Posts

Maneno ya AY na Fid Q kwa Mavoko, Hatukuwahi kuwa na wasiwasi juu yake tuliamini atarudi tu na atafanya vizuri (+Video)

Image
Wasanii wa muziki wa Bongo Fleva  @fidq_words  na  @aytanzania  walikuwa miongoni mwa watu waliojitokeza kwenye tukio la  @richmavoko  na walipopata nafasi ya kuongea walimshauri Mavoko maneno haya. Mbali na  @aytanzania  na  @fidq_words  kupata nafasi ya kuongea pia  @petitman_wakuache  alipata wasaa wa kuuliza swali na ilikuwa hivi. NancyTheDreamtz

Mama mzazi wa Rich Mavoko ashindwa na uvumilivu atimba jukwaani, aongea maneno mazito (+Video)

Image
Katika tukio la kuzindua Minitape ya  @richmavoko  imehudhuriwa na watu mbalimbali, miongoni mwa watu waliohudhuria ni Pamoja na mama yake mzazi. Baada ya kukaribishwa kuongea hakuwa na maneno mengi bali atoa ujumbe huu. NancyTheDreamtz

Alikiba aweka historia Mtwara afanya show ya kiutu uzima zaidi, taa zazimwa mashabiki watumia simu zao (+Video)

Image
Moja ya Show kubwa kufanyika katika kipindi hiki baada ya Corona kupungua Tanzania ni hii ya CEO wa  @kingsmusicrecords   @officialalikiba  Katika show hiyo ambayo ikifanyika katika uwanja wa Nangwanda Sijaona mjini Mtwara  @officialalikiba  ameweza kufanya show kubwa sana. Baada ya Show hiyo  @officialalikiba  anatarajiwa kurejea DSM mapema leo kwani kuna mchezo wa  #NIFUATE  yaani Teamkiba na TeamSamatta ambao utachezwa uwanja wa Mkapa. Pia Tatehe 14/8/2020 anatarajiwa kuelekea Kigoma kwa ajili ya show yake.   NancyTheDreamtz

Rich Mavoko afunguka kuruhusiwa kuzitumia nyimbo zake na lebo ya Diamond WCB, hata akaunti ya Youtube ya kwangu (+Video)

Image
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva Rich mavoko amefunguka kuhusu kuzitumia ngoma alizofanya akiwa bado yupo chini ya Diamond Platnumzkatika lebo ya WCB, Rich ameweka wazi kuhusu kuzitumia nyimbo hizo na kumiliki akaunti mbili za Youtube yaani ile ya Rich Mavoko na Bilionea Kid. Msikilize Rich Mavoko kwa ufasa. NancyTheDreamtz

Paul Makonda Kashindwa Kujizuia Katoboa Siri ya Diamond Platnumz Kwenda Kulipa Mahari

Image
Mh Paul Makonda  Amethibitisha Mwezi Ujao Yeye Akiambatana Na Diamond Platnumz Kwenda Kutoa Mahari ,Japo Mwanamke Anayetaka Kuolewa Na Diamond Platnumz Hajawekwa Wazi Ni Yupi...Ameyasema hayo akiwa kwenye Sherehe ya harusi ya Esma Platnumz Usiku uliopita NancyTheDreamtz

Gari yaacha njia nakuua wanafunzi watatu Arusha,wawili wajeruhiwa

Image
Wanafunzi watatu waliokuwa wanasoma katika shule ya Olmoti mkoani Arusha ,wamefariki na wengine wawili kujeruhiwa  baada yakugongwa na gari ambayo  imeacha njia Kamanda wa polisi mkoa wa Arusha Salum Hamduni amesema gari hiyo ilikuwa ikiendeshwa na Sariko Mwenda katika barabara ya East Afrika eneo la Olmort,ambapo iliacha njia nakuwagonga wanafunzi hao walikokuwa wanatembea pembezoni mwa barabara wakitoka shule “Chanzo cha ajali hiyo ni uzembe na dereva alishindwa kumudu gari lake nakupoteza  mwelekeo nakugonga gari nyingine ubavuni pamoja na baiskeli,mtuhumiwa amekamatwa”-Kamanda Hamduni NancyTheDreamtz

Afanyiwa Upasuaji na Kutolewa Kijiko, Betri, Vitambaa Tumboni

Image
Hospitali Teule ya Wilaya ya Missenye ya Mugana mkoani Kagera imefanya upasuaji na kutoa kijiko, betri ndogo ya redio na vitambaa kwenye tumbo la mgonjwa wa akili. Vitu vingine vilivyotolewa vilivyokuwa vimeziba njia ya haja kubwa na kumfanya apate maumivu makali ya tumbo ni vibiriti viwili vya gesi, mswaki na ganda la limao. Dk Eliud Nyonyi aliyeshiriki kumfanyia upasuaji mgonjwa huyo amesema baada ya vitu hivyo kutolewa hali ya mgonjwa huyo inaendelea vizuri. “Hiyo picha inayosambaa mitandaoni sijaiona, lakini ni kweli kuna mgonjwa tumemfanyia upasuaji na tumemkuta hivyo vitu tumboni, ila siwezi kuzungumzia zaidi taarifa za mgonjwa,” alisema. Picha inayoonyesha vitu hivyo imekuwa ikisambaa kwenye mitandao mbalimbali huku kila mtu akisema lake kuhusu vitu hivyo. Dk Nyonyi ambaye anakaimu nafasi ya mganga mkuu wa hospitali hiyo alimtaja mgonjwa huyo kuwa ni Eliud Novart (25) na kwamba, bado amelazwa katika wodi ya wagonjwa waliofanyiwa upasuaji akiendelea kupatiwa matibabu. Mganga mkuu...