Aunt Ezekiel Adaiwa Kodi ya Pub Mwenyewe Afunguka Haya

NancyTheDreamtz
Aunt Ezekiel Adaiwa Kodi ya Pub Mwenyewe Afunguka Haya
STAA wa filamu za Kibongo, Aunt Ezekiel baada ya kudaiwa kukosa kodi ya kulipia pango la Pub yake iliyopo Kinondoni jijini Dar na kuifunga, mwenyewe amefungukia madai hayo na kueleza kilichotokea. 



Akizungumza na Risasi Jumamosi, Aunt alisema siyo kwamba amefunga Pub yake kwa sababu ya kudaiwa kodi bali eneo hilo anataka kufanya biashara nyingine na hiyo ya pub ataihamishia sehemu nyingine.



“Kwa nini nidaiwe kodi wakati nina biashara nyingine nafanya na zinaenda vizuri? Watu huongea vitu ambavyo hawavijui kabisa, nafanya marekebisho ili niweke biashara nyingine na hii nitaihamishia sehemu nyingine,” alisema Aunt.

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais