Posts

Showing posts from August, 2018

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa filamu za Bongo Movie na mfanyabiashara Jacqueline Wolper amefunguka na kudai anatamani sana kama angetoa Penzi lake kwa Raisi. Wolper amedai anaona ni bora kama atakuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi kwa sasa statute Penzi pa Raisi yoyote Afrika kwani atakuwa salama zaidi kuliko kufaidi Penzi na wadananda wengine. Kwenye mahojiano na Global Publishers, Wolper alisema mara nyingi amekuwa kwenye uhusiano wa kimapenzi na wanaume ambao mwishoni wanamsaliti jambo ambalo halipendi na linamkera, lakini anaamini akimpa moyo wake wa upendo Rais yeyote Afrika anaona atakuwa salama. Unajua ndoto yangu mimi ningependa kutoa penzi langu kwa Rais maana najua kabisa, kwanza atakuwa ananiheshimu na itakuwa ni ngumu sana kunitenda kama wafanyavyo wengine na hapo nitatulia kabisa wala sitakumbuka wanaume wazugaji“. Wolper amekuwa muwazi kuhusu maumivu anayokutana nayo Kwenye  mapenzi yake ambapo uhusiano wake na staa wa Bongo fleva Harmonize uliisha baada ya kumuacha na Harmo

Breaking News: Magufuli Amuwashia Moto Makonda Sakata la Makondena Amtaka Alipe Kodi

Image
NancyTheDreamtz Rais John Magufuli ashangazwa na kitendo cha Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda kuingiza makontena 20 nchini yenye samani mbalimbali na kukataa kutalipia kodi akidai kwamba ni msaada kwa ajili ya kuboresha miundombinu ya elimu kwa mkoa huo. Magufuliamesema hayo leo wakati akizungumza na watumishi wa serikali wilayani chato mkoani Geita ambako yuko mapumzikoni. “Umezungumza na wafanyabiashara huko, umeingiza makontena yako eti yana fenicha za walimu hata shule zenyewe hazitajwi, nani amekwambia walimu wanahitaji masofa?” amesema Rais Magufuli. 

Ommy Dimpoz Kafunguka Kila Kitu Kuhusu Ugonjwa Wake....Anasema Alilishwa Sumu Bila Kujua

Image
NancyTheDreamtz Vipimo  vya afya alivyofanyiwa msanii wa Bongofleva, Omary Nyembo maarufu kama Ommy Dimpoz ambaye yupo nchini Afrika Kusini kwa matibabu, vimeonyesha aliwekewa sumu kwenye chakula. Ommy Dimpoz alianza kuugua mapema Mei mwaka huu na kwenda kutibiwa mjini Mombasa kabla ya kupelekwa Afrika Kusini ambako aligundulika kuwa na tatizo katika njia ya chakula ambako alifanyiwa upasuaji. Akizungumza na Kituo cha Redio cha Clouds, Dimpoz, alisema vipimo vya madaktari vimeonyesha tatizo lake linatokana na kuwekewa sumu kwenye chakula ama kinywaji. “Awali nilifanyiwa vipimo katika moja ya hospitali jijini Dar es Salaam na kugundulika nina kansa, lakini baada ya vipimo vikubwa huku Afrika Kusini, imeonekana nimekula sumu,”  alisema Ommy Dimpoz. Alisema anashukuru kuona hali yake imeanza kuimarika baada ya awali kushindwa kuzungumza kabisa na anaamini sala za Watanzania wenzake na watu ambao wamekuwa karibu naye zitamsaidia na kuweza kurejea kwenye hali yake.

Kauli ya Serikali kuhusu mwanafunzi aliyefariki kwa kipigo cha Mwalimu

Image
NancyTheDreamtz Waziri wa Elimu, Profesa Joyce Ndalichako amezungumzia tukio la kuuawa kwa mwanafunzi wa darasa la tano katika shule ya msingi Kibeta, mkoani Kagera Siperius Eradius akitaka vyombo vya usalama kuchukua hatua za kisheria dhidi ya mwalimu anayetuhumiwa. Akizungumza leo Agosti 29 wakati wa Kongamano la Kimataifa la Hisabati linalofanyika Chuo Kikuu cha Aga Khan, Profesa Ndalichako amedai kusikitishwa na tukio hilo na kwamba Serikali haitamfumbia macho yeyote atakayebainika kuhatarisha usalama wa wanafunzi shuleni, wakiwamo walimu wao. Amesema mwalimu aliyesababisha mauaji hayo hakutumwa na mtu isipokuwa utashi wake. Profesa amewaomba wananchi kuwa watulivu wakati vyombo vya usalama vinapofanya kazi yake na kwamba tukio hilo lisitoe tafsiri kuwa shule  siyo mahali salama kwa watoto.     Shule ni sehemu ambayo ni salama kwa hiyo asitokee mtu akafanya vitendo ambavyo hata wazazi wajiulize harugusu mtoto kwenda shule au asiende lakini serikali itachukua hatua kwa mtu

Benki Ya Standard Charted Kuimwagia Tanzania Sh. Trilioni 3.3 Kujenga Reli Ya Kisasa-SGR

Image
NancyTheDreamtz Na Benny Mwaipaja, WFM, Dar es Salaam BENKI ya Standard Chartered Group imekubali kuipatia Tanzania mkopo nafuu wa dola za Marekani bilioni 1.46 sawa na zaidi ya shilingi trilioni 3.3 kwa ajili ya kujenga kipande cha Reli ya Kiwango cha Kimataifa (SGR) kuanzia Morogoro hadi Makutupora, mkoani Dodoma. Hayo yamebainishwa na Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango, baada ya kukutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Mtendaji wa Benki hiyo Bw. Bill Winters, Jijini Dar es Salaam. Dkt. Mpango ameishukuru Benki hiyo kwa kukubali kugharamia ujenzi wa Reli hiyo ya kisasa ambayo lengo lake ni kuimarisha usafiri na usafirishaji wa abiria na mizigo kwenda bara na nchi jirani za Maziwa Makuu na zile ambazo hazipakani na Bahari. "Tunajenga Reli hiyo ya Kisasa kutoka Dar es Salaam - Morogoro hadi Makutupora ambazo ni awamu mbili lakini pia tutajenga reli hiyo kuelekea Isaka mpaka Mwanza na baadaye Rusumo ambapo wenzetu wa nchi ya Rwanda, tutasaidiana,

Tundu Lissu Kurejea Nchini Mwakani.....Kaka Yake Asema Risasi Iliyoko Ndani ya Uti wa Mgongo haitaondolewa

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine na ataendelea kubaki na risasi moja kwenye uti wa mgongo. Hayo yameelezwa leo Agosti 29 na kaka yake Lissu, Wakili Alute Lissu, alipozungumza na wanahabari. Amesema Lissu hatafanyiwa upasuaji mwingine baada ya kufanyiwa upasuaji zaidi ya mara nne akiwa Ubelgiji ingawa kuna risasi moja ambayo bado imebaki nyuma ya uti wa mgongo. “Wakijaribu kuitoa huenda ikaathiri uti wa mgogo na hivyo kupata tatizo la kupooza,"amesema. Lissu alihamishiwa hospitali ya Leuven iliyopo Ulelgiji akitokea hospitali ya Nairobi, baada ya kushambuliwa kwa risasi kadhaa na watu wasiojulikana Septemba 7 mwaka jana. Alute ambaye amerejea nchini, wiki hii akitokea Ubelgiji kumjulia hali Lissu, amesema huenda mwanasiasa huyo akarejea nchini mwakani, hasa kutokana na mfupa wa mguu wa kulia kuwa bado haujaunga vizuri. "Hali ya Lissu inaendelea vizuri, lakini napenda kukanusha taarifa kuwa kuna kamati ya mapokezi yake k

Chadema kumshtaki Waitara Kamati ya Maadili

Image
NancyTheDreamtz Chama cha Demokrasia Maendeleo (Chadema) kimempeleka kwenye kamati ya maadili mgombea ubunge wa jimbo la Ukonga kwa tiketi ya CCM, Mwita Waitara kwa kile walichodai kufanya uchochezi. Akizungumza leo Agosti 29, mkurugenzi wa oparesheni na mafunzo wa Chadema, Dingo Kigaila kuwa amesema sababu ya kumpeleka kwenye kamati hiyo ni kutokana na madai ya kuhamasisha vurugu kwa kupitia mtandao wa kijamii. Amesema kwa kutumia simu yake ya kiganjani Agosti 26 mwaka huu aliandika kwamba watu wa kabila lake yaani Wakurya hususani ukoo wa Wairegi wanoe mapanga yao na kumwaga damu katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi jimbo la Ukonga. Amesema Waitara alitumia lugha ya Kiswahili na Kikurya kuandika ujumbe huo, hivyo wameitaka kamati ya maadili, kumuita na kumuhoji mgombea huyo. Julai 28, 2018 Mwita Mwikwabe Waitara, alitangaza kujiuzulu nafasi yake ya Ubunge na kujivua nyadhifa zake zote ndani ya CHADEMA na kuhamia CCM.

Waziri Mkuu: Flyover Ya Tazara Imekamilika Kwa Asilimia 98

Image
NancyTheDreamtz WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesemaujenzi wa barabara ya juu katika eneo la Tazara umekamilika kwa asilimia 98 na itafunguliwa Oktoba mwaka huu na Rais Dkt. John Magufuli. Mradi wa barabara ya juu (Mfugale flyover) chini ya ufadhili wa Serikali ya Japani, unalengo la kupunguza msongamano wa magari katika makutano ya barabara ya Mandela na Nyerere.   Ameyasema hayo leo (Jumatano, Agosti 29 ,2018) baada ya kukagua ujenzi wa mradi huowa barabara ya juu katika eneo la Tazara jijini Dar Es Salaam. Waziri Mkuu amesema ameridhishwa kazi ya umaliziaji wa mradi huo inayoendelea kwenye hilo. “Mradi utapunguza muda wa usafiri katika barabara ya Nyerere hususani  kwa wananchi wanaotoka katikati ya jiji kwenda uwanja wa ndege na wanaotoka Buguruni, Temeke.” Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amewaagiza viongozi Mkoa wa Dar Es Salaam watafute eneo kwa ajili ya  wafanyabiashara ndogondogo ili waweze kuondoka kandokando ya barabara hizo za juu zinazojengwa.

Halima Mdee amuunga mkono Waziri Mpango Sakata la Makonda....."Laana ya KuKu haiwezi mpata Mwewe"

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Jimbo la Kawe kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), Halima Mdee ameunga mkono agizo la Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Philip Mpango la kupiga mnada makontena 20 ya mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Paul Makonda. Kupitia mtandao wake wa Twitter ameunga mkono agizo hilo huku akiwataka wananchi kujitokeza kununua samani hizo kama ambavyo Waziri Dkt.Mpango aliwataka watu wenye uwezo wa kununua wajitokeze bila kuogopa chochote. “Wenye pesa zenu mnada ukipigwa jongeeni kwa wingi, laana ya kuku haiwezi mpata mwewe,” ameandika Mdee kwenye ukurasa wake wa Twitter Aidha, Dkt. Philip Mpango, Agosti 27, 2018 aliagiza makontena 20 ya samani yaliyoingizwa nchini na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda yapigwe mnada ikiwa ni sehemu ya kusimamia sheria na kanuni za kodi zilizopo nchini. Hata hivyo, tangazo la TRA lililotolewa na Kaimu Kamishna wa Forodha na Ushuru, Ben Asubisye lilikuwa na orodha ya makontena zaidi ya 800, huku jina l

Kelvin John ‘Mbappe’ Kazitosa Simba, Yanga malengo yake ‘yakiutu-uzima’

Image
NancyTheDreamtz Kelvin John ‘Mbappe’ amekuwa gumzo sana kwenye timu ya taifa ya vijana wa U17 Serengeti Boys mshambuliaji anaevaa jezi namba 10. Inawezekana umemuona lakini hufahamu historia yake hadi kufika Serengeti Boys. Jina Kelvin Pius John mchezaji wa timu ya taifa ya vijana ‘Serengeti Boys’, nina umri wa miaka 16 nipo kidato cha pili. Ni mtoto wa ngapi kwa mzee Pius John? Tupo wawili, kwa upande wa mama nipo pekeangu lakini kwa baba tupo wawili, mimi ndio mtoto wa kwanza. Form Two mwaka huu wana fanya mtihani wa taifa, anajigawa vipi shule na mpira? Nikiwa kambini kabla ya mashindano, kuna program naifanya kupitia laptop yangu. Natumiwa material ya shule na home work au vipindi vilivyoendelea darasani wakati mimi sipo mwalimu ananitumia kupitia email yangu nafanyia kazi. Natumiwa mitihani pia nafanya halafu namtumia tena mwalimu. Elimu ni kitu kikubwa, mpira una mwisho naweza kufika umri ambao huwezi tena kucheza mpira lakini ukiwa na elimu unaweza kufungua kampuni na kujie

BASATA washikwa kigugumizi kujibu sakata la WCB na Rich Mavoko ‘nyie mmesikia kafukuzwa tayari?’ (+video)

NancyTheDreamtz araza la Sanaa Taifa (BASATA) leo limewakutanisha tena Rich Mavoko na Uongozi wa WCB akiwemo Diamond Platnumz kujadili ishu ya mkataba inayoendelea kati ya msanii huyo na lebo ya WCB. BASATA wameshindwa kueleza kwa kina ni mambo gani waliyoafikiana lakini wamesema wanachojua ni kwamba Rich Mavoko yupo WCB na hajafukuzwa hizo ni ishu za mitandaoni.

Simba Yafungua Ligi Vizuri Yaitandika Tanzania Prison Bao 1-0

Image
NancyTheDreamtz MABINGWA watetezi, Simba wameanza vizuri Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kuichapa Tanzania Prisons ya Mbeya bao 1-0 katika mchezo uliofanyika usiku huu Uwanja wa Taifa mjini Dar es Salaam. Bao la Simba limefungwa na mshambuliaji kutoka Rwanda, Meddie Kagere aliyefunga dakika ya pili kwa shuti kali baada ya kupewa pasi na John Bocco kutoka upande wa kulia. Kikosi cha Simba: Aishi Manula, Shomari Kapombe, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’, Pascal Wawa, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, James Kotei, Hassan Dillunga/Nicholas Gyan dk82, Meddie Kagere, John Bocco/Adam Salamba dk83 na Shiza Kichuya/Muzamil Yassin dk67. Tanzania Prisons: Aaron Kalambo, Benjamin Asukile, Laurian Mpalile, Nudrin Chona, James Mwasote, Jumanne Elfadhili, Salum Kimenya, Cleophace Mkandala, Kelvin Friday/Lambert Sabiyanka dk82, Salum Bosco/Ramadhani Ibata dk71 na Ismail Aziz/Hassan Kapalata dk79. 

Nuh Mziwanda Afunguka Mazito Kuhusu Mjengo wa Shilole "Mimi Nilichangia Kununua"

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa muziki wa Bongo fleva Nuh Mziwanda ameibuka kuwa ana yeye pia aliweka mkono Kwenye kununua Mjengo mpya wa Shilole aliouanika Kwenye mitandao ya kijamii. Ikiwa ni siku chache zimepita tangibly shilole aanikr Mjengo wenye thamani ya zaidi milioni 90 anaoujenga hivi sasa, aliyekuwa mpenzi wake Nuh Mziwanda amedai na yeye pia ana chake Kwenye Mjengo huo.

Watoto wa Mzee Majuto Wafukuka Kuhusu Tuhuma za Kumfukuza Mama Yao

Image
NancyTheDreamtz Siku chache baada ya mke wa marehemu Mzee Majuto, Aisha Yusufu kudai kufukuzwa na familia ya msanii huyo, ndugu wametoa msimamo wao kuhusiana na sakata hilo wakisema wamezisikia tuhuma hizo. Madai hayo yanakuja ikiwa ni siku 15 zimepita tangu alipofariki msanii huyo maarufu wa vichekesho aliywahi kutamba na filamu kama Back From New York, Inye na Mzee wa Chabo. Wiki iliyopita mwanamke huyo alizungumza na vyombo vya habari akidai kwamba baada ya kumalizika kwa shughuli za maziko, ndugu walimwambia aanze kujitegemea kwa kila kitu ikiwemo chakula, jambo ambalo alilitafsiri ni sawa na wamemfukuza. Katika maelezo yake mama huyo wa watoto wanne, amesema ndugu hao walimwambia kwamba ataishi kwa fedha za pole ambazo waombolezaji mbalimbali wameendelea kumpa. MCL Digital ilizungumza na Hamza ambaye ni mtoto wa kwanza wa Mzee Majuto kwa njia ya simu, ambaye alisema hayupo tayari kuongea kwa sasa hivi lolote juu ya suala hilo mpaka hapo itakapofika siku ya kufanya arobaini. “A

Idriss Aamua Kupita Njia za Daimond Baada ya Kuwa na Wema Sasa Atoka Kimapenzi na Lynn

Image
NancyTheDreamtz Msanii wa Bongo movie na comedian maarufu Idris Sultan anadaiwa kuwa Kwenye Mahusiano ya Kimapenzi na Ex girlfriend wa staa wa Bongo fleva Diamond Platnumz. Kumekuwa na tetesi kuwa Video vixen ambaye hakauki vituko Kwenye mitandao ya kijamii Irene Geofrey maarufu kama Lynn ana banjuka na Idris Sultan. Tetesi za Mahusiano ya wawili hao zilianza juzikati ambapo watu wengi walipigia mstari baada ya mwanadada huyo kuposti picha ya Idris huku akiandika maneno ya kimahaba yalisomeka; “Babyboo baby boo bae.” Baada ya Tetesi hizo kupamba moto Kwenye mitandao ya kijamii gazeti la Risasi Vibes, lilimsaka Lynn ambaye mara moja alikana kuwapo kwa Mahusiano hayo: Unajua muda mwingine unaweza kuposti kitu halafu maneno yakajiandika yenyewe, sasa ndicho kilichonitokea na mimi sikutaka kufuta kwa sababu watu wangesema ni kiki. Lakini Idris ni mshikaji wangu wa karibu sana na ninampenda anavyochekesha, watu wasinitengenezee mambo ambayo hayapo jamani“.

Ninja Agoma Kuitumia Jezi ya Can­navaro..... Bado Aiweka Kabatini

Image
NancyTheDreamtz Jezi ya Yanga yenye namba 23 ambayo Nadir Haroub ‘Can­navaro’ alimkabidhi Abdallah Shaibu ‘Ninja’ aendelee kuitumia baada ya yeye kustaafu kucheza soka, jezi hiyo bado ipo kabatini. Cannavaro ambaye ni meneja wa Yanga kwa sasa, hivi karibuni alitan­gaza kustaafu kucheza soka akiwa nahodha wa timu hiyo ambapo uongo­zi ulitaka kuistaafisha jezi yake, lakini yeye akakataa na kumkabidhi Ninja. Ninja ambaye alisajiliwa na Yanga msimu uliopita, bado hajaanza kuitumia jezi hiyo na wikiendi iliyopita kwenye mchezo wa Kombe la Shirikisho dhidi ya USM Alger alivaa jezi yake namba 6 aliyokabidhiwa wakati anatua Yanga. Kwa mujibu wa Gazeti la Championi, Ninja amesema jezi hiyo anasubiri kuan­za kuitumia kwenye Ligi Kuu Bara msimu huu ambao unaanza leo huku Yanga ikicheza ke­sho Alhamisi dhidi ya Mtibwa Sugar kwenye Uwanja wa Uhuru, Dar. “Unajua jezi niliyoachiwa na Cannavaro siwezi kuitumia kwenye michuano ya kimataifa kwa sababu kule natam­bulika ninaitumia jezi namba 6, lakin

Breaking News: Bobi Wine Akamatwa Tena Muda Mfupi Baada ya Kuondolewa Mashtaka

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amekamatwa muda mfupi baada ya mahakama ya kijeshi kumuondolea mashtaka ya umiliki haramu wa silaha nchini. Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na inaarifiwa kwamba anatarajiwa kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa. Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo aliwasilishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.

Seebait.com 2018SeeBait Rapper 50 Cent Amsifia Nick Minaj Licha ya Kuchanwa Vibaya na Mrembo Huyo

Image
NancyTheDreamtz Rapper 50 Cent amekuwa wa kwanza kujibu kati ya male rappers kadhaa waliochanwa kiutani na Nicki Minaj kwenye wimbo wake wa hivi karibuni 'Barbie Dreams' kutoka kwenye album ya QUEEN. Kwenye mahojiano na 'Extra' kupitia Hip Hop N More, 50 Cent ameweka wazi hisia zake juu ya wimbo ule kwa kuupa alama 100. Alisema: "Nimeupenda ule wimbo, niliwahi kufanya wimbo unaitwa 'How to Rob' na aliwahi kusema mwenyewe (Nicki Minaj) kuwa alivutiwa nao sana." alisema 50 Cent na kumsifia Nicki kwa uandishi wake wa mtindo wa mtazamo tofauti yaani kinyume (reverse perspective) Aliongeza pia kuwa 'Barbie Dreams' inaonesha wazi kabisa kuwa wanawake kwenye Hip Hop wameanza kuchukua nguvu kutoka kwa wanaume - Swipe kuona interview hiyo. Kwenye dude hilo, 50 Cent alichanwa kwenye line isemayo: "I tried to f k 50 for a powerful hour, but all that ni *a wanna do is talk 'Power' for hours." alichana Nicki. Wengine waliotajwa kwenye w

Ray C "Wabongo Mitandaoni Wanapenda tu Vitu vya Kijinga vya Maana Holla"

Image
NancyTheDreamtz Mwanamuziki mkongwe nchini Tanzania, Ray C amedai kwamba asilimia kubwa ya watanzania hawajui kuitumia mitandao ya kijamii ipasavyo ili iwaingizie fedha, na badala yake wanaitumia kwa kujadili mambo yasiyo na tija kwa mtu mwenyewe na taifa kwa ujumla. Ray C ameeleza hayo wakati akizungumza na www.eatv.tv hii leo Agosti 23, 2018, na kusema watu wengi wamekuwa wakipoteza muda na fedha zao kuingia kwenye mitandao hiyo bila ya kufikiria ni jinsi gani itaweza kuwarudishia faida. "Watu wengi mitandaoni wanapenda upuuzi, ukiweka kitu cha maana hakuna mtu ambaye ata 'comment' chochote katika hicho ulichokiweka, maana wanakichukulia poa lakini fanye kinyume chake hapo ndio utawajua walipo. Wenzetu Ulaya mitandao ya kijamii kama wakina Kim Kardishian na wengine wanatumia mitandao hiyo kuuza 'product' na kuonyesha kazi zao ili wapate pesa... lakini sisi ndio tumekuwa wakutoa pesa kwa kununua bando ili tukaharibu, tena sana sana Tanzania hatujui kutumia mita

Young Dee "Ile Gari Nimenyanganywa Haipo Tena Mikononi Kwangu"

Image
NancyTheDreamtz Rapper Machachari Young Dee Ametoboa siri kuwa kwa sasa ile gari aliyoinunua kwa mil 25 haipo mikononi mwake kwani ilinunuliwa na Uongozi aliyokuwa nayo kipindi cha nyumba hivyo wamechukua gari lao Young Dee akihojiwa ameweka wazi kuwa kwa sasa anataka kununua Lambogini kama mambo yakimwendea vizuri Young kwa sasa anakampuni yake inayoitwa Dream City ambayo inasimamia kazi zake pia

Wanaharakati Kenya Waungana Kumpinga Rais Museven wa Uganda

Image
NancyTheDreamtz Nchini Kenya wanaharakati pamoja na wanasiasa wamejiunga na wenzao wa Uganda kushinikiza utawala wa rais wa Yoweri Museveni kuzingatia sheria na kuwaachilia huru wafungwa wa kisiasa. Makundi ya kutetea haki za binadamu yamesema yatawasilisha kesi katika mahakama ya Jumuiya ya Afrika Mashariki ili kuishinikiza serikali ya rais Museveni kuzingatia sheria dhidi ya wafungwa wa kisiasa.

Breaking News: Bobi Wine Akamatwa Tena Muda Mfupi Baada ya Kuondolewa Mashtaka

Image
NancyTheDreamtz Mbunge wa Kyadondo nchini Uganda Robert Kyagulanyi maarufu Bobi Wine amekamatwa muda mfupi baada ya mahakama ya kijeshi kumuondolea mashtaka ya umiliki haramu wa silaha nchini. Muda mfupi baada ya kuachiliwa huru, Wine alikamatwa tena na inaarifiwa kwamba anatarajiwa kushtakiwa katika mahakama ya hakimu mkuu kujibu mashtaka ya uhaini pamoja na wabunge wengine waliokamatwa. Mbunge huyo ambaye pia ni mwanamuziki nchini kwa jina maarufu Bobi Wine leo aliwasilishwa katika mahakama ya kijeshi mjini Gulu kaskazini mwa Uganda.