Skip to main content

Hii ndio sababu ya Tundu Lissu kusimamishwa kufanya kampeni kwa siku 7

Kamati ya Maadili ya Kitaifa imemsimamisha kufanya kampeni kwa siku 7 mgombea urais kupitia CHADEMA, Tundu Lissu, kutokana na malalamiko yaliwasilishwa na vyama viwili vya NRA na CCM ya kutoa lugha ya uchochezi na tuhuma zisizothibitika.

Taarifa hiyo imetolewa leo Oktoba 2, 2020 na Katibu wa kamati ya maadili ya kitaifa Emmanuel kawishe, ambapo imedaiwa kuwa maneno hayo ya uchochezi aliyatoa akiwa mkoani Mara na Geita na kamati imeridhia kuwa Lissu amekiuka maadili ya uchaguzi.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa barua ya kumtaka Lissu kujibu tuhuma hizo iliwasilishwa kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA, ambapo alijibu kuwa malalamiko hayakihusu chama, na hivyo kamati hiyo imeridhia kuwa taarifa kuhusu malalamiko ya ukiukwaji wa maadili iliwasilishwa kwa mlalamikiwa kwa kuwa CHADEMA ndiyo ilimdhamini kuwa mgombea wa urais, hivyo barua kuwasilishwa kwa katibu mkuu ni sahihi kabisa.

Related Articles


NancyTheDreamtz

Comments

Popular posts from this blog

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Top Ten ya Makabila Yaliyotoa Wasomi Wengi Nchini Tanzania

Jacqueline Wolper Atamani Kutoka Kimapenzi na Rais