Posts

Kasi ya Kagere Yamuibua Hamissi Tambwe "Kagere ni Moto wa Kuotea Mbali Sitashangaa Akiwa Mchezaji Bora Msimu Huu"

Image
NancyTheDreamtz Mshambuliaji wa Yanga, Amissi Tambwe, ameibuka na kusema straika wa Simba, Meddie Kagere ni moto wa kuotea mbali. Ni baada ya Kagere kufunga mabao yote mawili juzi, wakati Simba ikiichinja JKT Tanzania 2-0 kwenye mchezo wa Ligi Kuu Bara katika Uwanja wa Mkwakwani, Tanga. Tambwe amesema amekuwa akimfuatilia kwa karibu mchezaji huyo ambaye alijiunga na Simba Juni, mwaka huu akitokea Gor Mahia ya Kenya. Tambwe amempongeza Kagere kwa kufikia rekodi yake ya kufunga mabao saba katika mechi 11 za kwanza Simba. Alisema, yeye pia msimu wa 2013/14 aliposajiliwa na Simba akitokea Vital’O ya Burundi, alifunga mabao saba katika mechi 11 za kwanza. “Kwa hiyo, Kagere ni mmoja kati ya washambuliaji hatari sana msimu huu na jinsi mambo yanavyoenda, sitashangaa kama ataibuka mfungaji bora. “Ana tofauti kubwa na washambuliaji wengine wa Simba, anafunga Uwanja wa Taifa lakini pia katika viwanja vya mikoani, kwa hiyo nampongeza kwa hilo, lakini pia kitendo chake cha kuifikia rekodi yang...

Daimond Amuomba Alikiba Kuungana naye Kwenye Tamasha Lake la Wasafi Festival

Image
NancyTheDreamtz MKURUGENZI wa Wasafi Media, Naseeb Abdul ‘Diamond Platnumz’ amemuomba msanii mwenzake, Alikiba,  kuungana naye kwenye Tamasha la Muziki lililoandaliwa na uongozi wa Wasafi ili kuonyesha kwamba wasanii wa Tanzania wanaweza kufanya matamasha makubwa kama yanayofanywa kwenye mataifa makubwa kama Marekani, Canada na Uingereza. Diamond amesema hayo leo Jumatatu, Novemba 5, 2018 wakati akizindua tamasha hilo na Urushaji wa Matangazo wa Kituo cha Redio cha Wasafi FM katika ofisi za Wasafi media zilizopo, Mbezi Beach jijini Dar es Salaam. “WASAFI FESTIVAL ni tamasha la kwetu wote, tunataka tujitahidi sana kuhakikisha msanii yeyote ambaye atakua tayari kushirikiana na sisi, tutashirikiana naye, tutafurahi sana kwenye Wasafi Festival endapo tukiwa na mtu kama Alikiba, kwa sababu ni tamasha la nyumbanui, ni matamasha yetu. “Lengo letu ni kuonyesha watu wa nje kuwa muziki wa Tanzania ni mkubwa kwelikweli, ndicho tunachotaka kukifanya, hata kama mtu akitoka Ulaya, Marekani a...

Kidato Cha NNE Kuanza Mitihani Leo....Serikali Yatoa Onyo Kwa Watakaoiba Mitihani

Image
NancyTheDreamtz Mtihani  wa taifa wa kidato cha nne unaanza leo, huku Baraza la Taifa la Mitihani (Necta) likitoa onyo kali kwa watakaobainika kujihusisha na vitendo vya udanganyifu. Baraza hilo limesisitiza kuwa halitasita kukifutia matokeo kituo chochote cha mtihani ambacho kitabainika kujihusisha na udanganyifu. Hayo yalisemwa jana jijini Dar es Salaam na Katibu Mtendaji wa Necta, Dk. Charles Msonde, alipozungumza na waandishi wa habari kuhusiana na mtihani huo ambao utawahusisha jumla ya watahiniwa 427,181. Dk. Msonde alisema baraza linazitaka kamati za mitihani za mkoa, halmashauri kuhakikisha kuwa taratibu zote za uendeshaji mitihani ya taifa zinazingatiwa ipasavyo. “Kamati zihakikishe kuwa mazingira ya vituo vya mitihani yapo salama, tulivu na kuzuia mianya yote inayoweza kusababisha kutokea kwa udanganyifu,” alisema. Alisema wasimamizi wote wanatakiwa kufanya kazi yao kwa umakini na uadilifu wa hali ya juu. Wasimamizi wanaaswa kujiepusha na vitendo ...

Matokeo ya Uchaguzi wa Simba SC

Image
NancyTheDreamtz Club ya Wekundu wa Msimbazi Simba SC Jumapili ya November 4 2018 ilifanya mkutano wake mkuu sambamba na uchaguzi mkuu wa mwenyekiti na wajumbe wa Bodi ya wakurugenzi wa kampuni ya Simba SC ambapo kura zilihesabiwa hadi alfajiri ya November 5 2018. Simba SC sasa inahesabika kama kampuni baada ya kufanikiwa kuingia katika mfumo wa mabadiliko ya uwekezaji wa hisa, ambapo mfanyabiashara Mohammed Dewji ndio alishinda Zabuni ya uwekezaji ndani ya club ya Simba hivyo maamuzi ya timu hiyo kwa sasa yatakuwa yanajadiliwa ndani ya bodi.

Breaking News: Mahakama Yamwachia Huru Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo

Image
NancyTheDreamtz Mahakama ya Hakimu Mkazi Iringa imemuachia huru Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi (TSNP), Abdul Nondo leo Novemba, 5  baada ya upande wa Jamhuri kushindwa kuthibitisha makosa mawili yaliyokuwa yanamkabili Nondo alikuwa anakabiliwa  na mashtaka mawili; shitaka la kwanza ni kusambaza taarifa za uongo akiwa jijini Dar es Salaam kuwa ametekwa na kosa la pili ni kutoa taarifa za uongo akiwa mjini Mafinga kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.

Kimewaka tena: Marekani Yaiwekea Vikwako Iran....Jeshi La Iran leo Kufanya Mazoezi Makubwa Kuonesha Ubabe Wao

Image
NancyTheDreamtz Marekani imetangaza kuwa leo Nov 5 imeirejeshea vikwazo nchi ya Iran vitakavyolenga sekta ya mafuta na sekta ya kifedha. Marekani imesema imeiwekea Iran vikwazo vigumu zaidi ambavyo haijawahi kuiwekea. Vikwazo hivyo vitalenga mauzo ya mafuta, usafiri kwa njia ya baharini na mabenki ambavyo vyote ni muhimu sana kwa uchumi. Maelfu ya raia wa Iran wakiwa na mabango yaliyoandikwa  "Kifo kwa Marekani" wameandamana  wakiitaka serikali  yao kutofanya mazungumzo yoyote na Marekani. Jeshi la Iran nalo limesema kuwa litafanya mazoezi ya kijeshi leo Jumatatu na Jumanne kuonyesha uwezo wake wa kijeshi. Marekani imetangaza vikwazo hivyo  baada ya  Rais Trump kutangaza  kujitoa kwenye  mkataba wa mwaka 2015 uliolenga kupunguza mipango ya nyuklia ya Iran. Marekani inasema inataka kuzima vitendo viovu vya Ina vikiwemo udukuzi wa mitandao, majaribio ya makombora ya masafa marefu na uungaji mkono wa makundi ya kigaidi mashariki ya kat...

RC Makonda Afunguka Siri Ya Kumwaga Machozi Kanisani...."Watu Wanadhani ni Utani, Ila Mbinguni Wanajua"

Image
NancyTheDreamtz Siku moja baada ya Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda kutokwa na machozi akiwa katika ibada katika kanisa la Efatha linaloongozwa na mtumishi wa Mungu Josephat Mwingira kiongozi huyo ameibuka na kutoa neno. Kupitia ukurasa wake wa Instagram Makonda amechapisha video ambayo alionekana  anatokwa na machozi kanisani hapo na kuandika ujumbe ambao alibainisha watu wengi hawajui kilichotokea. Makonda ameandika;  “Powerful, very powerful watu hawaelewi nini kimefanyika Ila mbinguni wameelewa na wameandika, people think it’s a joke. Ila kwa Mungu hakuna mzaha, asante Mungu Kwa kusimama upande wangu” Hivi karibuni Mkuu wa huyo wa Mkoa Dar es salaam alianzisha kampeni maalum ya kuwakamata watu wanaojihusisha na mapenzi ya jinsia moja, na kuunda kamati maalum ya watu 17 ili ya kushughulika na suala hilo. Jana kupitia ofisi ya Wizara ya Mambo ya Nje,  serikali ilisema zoezi linaloendeshwa na Mkonda  ni mawazo yake binafsi na si msimam...