MAHABA NIUWE: Kanye West amlipa Kim Kardashian Tsh bilioni 2 kulinda penzi lake
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Rapper Kanye West imemlazimu kumlipa mke wake Kim Kardashian kiasi cha dola milioni $1 ambayo ni sawa na Tsh bilioni 2 baada ya kumzuia mke wake kuposti picha moja ya tangazo kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Kanye West na Kim West
Kim akiwa kwenye mahojiano ya uzinduzi wa Podcast ya mtangazaji maarufu nchini Marekani, Ashley Graham ‘Pretty Big Deal’, Kim amesema kuwa wiki moja kabla ya siku ya Mama duniani alitafutwa na kampuni kubwa ya mavazi nchini Marekani ikimtaka aposti picha moja ya tangazo kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii na itamlipa dola laki 9.
Kim amesema yeye aliona ni fedha nyingi lakini ilimpasa aombe ushauri kwa mumewe, lakini Kanye West akamkatalia kufanya hivyo.
“Nilimpigia kuomba ushauri lakini akaniambia..’No babe, I really don’t want you to do that,’ nilipomuuliza kwanini? akasema kama unanipenda achana na hilo tangazo,“amesema Kim kwenye mahojiano hayo.
Hata hivyo, wiki mbele baadae May 12 mwaka huu siku ya Mama Duniani, Kanye alimtumia Kim maua na bahasha iliyokuwa na hundi (cheque) ya dola milioni 1 iliyoambatana na ujumbe uliosomeka “Nashukuru sana kwa kunisikiliza na kutoposti lile tangazo, nakupenda na nitakulinda kwa kila namna, furahia siku hii muhimu kwako“.
Ingawaje Kim hajaelezea sababu hasa ya kukatazwa kuposti tangazo hilo, lakini huenda isiwe ni ishu ya mahaba bali ikawa ni kutokana na ishu za kibiashara kwani na yeye ana bidhaa zake za mavazi za Yeezy.
Sikiliza interview yote ya Kim kwenye Podcast ya ‘Pretty Big Deal’
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini Mwanza kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine. NancyTheDreamtz
NancyTheDreamtz Na Mwandishi Wetu, MOHA, Songea. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mkoa wa Ruvuma, Seif Mgonja kwa kosa la kutogawa kwa wananchi Namba za Utambulisho wa Taifa (NIN), 14,493 tangu Disemba 31, 2019, licha ya kuzalishwa na Makao Makuu na kuletewa ofisini kwake Mjini Songea. Pia Waziri Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa NIDA Wilaya ya Namtumbo, Mkoani humo, Thobias Nangalaba kwa uzembe wa kutofika katika kikao chake cha viongozi wa Mkoa na Wilaya, licha ya kupewa taarifa ya kuhudhuria kikao hicho. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Soko Kuu la Manispaa ya Songea Mkoani humo, leo, Waziri Lugola amesema, amewatengua vyeo maafisa wawili hao kwa kucheza na kazi za Serikali, kwa kutojali majukumu yao. “Ndugu wananchi wa Songea, maafisa hawa wamekuwa wakienda kinyume na maagizo ya Serikali la kuwataka waweze kuwakamilishia wananc...
NancyTheDreamtz Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC) leo Septemba 16, 2019, Imemuidhinisha mchezaji wa zamani wa Inter Milan na timu ya taifa ya Kenya, McDonald Mariga, kugombea ubunge katika jimbo la Kibra kwa tiketi ya Chama cha Jubilee. McDonald Mariga aliyevaa kofia Wiki iliyopita, uteuzi wa McDonald Mariga uliotangazwa na Chama cha Jubilee, uliingia dosari baada ya kukataliwa na Tume hiyo kwa madai kuwa taarifa zake zinakinzana. Kwenye uchaguzi huo, Mariga atachuana na msanii maarufu wa muziki nchini humo, Prezzo ambaye anagombea ubunge kwa tiketi ya chama cha Wiper. Mgombea mwingine ni Imran Okoth atasimama kwa tiketi ya Chama cha ODM, Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kibra utafanyika Novemba 7, mwaka huu.
Comments