Ommy Dimpoz atoka Afrika Kusini kwenye matibabu na kutua Kenya akiwa mwenye afya njema, abadilisha muonekano (+picha)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz ambaye kwa miezi miwili amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya koromeo, hatimaye msanii huyo amepona kabisa kwa ushahidi wa picha alizopiga akiwa nchini Kenya.
Ommy Dimpoz
Kwa mujibu wa kinyozi maarufu nchini Kenya, George Dufanda ameposti picha za msanii huyo akiwa katika muonekano tofauti kabisa lakini mwenye uso wa tabasamu.
Maelezo kutoka kwa watu wanaofanya kazi karibu na Ommy Dimpoz wamesema msanii huyo amewasili nchini Kenya wiki moja iliyopita ma ameahidi kufanya Birthday Party yake nchini humo Septemba 17.
Bado haijajulikana kwa nini Ommy Dimpoz hajafikia Tanzania nyumbani kwake moja kwa moja. Tazama picha zake akiwa na kinyozi huyo maarufu nchini Kenya.
Ommy Dimpoz akiwa na kinyozi aliyemnyoa
Ommy Dimpoz wiki mbili zilizopita alirudishwa tena nchini Afrika Kusini akitokea Tanzania kwa kutazamwa maendeleo ya afya yake baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo wa koromeo miezi miwili iliyopita.
Mimi ni mwanamke.Naomba msaada wa mawazo maana sijui nina nini mimi... Umri unanitupa mkono maana nakaribia miaka 35 lakini sijampata aliyewahi kunitangazia ndoa.Cha ajabu kila anayelala na mimi siku ya pili harudii tena na hata nikimpigia simu hapokei Hapo ndo linapoanzia tatizo na kunifanya nijisikie vibaya...Saivi hata mtaani nachagua kwa kupita... Kuna mwanaume mmoja huyo ndo aliwahi kunichana live kuwa nina maji mengi ila sielewi alimaanisha nini Jamani naomba msaada nifanyaje mie nipendwe kama wengine nyandichethedreamtz
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo amesema atawachukulia hatua za kisheria wazazi au walezi wasiowapeleka watoto shule. Alisema hayo juzi alipofanya ziara katika shule za msingi Chazige A na B alikokutana na wananchi na kusikiliza kero zao. Jokate alisema mzazi au mlezi asiyempeleka shule mtoto hasa wa kike hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo kupelekwa mahakamani. Alisema wataendelea na kampeni ya “Tokomeza Ziro” yenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu na miundombinu ya shule, madarasa na vyoo. Naye ofisa elimu msingi wilayani Kisarawe, Shomari Bane alisema: “Kampeni imetusaidia, wanafunzi kuanzia mwaka jana ufaulu darasa la saba uliongezeka na walifanya vizuri. Pia, Jokate alimuagiza mganga mkuu na madaktari wilayani Kisarawe kutoa dawa zilizopo hospitalini kwa wagonjwa na kama hazipo, watoe mbadala ili wananchi wasipate usumbufu.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Comments