Muigizaji Elizabeth ‘Lulu’ Michael amaliza kimya chake cha mwaka mmoja mitandaoni, amuandikia ujumbe mzito Majizzo
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Baada ya kimya cha muda mrefu cha takribani siku 324 mitandaoni, hatimaye Muigizaji wa filamu nchini Tanzania, Elizabeth Michael almaarufu Lulu amerudi rasmi kwa kumuandikia ujumbe mahsusi mpenzi wake Majizzo ambaye pia ni Mkurugenzi wa EFM na TV-E .
Majizzo na Lulu
Lulu ameandika ujumbe huo kupitia ukurasa wake wa Instagram kwa kuandika, “Lover,Best Friend,Business Partner,Ride Or Die And A Shoulder To Always Cry On. Asante Kwa Kunionyesha Maana Halisi Ya Upendo Wa Agape(KIUNGU). Baraka Zikufuate Siku Zote Za Maisha Yako.” .
Lulu hajawahi kuposti kitu chochote kile mtandaoni tangu mwaka jana ahukumiwe jela na baadae kutolewa jela kwa msamaha wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Ujumbe huo pia ameutoa leo ikiwa ni siku ya kumbu kumbu ya kuzaliwa kwa Majizzo. Mashabiki wake wameoneshwa kufurahishwa zaidi na kitendo hicho kwa kuishambulia posti hiyo kwa kumkaribisha mitandaoni.
Mimi ni mwanamke.Naomba msaada wa mawazo maana sijui nina nini mimi... Umri unanitupa mkono maana nakaribia miaka 35 lakini sijampata aliyewahi kunitangazia ndoa.Cha ajabu kila anayelala na mimi siku ya pili harudii tena na hata nikimpigia simu hapokei Hapo ndo linapoanzia tatizo na kunifanya nijisikie vibaya...Saivi hata mtaani nachagua kwa kupita... Kuna mwanaume mmoja huyo ndo aliwahi kunichana live kuwa nina maji mengi ila sielewi alimaanisha nini Jamani naomba msaada nifanyaje mie nipendwe kama wengine nyandichethedreamtz
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo amesema atawachukulia hatua za kisheria wazazi au walezi wasiowapeleka watoto shule. Alisema hayo juzi alipofanya ziara katika shule za msingi Chazige A na B alikokutana na wananchi na kusikiliza kero zao. Jokate alisema mzazi au mlezi asiyempeleka shule mtoto hasa wa kike hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo kupelekwa mahakamani. Alisema wataendelea na kampeni ya “Tokomeza Ziro” yenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu na miundombinu ya shule, madarasa na vyoo. Naye ofisa elimu msingi wilayani Kisarawe, Shomari Bane alisema: “Kampeni imetusaidia, wanafunzi kuanzia mwaka jana ufaulu darasa la saba uliongezeka na walifanya vizuri. Pia, Jokate alimuagiza mganga mkuu na madaktari wilayani Kisarawe kutoa dawa zilizopo hospitalini kwa wagonjwa na kama hazipo, watoe mbadala ili wananchi wasipate usumbufu.
NancyTheDreamtz MFUNGAJI wa mabao ya mwisho yaliyoipeleka hatua ya makundi na Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika timu ya Simba Mzambia, Clatous Chota Chama ‘Triple C’ ameongeza mkataba mwingine wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea timu hiyo. Huyo, ni mchezaji wa sita kwa Simba kuongezewa mkataba wengine ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Aishi Manula, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na Meddie Kagere. Chama alijiunga na Simba kwenye msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara akitokea Power Dynamo inayocheza ligi ya nchini huko. Taarifa ya klabu ya Simba inaeleza kuwa kiungo huyo atakuwa sehemu ya kikosi hicho hadi 2020 baada ya kuongeza mkataba huo. Simba hivi sasa ipo kwenye mikakati ya kukiboresha kikosi hicho kwa ajili ya michuano ya kimataifa Afrika na kikubwa kufika hatua ya fainali baada ya msimu uliopita kufika robo fainali. Timu hiyo hadi hivi sasa tayari imefanikiwa kuwasajili wachezaji wapya watano ambao ni Beno Kakolanya, Kennedy Juma, Gerson Fraga ...
Comments