Posts

Nyandichethedreamtz

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele

Siri Yafichuka, Prince Dube Anakwenda Yanga Kuziba Nafasi ya Fiston Mayele YANGA wanahitaji sana duma ya mshambuliaji wa Azam FC, Prince Dube. Wanaamini Dube anaweza kuwa mtu sahihi wa kuziba nafasi ya Fiston Mayele. Inaaminika kwamba Yanga wamekuwa wakihangaika kumshawishi mchezaji huyo kwa muda mrefu kutua katika kikosi hicho kutokana na uwezo wake. . Hivi karibuni wakati Azam FC ikiwa mikoani kwa mechi za Ligi Kuu, Dube alionekana kwenye Uwanja wa Mkapa akishuhudia mechi ya Yanga ambapo ilishinda mabao 4-0 dhidi ya CR Belouizdad. Dube hakusafiri na Azam kwa sababu ni majeruhi ambapo amekosa michezo kadhaa hadi sasa. . Nyota huyo hajacheza mechi ya Azam FC tangu Februari 19 alipoingia kipindi cha pili dhidi ya Tabora United. Hakusafiri na timu katika mechi mbili za mikoani Mbeya dhidi ya Prisons na Mwanza dhidi ya Singida. Lakini ARENA ltuajua kwa kawaida Azam FC husafiri na wachezaji wake hata kama ni majeruhi kama sehemu ya kujenga umoja. Hata hivyo Dube hakusafiri ikisemekana ali

PAUL Makonda "Dhuluma Ikimekidhiri Kwenye Ardhi, Tunafurahishwa na Ajicho Kifanya Jerry Slaa"

PAUL Makonda "Dhuluma Ikimekidhiri Kwenye Ardhi, Tunafurahishwa na Ajicho Kifanya Jerry Slaa" Katibu wa NEC Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa CCM Taifa, Paul Makonda amesema kwa kiwango kikubwa dhuluma imekithiri Nchini na Watanzania wengi wameumizwa na dhuluma hususani katika sekta ya ardhi ambako imekithiri zaidi. Akiongea na Waandishi wa Habari leo Dar es salaam, Makonda amesema ———> “Dhuluma hii imegawanyika katika maeneo mengi au imegawanyika kwenye sekta nyingi na kama Chama tunao wajibu wa kuweka mkazo kwa kuisimamia na kuielekeza Serikali ili ipambane na dhuluma zinazowatesa na kuwaumiza Wananchi hasa walio wanyonge” “Ipo dhuluma kubwa sana kwenye sekta ya ardhi, huko kumekithiri, kilio cha Watu kunyang’anywa maeneo yao na wenye nguvu ya fedha imetawala, kilio cha Watu kupewa nyaraka au hati feki kimetawala na katika eneo hili tulitoa maelekezo mahususi tarehe 19 February 2024, kama Idara ya Itikadi na Mafunzo tunatiwa moyo na jitihada zinazochukuliwa na Waziri

Hiki Hapa Kikosi Cha Wananchi Kinachokwea Pipa Kuelekea Algeria

KIKOSI cha Wananchi, Young Africans SC kinachokwea pipa kuelekea Algeria kwa ajili ya mchezo wa marudiano wa fainali ya kombe la shirikisho Afrika dhidi ya USM Alger utakaopigwa Juni 3, 2023. nyandichethedreamtz

Kocha Wa Manchester City Pep Guardiola Atwaa Tuzo Ya Kocha Bora Wa Mwaka Wa LMA

Kocha wa Manchester City Pep Guardiola. Kocha wa Manchester City Pep Guardiola amechaguliwa kuwa kocha bora wa mwaka na Chama cha makocha wa Ligi. Hii ni mara ya tatu kwa Guardiola kutwaa Tuzo hiyo inayoitwa ‘Sir Alex Ferguson Award’, iinayopigiwa kura na mameneja ama makocha wa madaraja yote ya ligi nchini England. Mhispania huyo, 52, pia alishinda tuzo ya kocha ama meneja bora wa mwaka wa ligi kuu England baada ya timu yake kunyakua taji la tatu mfululizo na la tano katika misimu sita. Kocha wa Chelsea, Emma Hayes alishinda kwa upande wa Ligi ya Wanawake ya Super League. Ilikuwa tuzo yake ya nne mfululizo na ya sita kwa jumla. Guardiola amekuwa meneja wa tatu kushinda tuzo tatu au zaidi za kocha bora wa mwaka wa LMA, sawa na David Moyes, lakini bado yuko ya kocha wa zamani wa Manchester United Sir Alex Ferguson mwenye tuzo 5. City watamenyana na Manchester United katika fainali ya Kombe la FA Jumamosi. Ushindi katika mechi hiyo unaweza kuipa nafasi ya City kushinda makombe matatu

#Exclusive Video: Jokate Afichua Ya Ujauzito Wake, Mtoto Aliyemuokota – ”Ningeweza Kujificha”…

Mkuu Wa Wilaya ya Korogwe, Jokate Mwegelo ameweka wazi kuwa anafurahishwa na kitendo cha yeye kuitwa mama kwani ni steji aliyokuwa akiiogopa sana, ila kwa sasa anaongozwa na neno la Mungu na hivyo hana wasiwasi kwani yupo wa kumshindia katika maisha yake. Aidha Jokate ameongeza kuwa suala la yeye kuwa mama au wamama wengine kote duniani ni jambo la kumshukuru Mungu kwani daktari wake mmoja alimueleza kuwa kwa siku moja watu takribani 30 hufika hosptali kutafuta watoto. nyandichethedreamtz

Martha Mwaipaja – UNASEMA NINI (Official Video)

Muimbaji wa Nyimbo za Injili hapa nchini Martha Mwaipaja, Ameachia ngoma yake mpya inayokwenda kwa jina la-Unasema Nini. nyandichethedreamtz

Real Madrid Na Man United Zaongoza Orodha Ya Klabu Zenye Thamani Zaidi Duniani

Manchester United ndio klabu yenye thamani kubwa zaidi katika ligi ya Premier, kulingana na orodha iliyotolewa na tovuti ya biashara ya Forbes Jumatano. United, yenye thamani ya $6bn (£4.8bn), ni ya pili kwenye orodha nyuma ya Real Madrid ya Uhispania $6.07bn – mara ya kwanza klabu mbili kuwa juu ya $6bn. Liverpool, Manchester City, Chelsea, Tottenham Hotspur na Arsenal pia wameingia 10 bora. Thamani ya Forbes kwa Manchester United imeongezeka kwa 30% tangu mwaka jana. Klabu hiyo ya Old Trafford iliuzwa na familia ya Glazer mwezi Novemba, huku benki ya Qatar Sheikh Jassim bin Hamad Al Thani na Ineos Group ya Sir Jim Ratcliffe wakiwasilisha ombi la kuinunua United. Real ilishika nafasi ya kwanza kuanzia 2022 huku ikiongeza thamani yake kwa 19%, huku wapinzani wao Barcelona wakiwa katika nafasi ya tatu wakiwa wameongoza orodha hiyo mwaka 2021. Tangu Forbes waanze kuchapisha orodha ya timu zenye thamani kubwa zaidi za kandanda duniani mwaka 2004, ni Real Madrid na Manchester Unit