Posts

Showing posts from March, 2020

Jinsi Mgonjwa wa Kwanza wa CORONA Alivyoingia Uganda

Image
NancyTheDreamtz Waziri wa Afya wa Uganda, Ruth Jane Aceng alisema kisa hicho kilichothibitishwa ni raia wa Uganda mwenye miaka 36 ambaye aliingia nchini humo akitokea Dubai Jumamosi Machi 21 saa 2 asubuhi kwa ndege ya Shirika la Ethiopia (Ethiopian Airlines). Dk Aceng alisema mtu huyo ni mkazi wa eneo la Kibuli Kangungulu katika mji mkuu Kampala. "Mtu huyo alisafiri kwenda Dubai Machi 17, kwa sababu za biashara. Wakati wa kusafiri kwake alikuwa mzima kiafya," alisema Dk Aceng. Aceng alisema mtu huyo kwasasa ametengwa katika Hospitali ya daraja la Entebbe. Abiria wote waliosafiri na mtu huyo wako chini ya uangalizi na hati zao za kusafiria zimeshikiliwa na Serikali. Siku ya Jumamosi, Rais Yoweri Museveni alitangaza kwamba Uganda imefunga mipaka yote ili kuzuia watu kuvuka nchini kwa lengo la kujilinda na ugonjwa huo ambalo limekuwa janga duniani baada ya kuripotiwa vifo zaidi ya 10,000. Museveni leo Machi 22, 2020 atazungumza kuhusu hatua zitak

Harmonize Aanza Kupasua Anga Kumkalisha Diamond Platnumz Kupitia Afroeast

Image
NancyTheDreamtz  Wanapotajwa wasanii wakubwa wa Bongo Fleva nchi hii, jina la Harmonize haliwezi kuwekwa kando, licha ya kuingia katika tasnia hiyo miaka michache iliyopita. Ni kama vile ameanza kupasua anga kivyake vyake nchi ya WCB, wiki iliyopita alidhihirishia hadhira kuwa ni miongoni mwa wasanii wakubwa wa muziki wa kizazi kipya, kwa kufanya uzinduzi wa kishindo wa albamu yake ya kwanza aliyoipa jina la Afroeast2020 yenye nyimbo 18 uliofanyika katika Ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Harmonize anasema licha ya kutumia muda mwingi kubuni namna atakavyofanya uzinduzi huo, alichokuja nacho kilikubaliwa na wengi ikiwamo wasanii wenzake. “Lakini nimejifunza kitu, kuwa napaswa niendelee kuwa mbunifu ili nieleweke na mashabiki wangu na wanaofuatilia muziki wa kizazi kipya. “Muziki wenyewe kwa ujumla umekuwa sana, si ajabu kukuta wimbo wa Bongofleva unasikilizwa Marekani na kwingineko duniani, hivyo kuna kitu tunafanya kinachotakiwa kuongezwa vionj

Breaking News: Tanzania Yathibitisha Kuwa na Mgonjwa Mmoja wa CORONA..Aliingia Nchini Jana Kupitia Uwanja wa Ndege KIA

Image
Waziri wa Afya Ummy Mwalimu amesema mtanzania mmoja ambaye aliingia nchini Machi 15 kupitia uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro akitokea Ubelgiji amethibitika kuwa na virusi vya Corona. Ummy amesema ni mwanamke mwenye miaka 46.

Trump Akataa Kupima Corona ilihali waziri awekwa karantini

Image
× BREAKING NEWS Polisi Yapiga Mabomu Chadema Waliomfuata Mbowe Segerea Breaking News: Corona Yatua Kenya, Mmoja Athibitika CCM Yamnasua Mashinji Jela, Yamlipia Mil. 30 – Video Trump Agoma Kupima Corona, Waziri Mkuu Awekwa Karantini March 13, 2020 by  Global Publishers WAZIRI Mkuu wa  Canada, Justin Trudeau,  na mke wake watabaki kwenye karantini kwa siku 14, baada ya mkewe, Sophie Gregoire Trudeau, kukutwa na virusi vya Corona na ambaye kwa mujibu wa mkurugenzi wa mawasiliano wa Waziri Mkuu, ”anaendelea vizuri na dalili alizonazo si mbaya.” Bwana Trudeau pia atakuwa kwenye karantini kama hatua ya tahadhari. Hatapimwa katika hatua za sasa kwa kuwa haonyeshi dalili za maambukizi. Katika ukurasa wa Twitter, Bi Sophie aliandika ”nitarejea nikiwa na afya njema hivi karibuni.” Bi Trudeau amesema alikuwa amepata dalili ambazo hazikuwa za kawaida na kuongeza kuwa ”kuwa kwenye karantini si kitu ukilinganisha na fa