UCHAGUZI KENYA: Mchezaji wa zamani wa Inter Milan, McDonald Mariga kutoana jasho na Prezzo
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC) leo Septemba 16,
2019, Imemuidhinisha mchezaji wa zamani wa Inter Milan na timu ya taifa
ya Kenya, McDonald Mariga, kugombea ubunge katika jimbo la Kibra kwa
tiketi ya Chama cha Jubilee. McDonald Mariga aliyevaa kofiaWiki
iliyopita, uteuzi wa McDonald Mariga uliotangazwa na Chama cha Jubilee,
uliingia dosari baada ya kukataliwa na Tume hiyo kwa madai kuwa taarifa
zake zinakinzana.
Kwenye uchaguzi huo, Mariga atachuana na msanii
maarufu wa muziki nchini humo, Prezzo ambaye anagombea ubunge kwa
tiketi ya chama cha Wiper.
Mgombea mwingine ni Imran Okoth
atasimama kwa tiketi ya Chama cha ODM, Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kibra
utafanyika Novemba 7, mwaka huu.
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments