MAHABA NIUWE: Kanye West amlipa Kim Kardashian Tsh bilioni 2 kulinda penzi lake
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Rapper Kanye West imemlazimu kumlipa mke wake Kim Kardashian kiasi cha dola milioni $1 ambayo ni sawa na Tsh bilioni 2 baada ya kumzuia mke wake kuposti picha moja ya tangazo kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Kanye West na Kim West
Kim akiwa kwenye mahojiano ya uzinduzi wa Podcast ya mtangazaji maarufu nchini Marekani, Ashley Graham ‘Pretty Big Deal’, Kim amesema kuwa wiki moja kabla ya siku ya Mama duniani alitafutwa na kampuni kubwa ya mavazi nchini Marekani ikimtaka aposti picha moja ya tangazo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii na itamlipa dola laki 9.
Kim amesema yeye aliona ni fedha nyingi lakini ilimpasa aombe ushauri kwa mumewe, lakini Kanye West akamkatalia kufanya hivyo.
“Nilimpigia kuomba ushauri lakini akaniambia..’No babe, I really don’t want you to do that,’ nilipomuuliza kwanini? akasema kama unanipenda achana na hilo tangazo,“amesema Kim kwenye mahojiano hayo.
Hata hivyo, wiki mbele baadae May 12 mwaka huu siku ya Mama Duniani, Kanye alimtumia Kim maua na bahasha iliyokuwa na hundi (cheque) ya dola milioni 1 iliyoambatana na ujumbe uliosomeka “Nashukuru sana kwa kunisikiliza na kutoposti lile tangazo, nakupenda na nitakulinda kwa kila namna, furahia siku hii muhimu kwako“.
Ingawaje Kim hajaelezea sababu hasa ya kukatazwa kuposti tangazo hilo, lakini huenda isiwe ni ishu ya mahaba bali ikawa ni kutokana na ishu za kibiashara kwani na yeye ana bidhaa zake za mavazi za Yeezy.
Sikiliza interview yote ya Kim kwenye Podcast ya ‘Pretty Big Deal’
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Leo August 13, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli amefanya teuzi mbalimbali siku ya leo na kufanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Msafiri Simeoni wa Kwimba amepelekwa Chato, Senyi Simon amepelekwa Kwimba Wafuatao ni baadhi ya walioteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Majiji Halmashauri ya Misenyi Mkurugenzi ni Innocent Mbandwa Jiji la Mbeya Mkurugenzi ni James Kasusura Halmashauri ya Malinyi Mkurugenzi ni Mussa Elias Mnyeti Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ni Maulid Madeni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke ni Lusibilo Mwakabili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ubungo ni Beatrice Kwai Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kigamboni ni Mwilabu Nyabusu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa mkoani Dodoma ni Mustapha Yusuph Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi ni Tatu Seleman Kikwete Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko ni Masumbuko Stephano Mkurugenzi wa Halmashauri ya Katavi ni Ramadhan ...
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments