Sikuwahi kuolewa, najua tunakokwenda wanawake watakuwa na nguvu kuliko akina baba – Mh. Anne Makinda (+video)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Aliyewahi kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Bi. Anne Makinda ameelezea historia yake fupi ya maisha toka enzi anasoma hadi kuja kufanikiwa kuwa kiongozi mkubwa bungeni.
Mhe. Anne Makinda
Mhe. Makinda amesema maisha yake yote yalikuwa bungeni na kipindi hicho amesema kuwa alikuwa na fujo sana kuliko hizi ambazo zinafanywa na baadhi ya wabunge wa vyama vya upinzani bungeni.
“Mimi maisha yangu yote yalikuwa bungeni, mimi mwenyewe kama kuwa mtu wa fujo i was of those.. nilikuwaga backbencher nilikuwa na fujo nawambia ndugu zangu akina Tundu Lissu kuwa kwanza nyie hamuwezi kunifikia mimi,“amesema Anna Makinda.
Akielezea upande wa mahusiano Bi. Makinda amesema yeye hakuwahi kubahatika kuolewa na amewaasa wanawake waliokwenye ndoa kuwa makini sana pale wanapopata mafanikio kwani ndio kipindi cha kushirikiana karibu sana na wanaume zao ili kufika mbali.
“Mimi sikuwahi kuolewa lakini nilipopata mtoto wangu, aliyenisaidia sana ni dada yangu. Kwa hiyo nikiwa shuleni tu IDM nikipata ile shilingi 20 kumi napeleka kwa dada, 10 nabaki nazo kwa hiyo toka huko nilikuwa nafanya kazi I have to survive .“amesema Bi. Makinda na kusisitiza jambo kwa wanawake walioolewa.
“Tunakokwenda najua kabisa akina mama watakuwa na nguvu zaidi kuliko akina baba, na ndio maana nawa-advice pia tujifunze kuwapenda hawa watu. Kwa sababu kama wewe ni Couple umeolewa halafu unakuwa successful kuliko mume wako, usipoweza kumeneji hiyo anaweza kukuharibia hata wewe, ni vizuri kumshirikisha ikawa ile successful yako ikawa ni part ya familia yako au successful ya couple yenu,“amesema Anne Makinda akielezea historia yake kwenye mahojiano na TGNP Mtandao, tazama video hapa chini.
Mhe. Anne Makinda ndiye mwanamke wa kwanza nchini Tanzania kuwa Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na alishawahi kuhudumu pia kwenye shirika la UNICEF .
MSANII nguli wa muziki wa R&B na Bongo Fleva, Benham Paul ‘Ben Pol’, usiku wa kuamkia leo Juni 19, 2021 amefanya shoo ya aina yake jijini Mwanza kwenye tamasha lake la Nandy Festival 2021. Nandy, amesindikizwa na wanamuziki wengine akiwemo Baba Levo, Fid Q, Meja Kunta na wengine. NancyTheDreamtz
NancyTheDreamtz Na Mwandishi Wetu, MOHA, Songea. WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi Kangi Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) Mkoa wa Ruvuma, Seif Mgonja kwa kosa la kutogawa kwa wananchi Namba za Utambulisho wa Taifa (NIN), 14,493 tangu Disemba 31, 2019, licha ya kuzalishwa na Makao Makuu na kuletewa ofisini kwake Mjini Songea. Pia Waziri Lugola amemuondoa madarakani Afisa wa NIDA Wilaya ya Namtumbo, Mkoani humo, Thobias Nangalaba kwa uzembe wa kutofika katika kikao chake cha viongozi wa Mkoa na Wilaya, licha ya kupewa taarifa ya kuhudhuria kikao hicho. Akizungumza katika mkutano wa hadhara uliofanyika Viwanja vya Soko Kuu la Manispaa ya Songea Mkoani humo, leo, Waziri Lugola amesema, amewatengua vyeo maafisa wawili hao kwa kucheza na kazi za Serikali, kwa kutojali majukumu yao. “Ndugu wananchi wa Songea, maafisa hawa wamekuwa wakienda kinyume na maagizo ya Serikali la kuwataka waweze kuwakamilishia wananc...
NancyTheDreamtz Tume Huru ya Uchaguzi na Mipaka nchini Kenya (IEBC) leo Septemba 16, 2019, Imemuidhinisha mchezaji wa zamani wa Inter Milan na timu ya taifa ya Kenya, McDonald Mariga, kugombea ubunge katika jimbo la Kibra kwa tiketi ya Chama cha Jubilee. McDonald Mariga aliyevaa kofia Wiki iliyopita, uteuzi wa McDonald Mariga uliotangazwa na Chama cha Jubilee, uliingia dosari baada ya kukataliwa na Tume hiyo kwa madai kuwa taarifa zake zinakinzana. Kwenye uchaguzi huo, Mariga atachuana na msanii maarufu wa muziki nchini humo, Prezzo ambaye anagombea ubunge kwa tiketi ya chama cha Wiper. Mgombea mwingine ni Imran Okoth atasimama kwa tiketi ya Chama cha ODM, Uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kibra utafanyika Novemba 7, mwaka huu.
Comments