi au walezi wasiowapeleka watoto shule. Alisema hayo juzi alipofanya ziara katika shule za msingi Chazige A na B alikokutana na wananchi na kusikiliza kero zao. Jokate alisema mzazi au mlezi asiyempeleka shule mtoto hasa wa kike hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo kupelekwa mahakamani. Alisema wataendelea na kampeni ya “Tokomeza Ziro” yenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu na miundombinu ya shule, madarasa na vyoo. Naye ofisa elimu msingi wilayani Kisarawe, Shomari Bane alisema: “Kampeni imetusaidia, wanafunzi kuanzia mwaka jana ufaulu darasa la saba uliongezeka na walifanya vizuri. Pia, Jokate alimuagiza mganga mkuu na madaktari wilayani Kisarawe kutoa dawa zilizopo hospitalini kwa wagonjwa na kama hazipo, watoe mbadala ili wananchi wasipate usumbufu.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Comments