Harmonize achafua hali ya hewa mtandaoni, Barnaba na Eugy kutoka Ghana watoa baraka zao (+video)
Get link
Facebook
X
Pinterest
Email
Other Apps
-
NancyTheDreamtz
Msanii wa muziki wa Bongo Fleva, Harmonize amekuwa gumzo mitandaoni kwa siku ya leo Tanzania baada ya kutangaza kuwa anaachia ngoma mpya.
Harmonize
Harmonize kupitia ukurasa wake wa Instagram amewaahidi kuwa ataachia video ya wimbo wake mpya endapo atatapata maoni (Comments) zaidi ya 2000.
Posti hiyo mpaka sasa imeshangaa masaa manne na tayari imefikisha comments 3000+ na views 102,000+ na kinachofuatia sasa ni mashabiki wake kumuandama mitandaoni mkali huyo wa Kwangwaru kuachia kichupa hicho.
Wengine waliotoa neno juu ya ujio wa ngoma hiyo ni mwanamuziki Barnaba na Eugy kutoka nchini Ghana ambao nao wamedai kuwa wimbo huo utakuwa ni moto wa kuotea mbali.
“Aiseee hili chuma, chuma naikumbuka mzee balaa sana ni chuma na nusuu,“ameandika Barnaba huku msanii wa muziki kutoka Ghana, Eugy akiandika “Let’s goooo!!“.
Ngoma hiyo mpya ya Atarudi ni ngoma ya tatu ya Harmonize kufanya kwa mwaka huu baada ya ngoma yake ya DM Chick na Kwangaru aliyomshirikisha Diamond Platnumz kufanya vizuri.
Je, Atarudi huenda ukawa wimbo mkubwa na mkali zaidi ya Kwangwaru na DM Chick?
NancyTheDreamtz Huu kwa mujibu wa utafiti wa kabila zilizotoa wasomi wengi nchini tanzania. 1.wahaya wanapatikana mkoani kagera wakitokea bukoba na sehemu zingine za mkoa huoo 2.wagitaa wanapatikana wilaya ukerewe na musoma mjini na vijini mkoani mara 3.wachaga mkoani kilimanjaro wa wilaya ya moshi mjini,marangu,hai na sehemu zingine 4.wanyakyusaa mkoani mbeya wapo haswa wilaya ya kyela,songwe na zinginezo. 5.wakurya mkoani mara wilaya ya tarime na serengeti 6.wajaluo mkoani mara wilaya ya rorya na serengeti pia 7.wangoni wanatokea mkoa wa ruvuma 8.wapare wanatokea mkoa kilimanjaro wilaya ya same. 9.wasukuma hawa wapo mwanza na shinyanga 10.wanyamwezi hawa wanatokea mkoani tabora
Leo August 13, 2018 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dr. John Magufuli amefanya teuzi mbalimbali siku ya leo na kufanya mabadiliko madogo ya Wakuu wa Wilaya, Mkuu wa Wilaya ya Kwimba Msafiri Simeoni wa Kwimba amepelekwa Chato, Senyi Simon amepelekwa Kwimba Wafuatao ni baadhi ya walioteuliwa na Rais Magufuli kuwa Wakurugenzi wa Halmashauri na Majiji Halmashauri ya Misenyi Mkurugenzi ni Innocent Mbandwa Jiji la Mbeya Mkurugenzi ni James Kasusura Halmashauri ya Malinyi Mkurugenzi ni Mussa Elias Mnyeti Mkurugenzi wa Jiji la Arusha ni Maulid Madeni Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Temeke ni Lusibilo Mwakabili Mkurugenzi wa Halmashauri ya Ubungo ni Beatrice Kwai Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kigamboni ni Mwilabu Nyabusu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kondoa mkoani Dodoma ni Mustapha Yusuph Mkurugenzi wa Halmashauri ya Moshi ni Tatu Seleman Kikwete Mkurugenzi wa Halmashauri ya Kakonko ni Masumbuko Stephano Mkurugenzi wa Halmashauri ya Katavi ni Ramadhan ...
NancyTheDreamtz Jeshi la Uganda limezindua mifuko ya kondomu katika kambi yake ya kijeshi ya UPDF Bombo iliyopewa kibwagizo cha usiende nyama kwa nyama. Kwa mujibu wa Shirika la habari la BBC, Brigedia Leopoldo Kyanda amesema mwanajeshi hawezi kutekeleza wajibu wake ipasavyo bila wenyewe kujilinda kutokana na maambukizi ya zinaa na hususan virusi vya ukimwi. Kondomu hizo zimepewa jina Ulinzi na zinatarajiwa kusaidia katika juhudi za kupunguza kuenea kwa virusi vinavyosababisha Ukimwi. Kitengo cha kukabiliana na maambukizi ya Ukimwi jeshini kilizindua nembo hiyo mpya kwa ushirikiano na mashirika mawili yasiyo ya kiserikali.
Comments