Rais Magufuli apingana na Waziri wake wa Afya, asema Watanzania zaeni hakuna uzazi wa mpango
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli, amepingana na sera ya serikali yake ya uzazi wa mpango akidai kuwa sera hiyo inapunguza nguvu kazi kwa taifa.
Rais Magufuli
Rais Magufuli akiwahutubia mamia ya watu leo Septemba 9, 2018 mjini Meatu Mkoani Simiyu, ikiwa ni sehemu ya ziara yake katika mikoa ya kanda ya ziwa, amesemW watanzania waendelee kuzaa lakini wachape kazi ili kukidhi mahitaji ya watoto wao.
”Najua Waziri wa Afya Ummy Mwalimu hapa angependa kuongelea mambo ya uzazi wa mpango lakini mimi mengine huwa sikubaliani nayo sana, utapangiwaje kuzaa ?..Kwahiyo katika kushauriwa mengine tukubali na mengine tukatae tutumie msemo wa mzee Jakaya Kikwete ‘Ukiwambiwa changanya na za kwako’ kuzaa ni muhimu’”amehoji Rais Magufuli na kutolea mfano wa nchi ambazo alishawahi kuishi na hakusikia wimbo wa uzazi wa mpango.
“Mimi Ulaya nimekaa, nafahamu madhara ya kutokuzaa, nchi gani sijaenda, Japan nimekaa, Uingereza nimekaa mwaka mzima, Ujerumani nimekaa, Canada nimekaa na nikachaguliwa kuwa co-chair wa mawaziri ardhi duniani, Denmark, Norway, utanidanganya wapi, China nimefika,“amemaliza Rais Magufuli.
Mwaka huu Serikali kupitia Wizara ya Afya, inayoongozwa na Mhe. Ummy Mwalimu imetenga Tsh Bilioni 14 kwa ajili ya huduma ya uzazi wa mpango.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini Mwanza kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine. NancyTheDreamtz
NancyTheDreamtz Na Mwandishi Wetu, MOHA, Songea. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mkoa wa Ruvuma, Seif Mgonja kwa kosa la kutogawa kwa wananchi Namba za Utambulisho wa Taifa (NIN), 14,493 tangu Disemba 31, 2019, licha ya kuzalishwa na Makao Makuu na kuletewa ofisini kwake Mjini Songea. Pia Waziri Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa NIDA Wilaya ya Namtumbo, Mkoani humo, Thobias Nangalaba kwa uzembe wa kutofika katika kikao chake cha viongozi wa Mkoa na Wilaya, licha ya kupewa taarifa ya kuhudhuria kikao hicho. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Soko Kuu la Manispaa ya Songea Mkoani humo, leo, Waziri Lugola amesema, amewatengua vyeo maafisa wawili hao kwa kucheza na kazi za Serikali, kwa kutojali majukumu yao. “Ndugu wananchi wa Songea, maafisa hawa wamekuwa wakienda kinyume na maagizo ya Serikali la kuwataka waweze kuwakamilishia wananc...
Comments