Ommy Dimpoz atoka Afrika Kusini kwenye matibabu na kutua Kenya akiwa mwenye afya njema, abadilisha muonekano (+picha)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Ommy Dimpoz ambaye kwa miezi miwili amekuwa akisumbuliwa na matatizo ya koromeo, hatimaye msanii huyo amepona kabisa kwa ushahidi wa picha alizopiga akiwa nchini Kenya.
Ommy Dimpoz
Kwa mujibu wa kinyozi maarufu nchini Kenya, George Dufanda ameposti picha za msanii huyo akiwa katika muonekano tofauti kabisa lakini mwenye uso wa tabasamu.
Maelezo kutoka kwa watu wanaofanya kazi karibu na Ommy Dimpoz wamesema msanii huyo amewasili nchini Kenya wiki moja iliyopita ma ameahidi kufanya Birthday Party yake nchini humo Septemba 17.
Bado haijajulikana kwa nini Ommy Dimpoz hajafikia Tanzania nyumbani kwake moja kwa moja. Tazama picha zake akiwa na kinyozi huyo maarufu nchini Kenya.
Ommy Dimpoz akiwa na kinyozi aliyemnyoa
Ommy Dimpoz wiki mbili zilizopita alirudishwa tena nchini Afrika Kusini akitokea Tanzania kwa kutazamwa maendeleo ya afya yake baada ya kufanyiwa upasuaji mdogo wa koromeo miezi miwili iliyopita.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments