Posts

Showing posts from October, 2019

‘Ugonjwa wa Zari’ Wahamia Kwa Mama Diamond

Image
NancyTheDreamtz ULE ‘ugonjwa’ wa show-off (kujionesha na kuringishia) magari ya kifahari anaodaiwa kuwa nao mwanamama mjasiriamali wa Uganda, Zarinah Hassan ‘Zari The Boss Lady’, umehamia kwa mama wa staa wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’, Sanura Kassim ‘Mama D’. Zari ambaye amezaa watoto wawili na Diamond au Mondi amekuwa akisifika kwa kutupia picha mitandaoni akipozi na magari makali ikielezwa kuwa huwa analenga kuwarusha roho mahasimu wake. Sasa ishu hiyo imehamia kwa Mama D au Mama Dangote ambaye naye kwa siku kadhaa amekuwa akitupia picha za magari ya kifahari yanayomilikiwa na familia yake. Mama Dangote naye inasemekana amekuwa akifanya hivyo kama sehemu ya kuwaziba midomo wanaozusha mambo mengi kuhusu familia yake. Kwa sasa Mama Dangote siyo yule wa zamani aliyeonekana kutoka familia isiyokuwa vizuri kipesa ambapo sasa ‘anakomoa’ baada ya mwanaye kupata utajiri. Mama Dangote na Mondi wamekuwa bega kwa bega tangu staa huyo alipoanza kupata umaarufu yapata

Mbwana Samatta arahisishiwa kazi kwa mabeki wa Liverpool

Image
NancyTheDreamtz Mshambuliajiwa KRC Genk, Mbwana Samatta atakuwa katika wakati mzuri wa kuonesha uwezo wake mbele ya mabingwa watetezi wa michuano ya Klabu Bingwa Ulaya, Liverpool baada ya safu yao ya ulinzi kupungua nguvu. Mchezo huo wa tatu hatua ya makundi unatarajia kupigwa leo katika uwanja wa Luminius Arena mjini Genk, nchini Ubelgiji, ambako ndiyo maskani ya klabu hiyo anayokipiga nahodha wa Taifa Stars. Taarifa zilizopo hii leo zinaeleza kuwa mlinzi machachari wa upande wa kulia wa Liverpool, Trent-Alexander Anold hajafanya mazoezi na klabu yake kutokana na kukumbwa na homa, hivyo hatokuwa sehemu ya kikosi kitakachocheza dhidi ya Genk. Genk ya Mbwana Samatta iko katika kundi E ikiwa na pointi moja katika nafasi ya mwisho baada ya kufungwa mechi moja na kutoka sare mechi moja. Napoli inaongoza kundi hilo ikiwa na pointi 4, huku Liverpool ikiwa na pointi 3 katika nafasi ya pili na Red Bull Salzburg ikiwa katika nafasi ya tatu kwa pointi 3.

WhatsApp Yamponza Askari Magereza Apolwa Siraha Kisa Kuchart

Image
NancyTheDreamtz Askari wa Jeshi la Magereza nchini Uganda wanachunguza tukio la Afisa Mwanamke wa Gereza aliyeibiwa silaha ya kivita aina ya AK-47 wakati akiwa katika Gereza la Mpigi. Afisa aliyeibiwa ametambulika kwa majina ya Hadijah Katono ambaye imeelezwa kuwa wakati akiibiwa silaha hiyo alikuwa akipiga soga katika mtandao wa WhatsApp. Mashuhuda wameeleza kuwa kijana mmoja aliyekuwa ameshika mkuki alimshambulia afisa huyo kwa kumpiga mara mara kisha akachukua silaha na kutimua mbio.

Simba na Azam Kibaruani Leo Kusaka Point Tatu

Image
NancyTheDreamtz LEO uwanja wa Taifa Simba na Azam zitakuwa kazini kusaka pointi tatu muhimu. Wachezaji wanne wataukosa mchezo huu kutokana na sababu mbalimbali ambapo kwa Simba nyota hawa watakosekana leo John Bocco ameanza mazoezi mepesi ila leo hatacheza kwa kuwa hayupo fiti. Jonas Mkude na Mohamed Hussein 'Tshabalala' wanatibu majeraha waliyoyapata kwenye timu ya Taifa. Kocha Mkuu wa Simba, Patric Aussems amesema kuwa atatafuta mbadala wao kwani ana kikosi kipana. Kwa upande wa Azam FC wao hawana majeruhi kabisa isipokuwa ni maamuzi ya Kocha kuamua kumtumia nahodha Agrey Moris ambaye ametoka kupona majeraha yake muda si mrefu. NOMA ZAIDI YA NOMA TAZAMA ROSA REE ALICHOKIFANYA KWA VIDEO:

IRENE Uwoya "Roho Inaniume Sana Kwa Mwanangu Kutukanwa Mitandaoni"

Image
NancyTheDreamtz "Hakuna kitu kinachoniuma kama kutukaniwa mwanangu huwa naumia sana inafikia kipindi naogopa kumpost mitandoni japo Krish mwenyewe huwa nachukia nisipopost picha yake" Ameyasema hayo UWOYA alipoojiwa na Zamaradi

Top 5 ya Wasanii Matajiri Africa, Diamond Hayupo...Why?

Image
NancyTheDreamtz Mimi sio shabiki wa mambo ya muziki wa Tanzania, ila napenda sana kuingia mitandaoni na sifa anazopewa Diamond ni nyingi sana. Ila nimejiuliza, baada ya pitapita zangu nimekutana jarida maarufu Marekani la Forbes limetaja wasanii matajiri zaidi Barani Africa ila cha kushangaza Diamond sijamuona kabisa, shida nini? Nikaendelea kucheki hadi Top-Ten jamaa hayupo ila Wizkid & Davido wapo. Au uwa ni kiki tu na maisha ya kuigiza

Samatta atuma salamu za ushindi Taifa Stars

Image
NancyTheDreamtz Nahodha na mshambuliaji wa kikosi cha taifa Stars Mbwana Ally Samatta amewapongeza wachezaji wa timu hiyo, kwa kufanikisha lengo la kufuzu fainali za mataifa bingwa ya Afrika “CHAN” kwa kuifunga Sudan mabao mawili kwa moja mjini Khartoum, jana usiku. Samatta ambaye hakuwepo kikosini hiyo jana kufuatia kanuni za michuano ya CHAN kumnyima nafasi ya kushiriki, ametoa pongezi hizo kupitia ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa Twitter. Kanuni za michuano ya CHAN zinawabana wachezaji wanaocheza nje ya ligi za nyumbani kwao kushiriki kwenye vikosi vyao, kwa kusudio la kuwapa fursa wachezaji wanaocheza ligi za ndani, kuonekana kimataifa. Mshambuliaji huyo ambaye anaitumikia klabu ya KRC Genk ya Ublegiji ameandika, “Heshima kubwa mmetupa watanzania, nasimama kwa heshima, navua kofia yangu nawapigia saluti ya heshima, asante sana @TaifaStars na hongereni kwa kufuzu kwenye michuano ya CHAN 2020, na kama ilivyo ada basi hapo hapo Sudan anzeni kunywa izo koka bili juu yangu

Kwa Ishu ya King Bae Unajitekenya na Kucheka Mwenyewe!

Image
NancyTheDreamtz Z ARINAH  Hassan ‘The Boss Lady’ ni miongoni mwa wanamama maarufu Afrika Mashariki ambaye kwa namna moja au nyingine, umaarufu wake umekua zaidi baada ya kukutana na kuzaa watoto na mkali wa Bongo Fleva, Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’.   Wakati penzi lake na Diamond au Mondi linachipukia, watu wengi hususan Wabongo walikuwa hawamjui kivile. Baada ya kuanza uhusiano na Mondi ndipo watu sasa wakaanza kumfuatilia na kujua shughuli zake licha ya kuwa kwenye uhusiano huo bado kulikuwa na maswali mengi yaliyokosa majibu kwa mrembo huyo. Watu walikuwa wakihoji kwenye kurasa zake za mitandao ya kijamii anajinasibu na magari mengi ya kifahari yenye namba zilizosomeka Zari1, Zari2 na mengine kibao, je, yalikuwa ni ya kwake kweli kwa maana ya kumiliki au la? Achana na hilo, kuna lile suala la shule na maduka anayodaiwa kumiliki nchini Afrika Kusini ‘Sauz’ bado na vyenyewe vilikuwa ni kitendawili. Hakuna aliyeweza kutegua moja kwa moja kama ni kweli anamiliki au la. Kam