Sikuwahi kuolewa, najua tunakokwenda wanawake watakuwa na nguvu kuliko akina baba – Mh. Anne Makinda (+video)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Anne Makinda ameelezea historia yake fupi ya maisha toka enzi anasoma hadi kuja kufanikiwa kuwa kiongozi mkubwa bungeni.
Mhe. Anne Makinda
Mhe. Makinda amesema maisha yake yote yalikuwa bungeni na kipindi hicho amesema kuwa alikuwa na fujo sana kuliko hizi ambazo zinafanywa na baadhi ya wabunge wa vyama vya upinzani bungeni.
“Mimi maisha yangu yote yalikuwa bungeni, mimi mwenyewe kama kuwa mtu wa fujo i was of those.. nilikuwaga backbencher nilikuwa na fujo nawambia ndugu zangu akina Tundu Lissu kuwa kwanza nyie hamuwezi kunifikia mimi,“amesema Anna Makinda.
Akielezea upande wa mahusiano Bi. Makinda amesema yeye hakuwahi kubahatika kuolewa na amewaasa wanawake waliokwenye ndoa kuwa makini sana pale wanapopata mafanikio kwani ndio kipindi cha kushirikiana karibu sana na wanaume zao ili kufika mbali.
“Mimi sikuwahi kuolewa lakini nilipopata mtoto wangu, aliyenisaidia sana ni dada yangu. Kwa hiyo nikiwa shuleni tu IDM nikipata ile shilingi 20 kumi napeleka kwa dada, 10 nabaki nazo kwa hiyo toka huko nilikuwa nafanya kazi I have to survive .“amesema Bi. Makinda na kusisitiza jambo kwa wanawake walioolewa.
“Tunakokwenda najua kabisa akina mama watakuwa na nguvu zaidi kuliko akina baba, na ndio maana nawa-advice pia tujifunze kuwapenda hawa watu. Kwa sababu kama wewe ni Couple umeolewa halafu unakuwa successful kuliko mume wako, usipoweza kumeneji hiyo anaweza kukuharibia hata wewe, ni vizuri kumshirikisha ikawa ile successful yako ikawa ni part ya familia yako au successful ya couple yenu,“amesema Anne Makinda akielezea historia yake kwenye mahojiano na TGNP Mtandao, tazama video hapa chini.
Mhe. Anne Makinda ndiye mwanamke wa kwanza nchini Tanzania kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na alishawahi kuhudumu pia kwenye shirika la UNICEF .
Mimi ni mwanamke.Naomba msaada wa mawazo maana sijui nina nini mimi... Umri unanitupa mkono maana nakaribia miaka 35 lakini sijampata aliyewahi kunitangazia ndoa.Cha ajabu kila anayelala na mimi siku ya pili harudii tena na hata nikimpigia simu hapokei Hapo ndo linapoanzia tatizo na kunifanya nijisikie vibaya...Saivi hata mtaani nachagua kwa kupita... Kuna mwanaume mmoja huyo ndo aliwahi kunichana live kuwa nina maji mengi ila sielewi alimaanisha nini Jamani naomba msaada nifanyaje mie nipendwe kama wengine nyandichethedreamtz
Mkuu wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani, Jokate Mwegelo amesema atawachukulia hatua za kisheria wazazi au walezi wasiowapeleka watoto shule. Alisema hayo juzi alipofanya ziara katika shule za msingi Chazige A na B alikokutana na wananchi na kusikiliza kero zao. Jokate alisema mzazi au mlezi asiyempeleka shule mtoto hasa wa kike hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yake ikiwamo kupelekwa mahakamani. Alisema wataendelea na kampeni ya “Tokomeza Ziro” yenye lengo la kukusanya fedha kwa ajili ya kujenga nyumba za walimu na miundombinu ya shule, madarasa na vyoo. Naye ofisa elimu msingi wilayani Kisarawe, Shomari Bane alisema: “Kampeni imetusaidia, wanafunzi kuanzia mwaka jana ufaulu darasa la saba uliongezeka na walifanya vizuri. Pia, Jokate alimuagiza mganga mkuu na madaktari wilayani Kisarawe kutoa dawa zilizopo hospitalini kwa wagonjwa na kama hazipo, watoe mbadala ili wananchi wasipate usumbufu.
NancyTheDreamtz MFUNGAJI wa mabao ya mwisho yaliyoipeleka hatua ya makundi na Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika timu ya Simba Mzambia, Clatous Chota Chama ‘Triple C’ ameongeza mkataba mwingine wa miaka miwili ya kuendelea kuichezea timu hiyo. Huyo, ni mchezaji wa sita kwa Simba kuongezewa mkataba wengine ni John Bocco, Erasto Nyoni, Jonas Mkude, Aishi Manula, Mohammed Hussein ‘Tshabalala’ na Meddie Kagere. Chama alijiunga na Simba kwenye msimu uliopita wa Ligi Kuu Bara akitokea Power Dynamo inayocheza ligi ya nchini huko. Taarifa ya klabu ya Simba inaeleza kuwa kiungo huyo atakuwa sehemu ya kikosi hicho hadi 2020 baada ya kuongeza mkataba huo. Simba hivi sasa ipo kwenye mikakati ya kukiboresha kikosi hicho kwa ajili ya michuano ya kimataifa Afrika na kikubwa kufika hatua ya fainali baada ya msimu uliopita kufika robo fainali. Timu hiyo hadi hivi sasa tayari imefanikiwa kuwasajili wachezaji wapya watano ambao ni Beno Kakolanya, Kennedy Juma, Gerson Fraga ...
Comments