Ruge Mutahaba na Nikki wa Pili watoa neno kwa muandaaji wa shindano la Miss Tanzania 2018
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Mkurugenzi wa vipindi na uzalishaji wa Clouds FM, Ruge Mutahaba, na Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Nikki wa Pili wamemmwagia sifa za kutosha Muandaaji wa shindano la Miss Tanzania 2018, Basilla Mwanukuzi.
Basilla Mwanukuzi.
Ruge kwenye barua yake ya pongezi amesema Bi. Basilla amerudisha heshima ya shindano hilo ambalo lilikuwa linaonekana kupoteza sifa yake kwa miaka ya hivi karibuni.
“Basila Hongera sana mdogo wangu, kikubwa ulichofanikisha kufanya ni kuanza kurudisha imani kwa waliopoteza imani na hiyo brand. Sio siri, itakuchukua mwaka mmoja, miwili hata mitatu kufika kwenye level ya kupata the same integrity na value iliyokuwa imepotea. Kurudisha imani za wadhamini, wahisani na mwisho sisi wananchi tutarudi labda kwa ukubwa kuliko ilivyokuwa. Umefanya makosa mengi sana kwenye hii hatua ila ni sehemu ya ukuaji because najua hakuna mtoto anajaribu kutembea bila kuangukaanguka. Kama Clouds Media Group tupo na wewe na mawakala wote kwa pamoja mmewezesha jambo hili kurudi kupata heshima yake. Kubwa kuliko yote ili kujenga heshima inayodumu ungalizi wa washindi uendelee kwa muda mrefu kupata role models wengi kwa taifa letu. Mungu awabariki sana.“ameeleza Ruge.
Kwa upande mwingine, Nikki wa Pili naye amemmwagia sifa muandaaji huyo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika “nimpongeze mwandaaji wa miss tanzania @basillamwanukuzi kwanza kwakuwa ni mwanamke(yes) pili kuona fursa katika passion yake ya urembo, tatu kuirudisha misstanzania iliyo kuwa imepotea, nne kwa kuanza na kidogo lengo si zawadi lengo kujenga brand ya misstanzania na warembo pia……..Nachosema songa mbele ifanye kuwa taasisi itengeneza pesa na ajira mwaka mzima…….warembo wa 5 waliopata ajira nao wata tengeneza ajira kwa wapiga picha, wabunifu, na watu wa branding, media zimepata content, biashara zimetangazwa, watu wamepata burudani na fursa kibao umezifungua ni kwa vijana kufikiria kuziendeleza kutokea jana kwenda mbele..#wenye wingi wa lawama wana uchache wa kuona fursa.“.
Jana usiku kulikuwa na shindano la Miss Tanzania 2018 ambapo mrembo, Queen Elizabeth aliibuka kidedea kwa kuwamwaga wenzake 19.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Leo August 13, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli amefanya teuzi mbalimbali siku ya leo na kufanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Msafiri Simeoni wa Kwimba amepelekwa Chato, Senyi Simon amepelekwa Kwimba Wafuatao ni baadhi ya walioteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Majiji Halmashauri ya Misenyi Mkurugenzi ni Innocent Mbandwa Jiji la Mbeya Mkurugenzi ni James Kasusura Halmashauri ya Malinyi Mkurugenzi ni Mussa Elias Mnyeti Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ni Maulid Madeni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke ni Lusibilo Mwakabili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ubungo ni Beatrice Kwai Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kigamboni ni Mwilabu Nyabusu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa mkoani Dodoma ni Mustapha Yusuph Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi ni Tatu Seleman Kikwete Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko ni Masumbuko Stephano Mkurugenzi wa Halmashauri ya Katavi ni Ramadhan ...
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments