Mobetto aingia Red Carpet na baunsa kwenye shindano la Miss Tanzania

NancyTheDreamtz

Mrembo Hamisa Mobetto ambaye alikuwa host wa Miss Tanzania 2018 aliingia Red Carpet akiwa na mabaunsa ili kujikinga na waandishi wa habari ambao walimkimbilia kwa wingi baada ya kuonekana anaingia ukumbini hapo. Hata hivyo hakuna mwandishi ambaye alipata fursa ya kuzungumza naye zaidi ya Clouds Media ambao walikuwa wadhamini wa show hiyo.

Mobetto alikimbia kuongea na waandishi wa habari kwa kuhofia kuulizwa maswali ambayo alihisi yatamtoa kwenye mood kwani yeye ndio host wa sherehe nzima ya kumtafuta Miss Tanzania. 

Siku kadhaa nyuma mrembo huyo alikumbwa na tetesi za kutaka kumloga baba wa mtoto wake Diamond Platnumz kwa madai ya kutaka gari pamoja na nyumba.

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais