Posts

Showing posts from August, 2020
Image
Msemaji wa Simba, Haji Manara jana alikuwa kivutio kwenye Tamasha la Simba Day baada ya kupanda jukwaani la kucheza Yope wimbo wa mwanamuziki Diamond Platniumz na Mkongomani Innos’B. Tamasha hilo lilifanyika Uwanja wa Mkapa, Dar na kuhudhuriwa na maelfu ya mashabiki ambapo Diamond na kundi lake la WCB walipiga bonge la shoo kabla ya mechi ya timu hiyo na Vital’O ya  Burundi. Katika tukio hilo kundi hilo likicheza wimbo huo Manara naye aliavamia jukwaa na kuanza kuwanogesha mashabiki kwa kucheza sambamba na wasanii hao. Kwa jinsi jamaa alivyokuwa akienda sambamba na wanasanii hao ilikuwa ni kama walifanya mazoezi ya pamoja na hivyo kuzua shangwe za kumshangilia. NancyTheDreamtz

CCM YA 2020 INAONYESHA UKOMAVU KWA KUFANYA UCHAGUZI WA UMOJA WA VIJANA

Image
    Chama Cha Mapinduzi kimezidi kuonyesha ukomavu kwa kufanya Uchaguzi ulio Thabiti nakuweza kupata wabunge wa viti maalumu UVCCM kupitia mchakato vijana walionyesha ukomavu kwa Vijana na kufanikiwa kuwapata wawakilishi hao bila kulipua hata kidogo                                              NancyTheDreamtz

UMAWEZA BADO INAENDELEA KUONYESHA UIMARA WAKUKZA ELIMU YA SAYANSI VISIWANI ZANZIBAR

Image
      Ilikuonyesha dhamira ya dhati katika kuipa morali jamii ya Zanzibar Taasisi ya Umaweza imeonyesha uimara zaidi katika maonyesho ya Nanenane visiwani humo kwa kuonyesha bidhaa zinazoweza kumfanya Mwanafunzi kuwa imara katika elimu ya sayansi kwakuweka vitendea kazi vinavyoweza kumpa Mwanafunzi uelewa zaidi wakisayansi kama uonavyo picha hapo chini                                            NancyTheDreamtz

UNASUMBULIWA na Fangasi za Sehemu za Siri...? Usijali Zingatia Haya Kujitibu Bila Gharama Yeyote Ile..!!!

Image
Ugonjwa wa fangasi (Candidiasis) husababishwa na vimelea vijulikanavyo kwa kitaalamu kama ‘Candida albicans’. Vimelea hivi hushambulia jinsia zote lakini hushambulia zaidi wanawake sababu ya maumbile yao ya sehemu za siri kuwa na unyevunyevu kitu kinachopelekea wao kuathiriwa zaidi kuliko wanaume. Watu karibu wote tunaishi na vimelea hivi katika miili yetu kwa kiwango kidogo sana. Kinga ya mwili ikisaidiwa na bakteria wazuri wa mwili ndiyo kupambana na vimelea hivi hata unaona huuguwi ila kinga ya mwili ikiyumba kidogo na bakateria wabaya kuongezeka ndipo hapo unapokutana na ugonjwa kamili. Tatizo la kuwashwa sehemu za siri ni tatizo kwa watu wengi miaka ya sasa na linawapata watu wa jinsia na rika zote yaani watoto, vijana hata wazee. Fangasi siyo sababu pekee ya kuwashwa sehemu za siri, kuna sababu na magonjwa mengine yanahusika na tatizo hili na kupona au kuondoka kwa sababu hizo ndiyo kupona kwa huo muwasho. Sababu za muwasho sehemu za siri za mwanaume Sababu zifuatazo zinaweza kuh

Ibraah Tz "Siwezi kuwa na Jacqueline Wolper"

Image
Msanii wa lebo ya Konde Gang Music Ibraah Tz "Chinga" amesema hawezi kuwa kwenye mahusiano na Jacqueline Wopler kwa sababu anamchukulia kama mama yake japokuwa Harmonize alimpigia pande ili awe nae kwenye mahusiano.  Akizungumzia suala hilo la kupigiwa pande na Harmonize ili awe kwenye mahusiano na Wolper, Ibraah Tz amesema anamchukulia msanii huyo wa filamu kama mama yake na yeye bado yupo single.  "Ule ulikuwa ni utani tu unajua kuna muda kaka natakiwa ni-enjoy naye, haiwezi kuwa mimi nitoke na Jacquline Wolper yule ni mama yangu ananisapoti kwa hiyo namshuru sana sapoti yake ni kubwa kwangu, bado sina mahusiano nikiwa nayo nitaweka wazi na watu watajua" ameeleza Harmonize " NancyTheDreamtz

Wabunge wa chama cha Christian Kataeb cha Lebanon wajiuzulu ubunge

Image
Katika kadhia nyingine, mke wa balozi wa Uholanzi nchini Lebanon amefariki leo kutokana na majeraha yaliyosababishwa na mlipuko uliotokea kwenye bandari ya Beirut Jumanne iliyopita. Taarifa hiyo imetolewa na wizara ya mambo ya nje ya Uholanzi.  Wizara hiyo imeelezea masikito juu ya kifo cha mama huyo aliyekuwa na umri wa miaka 55. Syria imesema wananchi wake 43 walikuwa miongoni mwa watu waliokufa kutokana na mlipuko wa mjini Beirut. Wakati huohuo wabunge wa chama cha wakristo cha Kataeb wamejiuzulu ubunge.  Mwenyekiti wa chama hicho Sami Gemayel amesema wabunge hao wamejiondoa kutoka kwenye bunge hilo la wabunge 128 ili kupigania nchi wanayoitaka isiyobagua baina wa watu wa Lebanon. Gemayel amesema hayo kwenye maziko ya katibu wa chama hicho aliyekufa kutokana na mlipuko wa jumanne iliyopita. Chama cha Kataeb kilikuwa na wabunge watatu. NancyTheDreamtz

Timu Samatta Yachapwa Mabao 3-1 Na Timu Kiba, Morrison Akosa Penalti

Image
TIMUKiba leo imeibuka na ushindi wa mabao 3-1 mbele ya TimuSamatta kwenye mchezo wa hisani wa SamaKiba Foundation uliochezwa Uwanja wa Mkapa. Lengo la mchezo wa leo ni kurejesha kile wanachokipata kwa jamii ambapo mchezo wa leo ulikuwa ni wa tatu kwa TimuKiba na TimuSamatta kukutana huku mechi zote mbili zilizopita ushindi ulikuwa ni kwa TimuSamatta hivyo leo TimuKiba imepata ushindi wa kwanza. Mabao ya upande wa TimuKiba yalifungwa na Ibrahim Ajibu  dakika ya 25,Mudhathir Yahya dakika ya 53 na la tatu lilipachikwa na Hassan Dilunga dakika ya 90. Bao pekee la TimuSamatta lilifungwa na Yahaya ambaye alijifunga dakika 59. TimuSamatta walipata penalti mbili zote zilipigwa na Bernard Morrison ambaye alikosa penalti ya kwanza baada ya kumpa pasi Idd Naldo aliyepaisha na ile ya pili Morrison aliipaisha mwenyewe. Kiba amesema kuwa ni furaha kwa mashabiki kujitokeza kwa wingi huku akiwaomba waendelee kutoa sapoti. NancyTheDreamtz

Ndoa ya MONDI, ZUCHU Utamu Unakuja, unakata

Image
NDOA anayotarajia kufunga mwanamuziki mkubwa barani Afrika, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ imeibua mambo mazito, huku akihusishwa na msanii wake, Zuhura Othman ‘Zuchu’. Mwishoni mwa wiki iliyopita, Diamond au Mondi alitangaza kufunga ndoa Oktoba 2, mwaka huu ambayo ni siku ya kumbukumbu ya kuzaliwa kwake (birthday). UTAMU UNAKUJA, UNAKATA Chanzo kutoka ndani ya familia ya Mondi kimedai kwamba, kuna shinikizo kubwa kwa jamaa huyo kutoka kwa baadhi ya ndugu ambao wanamtaka amuoe Zuchu, jambo ambalo linaleta utamu na furaha ndani yao. Lakini wapo ambao wanachukizwa mno na taarifa au shinikizo hilo la Mondi kutakiwa amuoe Zuchu, hivyo hao ndiyo wanakata kabisa utamu wa tukio hilo. VUGUVUGU LA MONDI KUMUOA ZUCHU Vuguvugu la Mondi kutakiwa kumuoa Zuchu, lilianza muda mfupi tu baada ya Aprili 8, mwaka huu, pale mrembo huyo aliposainiwa kwenye Lebo ya Wasafi Classic Baby (WCB) chini ya Mondi. Baada ya hapo, wawili hao wakawa wanapostiana kwenye mitandao ya kijamii na familia ya Mondi kumsifi

Simba Washtuka, Wabadili Siku Ya Kumtambulisha Morrison

Image
UONGOZI wa Simba ni kama umeshtukia kitu, ni baada ya kuchukua maamuzi ya kusogeza mbele siku ya kumtambulisha kiungo mshambuliaji Mghana, Bernard Morrison. Mghana huyo jana zilizagaa tetesi za kutambulishwa na uongozi wa Simba baada ya kufikia muafaka mzuri na kusaini mkataba wa miaka miwili ya kukipiga Msimbazi. Kiungo huyo alijiondoa kwenye kikosi cha Yanga mara baada ya mchezo wa Nusu Fainali ya Kombe la FA iliyochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam iliyomalizika kwa Simba kushinda mabao 4-1. Taarifa ambazo imezipata Championi Jumamosi, kiungo huyo tayari amesaini mkataba wa miaka miwili wenye thamani ya Sh 230Mil kwa siri kwa ajili ya kuichezea timu hiyo. Mtoa taarifa huyo alisema kuwa Mghana huyo atatambuLishWa rasmi Simba Day ambayo imepangwa kufanyika Agosti 22, mwaka huu Uwanja wa Taifa baada ya kupata ruhusa kutoka TFF. Aliongeza kuwa mabosi wa Simba wana uhakika mkubwa wa kumpata kiungo huyo mwenye mbwembwe nyingi ikiwemo ya kuupanda mpira kwa juu baada ya kupen

Tazama Kitumbo cha Sarah Baada ya Harmonize Kutangaza Kuwa ni Mjauzito....

Image
Tazama Kitumbo cha Sarah baada ya Harmonize kutangaza kuwa ni MJAMZITO VIDEO: NancyTheDreamtz

Matokeo ya Kura za Maoni Viti Maalum UVCCM

Image
Katika Mkutano wa Baraza kuu la umoja wa vijana UVCCM, uliofanyika jana Agosti 8, 2020, zoezi la upigaji kura wa kupata wabunge wa viti maalumu katika kundi la vijana limemalizika. Halima Bulembo Matokeo ya kura za maoni UVCCM Wabunge wa Viti Maalum Kundi la Vijana Baraza la Wawakilishi nafasi mbili. Walioongoza ni, 1. Saraham Mohamed kura 66 2. Hudhaina Mbaraka Kura 50 Matokeo ya kura za maoni UVCCM Wabunge wa Viti Maalum Kundi la Vijana Wabunge Zanzibar nafasi nne. Walioongoza ni, 1. Munira Khatib kura 88 2. Latifa Juakali kura 84 3. Amina Baraka Yusuf kura 79 4. Amina Ally Mzee Kura 73 Matokeo ya kura za maoni UVCCM  kupata Wabunge wa Viti Maalum Kundi la Vijana, Wabunge Tanzania Bara nafasi sita. Walioongoza ni, 1. Lulu Mwacha kura 77 2. Halima Bulembo kura 74 3. Juliana Masaburi kura 70 4. Lucy John kura 48 5 na 6 wamefungana, Judith Kipenga na Asia Abdukarim kura 33. NancyTheDreamtz

Magufuli si Mgombea wa Tanzania Pekee Bali Afrika Nzima Inamuhitaji

Image
T anzania IPO katika nchakato wa Uchaguzi Mkuu, miongoni mwa wagombea URAIS ni Mheshimiwa Daktari John Joseph Pombe Magufuli. Rekodi alizovunja Mheshimiwa JPM nchini Tanzania, Afrika na dunia nzima, zinamfanya asiwe mgombea wa Tanzania pekee Bali tegemeo LA Afrika kama mfano wa Kiongozi bora, shupavu, jasiri, Mzalendo na Mchapakazi. Katika nchi nyingi, RAIA na viongozi wanamtazama Magufuli kama kiongozi bora wa mfano wa kuigwa katika ulinzi wa Rasilimali na Maendeleo ya nchi. Tungekuwa na uchaguzi wa RAIS wa Afrika, JPM angeshinda kwa kura nyingi maana Afrika inamhitaji kuliko yeye anavyoihitaji Afrika. Hizi rekodi zake haziwezi kufikiwa na Rais mwingine yeyote wa Afrika hivyo kumpambanua kama kiongozi bora wa karne hii: 1. Kuongoza nchi ya kiafrika kwa miaka mitano bila kukanyaga Ulaya, Amerika wala Asia 2. Kuzuia safari za nje kwa viongozi na watumishi wa umma ili viongozi wawatumikie wananchi 3. Kudhibiti biashara ya kulevya nchini 4. Kudhibiti ujangili 5. Kujenga ukuta ili kulinda