Masaa 48 Yamepita Bado Mo Dewji Ajapatikana Baba yake aulizwa ishu ya simu ya mwanaye kuwa hewani

NancyTheDreamtz
Masaa 48 Yamepita Bado Mo Dewji Ajapatikana Baba yake aulizwa ishu ya simu ya mwanaye kuwa hewani
Jeshi la Polisi bado linaendelea kumsaka mfanyabiashara mkubwa nchini Tanzania Mohamed Dewji ‘Mo’ ikiwa ni zaidi ya saa 48 zimepita tangu atekwe nyara na watu wasiojulikana wakati akingia kufanya mazoezi katika gym ya Colosseum, Oysterbay jijini Dar leo Oktoba 11.


Hadi sasa mamlaka zinazohusika hazijatoa taarifa mpya kuhusu upatikanaji wa ‘Mo’.

Ijumaa hii baba wa mfanyabiashara huyo, Gulam Dewji Hussein alipotafutwa na Mwananchi kuzungumzia taarifa zozote kuhusu mwanaye, alisema familia ilikuwa haijapata chochote kutoka polisi hadi jana jioni.

Alipoulizwa kuhusu simu ya mwanaye inayosemekana ikipigwa inaita na kupokea ujumbe mfupi wa maandishi (sms), mzazi huyo alimtaka mwandishi wa habari hizi asubiri kwa kuwa muda huo (wa jioni) alikuwa na wageni na asingeweza kuzungumzia suala hilo. Hata alipotafutwa baadaye hakuweza kupatikana.

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais