Rais Magufuli apingana na Waziri wake wa Afya, asema Watanzania zaeni hakuna uzazi wa mpango
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amepingana na sera ya serikali yake ya uzazi wa mpango akidai kuwa sera hiyo inapunguza nguvu kazi kwa taifa.
Rais Magufuli
Rais Magufuli akiwahutubia mamia ya watu leo Septemba 9, 2018 mjini Meatu Mkoani Simiyu, ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa, amesemW watanzania waendelee kuzaa lakini wachape kazi ili kukidhi mahitaji ya watoto wao.
”Najua Waziri wa Afya Ummy Mwalimu hapa angependa kuongelea mambo ya uzazi wa mpango lakini mimi mengine huwa sikubaliani nayo sana, utapangiwaje kuzaa ?..Kwahiyo katika kushauriwa mengine tukubali na mengine tukatae tutumie msemo wa mzee Jakaya Kikwete ‘Ukiwambiwa changanya na za kwako’ kuzaa ni muhimu’”amehoji Rais Magufuli na kutolea mfano wa nchi ambazo alishawahi kuishi na hakusikia wimbo wa uzazi wa mpango.
“Mimi Ulaya nimekaa, nafahamu madhara ya kutokuzaa, nchi gani sijaenda, Japan nimekaa, Uingereza nimekaa mwaka mzima, Ujerumani nimekaa, Canada nimekaa na nikachaguliwa kuwa co-chair wa mawaziri ardhi duniani, Denmark, Norway, utanidanganya wapi, China nimefika,“amemaliza Rais Magufuli.
Mwaka huu Serikali kupitia Wizara ya Afya, inayoongozwa na Mhe. Ummy Mwalimu imetenga Tsh Bilioni 14 kwa ajili ya huduma ya uzazi wa mpango.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Leo August 13, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli amefanya teuzi mbalimbali siku ya leo na kufanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Msafiri Simeoni wa Kwimba amepelekwa Chato, Senyi Simon amepelekwa Kwimba Wafuatao ni baadhi ya walioteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Majiji Halmashauri ya Misenyi Mkurugenzi ni Innocent Mbandwa Jiji la Mbeya Mkurugenzi ni James Kasusura Halmashauri ya Malinyi Mkurugenzi ni Mussa Elias Mnyeti Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ni Maulid Madeni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke ni Lusibilo Mwakabili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ubungo ni Beatrice Kwai Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kigamboni ni Mwilabu Nyabusu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa mkoani Dodoma ni Mustapha Yusuph Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi ni Tatu Seleman Kikwete Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko ni Masumbuko Stephano Mkurugenzi wa Halmashauri ya Katavi ni Ramadhan ...
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments