Muziki wetu wa BongoFleva kwa sasa umekuwa kama Bubble Gum (Big G) unakula na kutema – Lamar

Mwandaaji wa Mziki wa kizazi kipya kutoka hapa Tanzania ambaye kwa sasa anajishughulisha na vitu vingine nje na muziki kama vile kufungua kituo cha kuoshea magari (Carwash) pamoja na sehemu ya kupikia na kuuzia chakua (Restaurant)  Lamar,amefunguka na kusema kuwa muziki wa Bongo Flava kwa sasa hauna ladha.

Lamar ameongea hayo katika mahojiano aliyoyafanya na kituo cha habari cha Clouds Fm na kuongea yote jinsi anavyouona muziki wa sasa na muziki wa kipindi cha nyuma kidogo Lamar amesema:-

“Muziki wa sasa hivi uko Bubble Gum (Big G) unautafuna halafu unautema tofauti na muziki wa zamani akimaanisha kipindi cha nyuma ambao uko kimziki zaidi maana unaishi muda mrefu,hii ni kwasababu ya upangiliaji wa codes za muziki (akimaanisha mfumo) maana zamani walikuwa wacheza codes ambazo zinaishi muda mrefu tofauti na sasa hivi ambao hutumii codes bali watu wameurahisisha tu kwani umekuwa muziki wa kawaida tu”



Lamar amefunguka hayo kwa hisia sana kwani muziki wetu ulipotoka ni mbali na kuna baadhi ya kundi la watu wanataka kuupoteza muziki wetu mana wanaleta mambo ya kuiga zaidi.

Kinachochangia zaidi i aina ya waandaji (Maproducer) wa kipindi hicho cha nyuma kidogo na waandaji wa sasa hivi ambao wameufanya muziki kuwa rahisi.

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais