Muigizaji Elizabeth ‘Lulu’ Michael amaliza kimya chake cha mwaka mmoja mitandaoni, amuandikia ujumbe mzito Majizzo
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Baada ya kimya cha muda mrefu cha takribani siku 324 mitandaoni, hatimaye Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael almaarufu Lulu amerudi rasmi kwa kumuandikia ujumbe mahsusi mpenzi wake Majizzo ambaye pia ni Mkurugenzi wa EFM na TV-E .
Majizzo na Lulu
Lulu ameandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika, “Lover,Best Friend,Business Partner,Ride Or Die And A Shoulder To Always Cry On. Asante Kwa Kunionyesha Maana Halisi Ya Upendo Wa Agape(KIUNGU). Baraka Zikufuate Siku Zote Za Maisha Yako.” .
Lulu hajawahi kuposti kitu chochote kile mtandaoni tangu mwaka jana ahukumiwe jela na baadae kutolewa jela kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ujumbe huo pia ameutoa leo ikiwa ni siku ya kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa Majizzo. Mashabiki wake wameoneshwa kufurahishwa zaidi na kitendo hicho kwa kuishambulia posti hiyo kwa kumkaribisha mitandaoni.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini Mwanza kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine. NancyTheDreamtz
NancyTheDreamtz Na Mwandishi Wetu, MOHA, Songea. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mkoa wa Ruvuma, Seif Mgonja kwa kosa la kutogawa kwa wananchi Namba za Utambulisho wa Taifa (NIN), 14,493 tangu Disemba 31, 2019, licha ya kuzalishwa na Makao Makuu na kuletewa ofisini kwake Mjini Songea. Pia Waziri Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa NIDA Wilaya ya Namtumbo, Mkoani humo, Thobias Nangalaba kwa uzembe wa kutofika katika kikao chake cha viongozi wa Mkoa na Wilaya, licha ya kupewa taarifa ya kuhudhuria kikao hicho. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Soko Kuu la Manispaa ya Songea Mkoani humo, leo, Waziri Lugola amesema, amewatengua vyeo maafisa wawili hao kwa kucheza na kazi za Serikali, kwa kutojali majukumu yao. “Ndugu wananchi wa Songea, maafisa hawa wamekuwa wakienda kinyume na maagizo ya Serikali la kuwataka waweze kuwakamilishia wananc...
Comments