China wadai huenda Virus vya Corona Vilienezwa na jeshi la USA
NancyTheDreamtz Na AFP AFISA wa cheo cha juu wa China amedai huenda jeshi la Amerika lilipeleka virusi hatari vya corona nchini humo huku maradhi hayo yakiendelea kuenea mataifa mbalimbali na kuua watu zaidi ya 5,000. Bila kufafanua, msemaji wa wizara ya ulinzi wa China, Zhao Lijian, aliandika kwenye Twitter kwamba, kuna uwezekano virusi hivyo vilipelekwa China na wanajeshi wa Amerika. Dai lake linawiana na habari zilizoenezwa kwenye mitandao ya kijamii nchini China zikilaumu Amerika kwa mkurupuko huo. Mkuu wa kituo cha kudhibiti maradhi nchini China amesema, maradhi hayo yalianza soko la Wanyama katika jiji la Wuhan. Hata hivyo, maafisa wa China na wataalamu mashuhuri wa afya wanadai huenda virusi hivyo vilitoka kwingineko. China imefokea maafisa wa Amerika wanaoita maradhi hayo “virusi vya Wuhan.” Kwenye ujumbe wake wa Twitter, Zhao alipakia video ya mkuu wa kituo cha kuzuia maradhi cha Amerika akiwa mbele ya bunge la Congress akisema, baadhi ya r...